Mtu huyu Eddo Kumwembe

ebaeban

JF-Expert Member
Jan 15, 2012
2,205
2,690
Huyu Eddo Kumwembe.


Huyu Edo Kumwembe jinsi anavyonikoroga mimi katika makala zake Fulani Fulani ni hivyo hivyo angemkoroga na Advocate Kumwembe, nimeisha muonya mala nyingi lakini mbishi, hasa katika suala la kuwalinganisha King Pele na eti akina Messi na mwenzie Ronaldo.


Niliisha mueleza usiwalinganishe hawo vijana na wazee kama akina Pele katika suala la kusakata gozi la nyamafu watu hao wala hawakalibiani, kwa nini huyu kijana mbishi? Mfano katika gazeti la mwanasporti toleo No.1623 la jumamosi tarehe18-19 ukurasa wa 17 katika makala yake nyuma ya pazia Miaka 10 ya Messi Barcelona nyuma ya pazia, amenikera, amenikera, amenikera. Anasema eti nani amemona Pele akicheza, anajibu yeye Hapana , pia Diego Maradona na wengine.


Mimi wachazaji wote uliowataja nimewaona na pia ninaendelea kuwaona wachezaji wa sasa ambao mnasema ni wa kizazi kipya. Nasema hakuna wa kuwalinganisha na akina Pele, hawafikii hata robo. Kwanza huyo Ronaldo hana kipaji chochote zaidi ya mambio afadhari hata Messi.


Tafauti zao kubwa ni hii ifuatayo, kwamba Pele angerudi katika enzi zake anaweza kabisa kucheza na walinzi(Defence) ya wachezaji wa sasa, wakati Messi au Marodana hawawezi kabisa kucheza na walinzi waliokuwa wanamkaba Pele, kwa hakisa akina Messi au Ronaldo wangekutana na walinzi wa akina Pele au wangevunjika vipande vipande au wangeacha kabisa kucheza. Pele angeweza kucheza kipindi hiki cha kizazi kipya lakini Messi wa sasa akutane na walinzi wa zamani haweizi kabisa kufurukuta.


Mfano Mwalimu wa sayansi anaweza kufundisha masomo ya art, wakati mwalimu mahili wa art hawezi kufundisha masomo ya sayansi sasa nani zaidi?


Au Sisi tuliosoma zamani pamoja na advocate Kumwembe tulikuwa tunauwezo wa Ku-calculate Quadratic equation kwa kutumia njia nne yaani Kufactorise, Kutumia master formula, kucomplete the square na kutumia graphing method kwa kutumia rogarismic table wakati hawa akina Edo Kumwembe ambao wanatumia scientific calculator hawawezi kabisa kutumia hizi njia mbili za mwisho, kwa hili sitaki ubishi nimeisha wajaribu sana, sasa jee, katika ya sisi na hawa wanaotumia nyenzo na zaidi? Wakati mimi nikitumia Calculator itakuwa kama nakula nyama ya ubongo tu wenyewe wape Log table hawawezi hata kuitumia sasa je Nani zaidi?
Hebu pimeni kutumia jedwali lifuatalo halafu mumweleze Eddo Kumwembe:-



Kigezo
King Pele
Christiani Ronaldo
Umri wa kuanza kucheza world cup
Miaka 17
Ameanza kijeba
Maback(walinzi)
Walikuwa wanapiga kiatu bila huruma lakini Pele aliweza kucheza
Walinzi wamedhibitiwa kwa sheria kali za kuwalinda mastaa
Viwanja
Vilikuwa vibovu hata hivyo Pele alikuwa anacheza
Viwanja vimeboreshwa sana kiasi unaweza ukasota hata mita 10
Ustadi (skills)
1 A.Mfalme na muasisi wa style zote
1.Tik-taka
2.Guard Muller (zile alikuwaakipiga Tony Yeboah)
3.Scorpion kick
4.Biycle kick ( alikuwa akipiga Bebeto)
4. Vichwa
5.Free Kick
B. Alikuwa anatumia viungo vyote na miguu yote pia mpira uje vyovyote anaumiliki, anaweza kukimbia na mpira ukiwa mbele, nyuma , kichwani hata mgogongoni.
Hana jipya ni mambio tu kama anafukuza paa.







B. Ni mpaka uje kwa mbele tu ndipo akimbie nao nyuma ni mpaka ageuke.Anatumia miguu tu kudrible.
Kucheza Ulaya
King Pele hakuwahi kucheza ulaya kwa sababu alikuwa ni nyara za serikali. Bunge la Brazil lilikaa likaamua Pele hauzwi kwa bei yoyote ni shara ya serikali mpaka alipostaafu ndipo alienda kucheza Amerika (USA)
Amecheza Ulaya kule ndipo akina Edo Kumwembe wanamwona sana na kudhani yeye ni mchezaji .
Mabao
1300 katika mechi za kimataifa
Hata nusu ya Pele hafikii.
Kombe la dunia
Amecheza mala 4. 1958,1962,1966 na 1970 kati ya hapo amenyakua ndoo mala3 na mchazaji bora 1970.
Ameenda mala 3, 2006, 2010, na 2014 mala zote ameenda kuuza magazeti na sura tu.

Ukipekee (unique)
Akiwa na club chake cha Santos huko Columbia Pele alifanya rafu mbaya ya kulipiza kisasi akapewa kadi nyekundu , lakini uwanja mzima uliikata kadi hiyo matokeo yake refa akatolewa Pele akaendelea na mchezo. Hajawahi kufanyiwa mchezaji mwingine tena jambo hilo
Sijui, labda Edo Kumwembe anafahamu.

