Mtoto wa Mwaka Mmoja Mwenye Mimba Awashangaza Madaktari China

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
808.jpg


Madaktari nchini China walipigwa na butwaa baada ya kugundua kuwa mtoto wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja, Kang Mengru, ambaye alipelekwa hospitali baada ya tumbo lake kuzidi kuwa kubwa, alikuwa na mimba. GONGA Life Style kwenye menu kushoto kwa habari kamili.

http://www.nifahamishe.com/photos_news.aspx?topic=187
 
huyu mtoto madaktari wanadai mama yake alikuwa na mimba ya mapacha ila pacha wake alijitunga tumboni mwa mwenzake, swali ni kwa nini hao mapacha watofautiane muda kiasi hiki, kwamba mmoja awe ameshazaliwa na mwingine ndio kwanza yupo kwenye hatua ya uumbwaji, na huyo mtoto aliembeba mwenzake anapata hali zilezile ambazo kina mama wajawazito wanazipata kama vile kichefuchefu nk? duh dunia hii kweli mshukuru Mungu kila unapoamka ukiwa mzima coz kuna mambo ambayo yana maswali ila majibu hakuna.
 
Sisemi haiwezi kuwa kweli,kwani katika hii dunia ya Musa kila kitu kinawezekana.Tatizo akili inakataa,kijisayansi changu kidogo nilichonacho pia kinagoma.labda madaktari wachip in watueleze inawezekana vipi hilo kutokea.Maswali ni mengi kuliko majibu.
 
Nina amin hapa yalazima kuna jambo, dunia inazidi kubadilika yawezekanaje suala kama hili, kiutalaamu haliji na hata ki-imani halipo maana hakuna maandiko wala historia inayofanana na hii..hii kiboko. Lakin mi nafikiri tunajambo lakufanya huu ni wakati wakukaa na kumtafakari muumba wetu na hii yote inatotokea ni kwasababu ya uasi tunaoendelea kuufanya kwa kuto tii maangizo ya Mungu na njia Mungu alizotupa katika kumjua yeye. Mungu amekuja dunian kumtafuta mwanadamu na Mwanadamu yuko busy anatafuta njia ya kwenda mbinguni kumtafuta Mungu. Tupunguze uasi
 
imani inakataa kidogo hapa kwa sababu ili mimba iweze kutungwa kuna umri na muda maalumu ambao mwanamke anakuwa ameshabalee, lakini kwa hili kaazi hipo au ndio mambo ya Wachina tena kila kitu FAKE
 
Hizi kamba za wachina kila kitu ni 'fake' kitaalamu hilo haliwezekani. Mtoto ansumbuliwa na ugonjwa fulani hawajaweza kujua, mtoto mwenye kwashakoo kali unaweza kusema an mimba. Wachina ni FAKE!!!!!!!!!!!!!!! hata dunia inatambua hilo.
 
yeah,kimsingi mimba inatungwa ndani ya yai na kisha kutanuka kwenye mfuko wake ndani ya tumbo.Kwa kesi hii ambayo mbegu moja imewahi kutengeneza mtoto na nyingine ikiwa ndani ya mtoto anayekua ikisubiri kurutubishwa inawezekana ila tu hiyo tofauti ya mda inawezekana kwa kuwa joto la mtoto (viungo vyake vya ndani) ni laini kitu ambacho ndani ya mwaka mmoja haikua rahisi kwa ile mbegu kukuzwa ndo maana baada ya mwaka imeanza kukua.....endeleeni na utafiti!
 
Back
Top Bottom