Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Habari zenu wanaJF!
Mimi ni baba wa watoto wawili: mmoja ni wa kike mwenye miaka 9 na mwingine ni wa kiume mwenye miaka mitatu na miezi mitatu. Tatizo lipo kwa huyu wa kiume kwani hadi sasa bado hajaanza kuongea wala kufuata maelekezo ingawa ni mtundu sana. Akiwa na miaka miwili na zaidi tulijaribu kumpeleka kwa madaktari kadhaa ili wamchunguze kama ana tatizo lolote, lakini walitujibu kwamba alikuwa hana tatizo lolote katika afya yake. Anasikia vizuri, ana uzito unaoendana na umri wake, kinywa na koo lake havina matatizo yoyote na hivyo kututaka tuwe na subira kwa vile watoto wanatofautiana katika makuzi hata kama watakuwa wamezaliwa na wazazi haohao. Tangu wakati huo hadi leo hajaongeza chochote kwa matamshi ila anaweza kutamka silabi tu kama ma, ba, bi, ta, sa, si, da, chi, nk bila kuziunganisha wala kudhumunia chochote na kwamba akitaka kitu kama maji anamshika mtu mkono mtu wa karibu yake na kumuelekeza kwenye friji au mtungi wa maji. Anafanya hivyo kwa chakula na mengineyo.
Sasa mimi nina wasiwasi na mwanangu ana tatizo gani linalosababisha achelewe au ashindwe kuongea hadi umri huo? Nawaomba msaada wenu wa kitaalamu au wenye uzoefu na hili mnipe matumaini au uelewa!
Mimi ni baba wa watoto wawili: mmoja ni wa kike mwenye miaka 9 na mwingine ni wa kiume mwenye miaka mitatu na miezi mitatu. Tatizo lipo kwa huyu wa kiume kwani hadi sasa bado hajaanza kuongea wala kufuata maelekezo ingawa ni mtundu sana. Akiwa na miaka miwili na zaidi tulijaribu kumpeleka kwa madaktari kadhaa ili wamchunguze kama ana tatizo lolote, lakini walitujibu kwamba alikuwa hana tatizo lolote katika afya yake. Anasikia vizuri, ana uzito unaoendana na umri wake, kinywa na koo lake havina matatizo yoyote na hivyo kututaka tuwe na subira kwa vile watoto wanatofautiana katika makuzi hata kama watakuwa wamezaliwa na wazazi haohao. Tangu wakati huo hadi leo hajaongeza chochote kwa matamshi ila anaweza kutamka silabi tu kama ma, ba, bi, ta, sa, si, da, chi, nk bila kuziunganisha wala kudhumunia chochote na kwamba akitaka kitu kama maji anamshika mtu mkono mtu wa karibu yake na kumuelekeza kwenye friji au mtungi wa maji. Anafanya hivyo kwa chakula na mengineyo.
Sasa mimi nina wasiwasi na mwanangu ana tatizo gani linalosababisha achelewe au ashindwe kuongea hadi umri huo? Nawaomba msaada wenu wa kitaalamu au wenye uzoefu na hili mnipe matumaini au uelewa!