Edo Kumwembe nakuonya kwa mala ya mwisho usiwalinganishe Pele na Messi au Ronaldo ni ukosefu wa adabu mulio karibu na yeye mumwabie.

 
nimekuelewa makala nimeisoma ila kuna msemo kwamba ukianza kumtafuta nyoka lazima uanzie kwenye miguu yako, yeye kasema hawezi kumpa sifa pele au kumuelezea kiundani wakati kakuta historia tu
 
utangulizi mreeeefu kama jukwaa la katiba mpya na siasa..huku kwenye sports hatujazoea hayo mambo
 
alafu hueleweki..shida yako ni kumjadili edo au kumpambanisha mesi na pele
 
kudos kaka unajua saana mpira,Edo anajua pia lakini inaignore opponents quality which is critical in assessing somebody's strength.mimi nimekuelewa saana.
 
ebaeban Mkuu wewe kweli ni mtu soka japo kwenye mpira kutofautiana ni jambo la kawaida.
 
Last edited by a moderator:
inabidi mods wafungue jukwaa jipya la majivuno....haya tumejua ndugu wewe ni genious
 
Mambo ya baba ake Edo yanakujaje hapa?
Unamuonya kama nani?
Unataka kila MTU afikiri sawa?
Kuna wengine wanáamini ngasa ni zaidi ya mmessi!

Mkuu Mimi umenifurahisha hapo kwenye QUADRATIC tu ingawa si mfano halisi,tuna kila sababu ya kujivunia kizazi hiki cha kina Mess
 
Sisi tuliosoma zamani pamoja na advocate Kumwembe tulikuwa tunauwezo wa Ku-calculate Quadratic equation kwa kutumia njia nne yaani Kufactorise, Kutumia master formula, kucomplete the square na kutumia graphing method kwa kutumia rogarismic table wakati hawa akina Edo Kumwembe ambao wanatumia scientific calculator hawawezi kabisa kutumia hizi njia mbili za mwisho, kwa hili sitaki ubishi nimeisha wajaribu sana, sasa jee, katika ya sisi na hawa wanaotumia nyenzo na zaidi? Wakati mimi nikitumia Calculator itakuwa kama nakula nyama ya ubongo tu wenyewe wape Log table hawawezi hata kuitumia sasa je Nani zaidi?

Nyie watu wa zamani kwa kujikweza tu hamjambo!!

Hamna njia inaitwa master formula, hii njia inaitwa General formula.

Njia nyingine ni hizi hapa

(1) Factorization method

(2) Graphical method. Hapa unachora graphs, baadae unapata majibu kupitia kwenye graphs. Wala hutumii rogarithmic table hapa

(3) Completting the square method
 
Hongera ebaeban, umeenda mbali sana. Hao akina Eddo Kumwembe wacha wachezaji hao waliowataja kwamba hawajawaona, pia akina Sunday Manara, au Kassim Manara wala tu akina Charles Mngodo (kijiko au spoon) hawajawaona na wa hapahapa bongo.

Sasa Ronaldo na Messi wake wachezaji hawa niliowataja hapo juu hawawafikii hata nusu, Ronaldo hamfikii kabisa Kassim Manara kwa kila kitu iwe stamina au ball control wachezaji hao wamecheza miaka ya 70 na 80 mwanzoni, sasa kama hao hawawafikii itakuwaje Eddo awalinganishe na King Pele?

Lazima akina Eddo kwataniuliza swali kama kweli Tanzania imewahi kuwa na wachezaji wenye vipaji kama hao kwa nini soccar lake liko chini namna hii? Jibu kwa maoni yangu:-
Tanzania Soccar limekuwa chini sana kwa sababu kuu mbili.

1. Ule mgogoro mkubwa wa Yanga wa mwaka 1975 ulishusha sana soccar letu, kabla ya hapo africa mashariki tulikuwa hatukamatiki.

2. Utawala wa mpira wa miguu wa Ndolanga na mwenzie Rage ndo ulikuja kuzika kabisa mpira wetu, kwa sababu ndani ya UTAWALA ULE mpira ulikuwa unachezewa guest, uwanjani yalikuwa nai matokeo tu, utawala huo ndio muasisi wa RUSHWA kwenye mpira wa migguu, ni hadi mpira ukichezewa uwanjani ndipo utapanda na si vinginevyo.

Product za utawala ule(RAGE NA NDOLANGA) ni marefa kama akina NJIMBWI ambae Eddo anamfahamu sana. Bandari ya Mtwara mala ya mwisho imepanda daraja siyo kwa kujua kusakata kabumbu bali ni kwa juhudi binafi za referre NJIMBWI.

Sasa na mimi namwuuliza Eddo kwa style hizo za akina NJIMBWI mpira wetu utapanda kweli?
 
Kweli kila nabii na zama zake lakin nabii mwingira hawez wasahaurisha zama za yesu,atolewe refa kwa kadi nyekundu na mashabiki kwa kosa la kumpa ronaldo au mesi kad ndo ndo kidogo wawe ka manara kweli kila ktu hadi usome me nipo tayar kusoma kila utachonifundisha mana unaujua haswa
 
Pele hawafikii hao watu.. Hata kidogo, usilinganishe wachezaji wa Sheria 3 na 17.

Pele sijamwona live ila clip zake nimeziona, ana mpira wa kawaida sana na mabeki na makipa wa wakati ule hawakua na viwango vyovyote, no offsides.. Saivi beki anakuchezea offside trick which means mshambuliaji anatumia akili mingi sana aweze kufunga. Akina Pele walikua wanajifungia tu kama rede
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom