Waziri Mkuu Mizengo Pinda, maarufu kama "Mtoto wa Mkulima," Ijumaa wiki hii (Juni 30, 2011) atahitimisha mjadala wa bajeti ya ofisi yake ya 2011/12 Bungeni. Hii itakuwa ni fursa nzuri kwa Pinda kujibu mapigo kufuatia Waziri Mkuu wa zamani aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond, Edward Lowassa, kuinyooshea kidole serikali ya Rais Jakaya Kikwete na Pinda kuwa inaugua ugonjwa wa kuogopa kufanya maamuzi magumu.
Lowassa, huku akishangiliwa na kundi la wabunge njaa wa CCM wanaomuunga mkono, alijitapa kuwa alipokuwa PM alithubutu kufanya maamuzi magumu kama kuvuta maji kutoka Lake Victoria mpaka mikoa ya kanda ya ziwa licha ya Misri kupinga mradi huo.
Ijumaa itakuwa ni fursa muafaka kwa Pinda kukabiliana na Lowassa moja kwa moja kwa kujibu kitendo chake cha kuifokea serikali eti inashindwa kuthubutu na kufanya maamuzi magumu.
Swali la kujiuliza, Je Pinda ana ubavu (guts) za kumjibu Lowassa au atanywea na kuogopa kupambana naye? Kuna uwezekano kuwa Pinda atawapa mawaziri wa ofisi ya Waziri Mkuu kumjibu Lowassa, badala ya yeye mwenyewe kufanya hivyo ambayo itakuwa ni kosa kubwa la kiufundi na ataonekana kumuogopa Lowassa.
Kama Pinda kweli ni kiongozi makini, atamjibu Lowassa kwa umakini mkubwa na kumwambia kuwa serikali imekuwa ikichukua maamuzi magumu kama kuhakikisha kuwa viongozi wakubwa wakiwemo mawaziri wanaohusishwa na kashfa za ufisadi wanalazimishwa kujiuzulu nafasi zao za uongozi kwenye serikali na chama.
Pinda inabidi aseme sasa serikali imefikia uamuzi mgumu wa kuiruhusu TAKUKURU iwachunguze kikamilifu na kuwafikisha mahakamani viongozi wote wa zamani waliojiuzulu kutokana na tuhuma za ufisadi. Hii ni pamoja na kuwafikisha mahakamani viongozi wa umma wenye utajiri wa mashaka (unexplained wealth) ili waeleze utajiri wameupata kwa njia zipi halali.
Je, Mtoto wa Mkulima yuko tayari kupambana na fisadi Lowassa? Jibu tutapata Ijumaa wiki hii!
Lowassa, huku akishangiliwa na kundi la wabunge njaa wa CCM wanaomuunga mkono, alijitapa kuwa alipokuwa PM alithubutu kufanya maamuzi magumu kama kuvuta maji kutoka Lake Victoria mpaka mikoa ya kanda ya ziwa licha ya Misri kupinga mradi huo.
Ijumaa itakuwa ni fursa muafaka kwa Pinda kukabiliana na Lowassa moja kwa moja kwa kujibu kitendo chake cha kuifokea serikali eti inashindwa kuthubutu na kufanya maamuzi magumu.
Swali la kujiuliza, Je Pinda ana ubavu (guts) za kumjibu Lowassa au atanywea na kuogopa kupambana naye? Kuna uwezekano kuwa Pinda atawapa mawaziri wa ofisi ya Waziri Mkuu kumjibu Lowassa, badala ya yeye mwenyewe kufanya hivyo ambayo itakuwa ni kosa kubwa la kiufundi na ataonekana kumuogopa Lowassa.
Kama Pinda kweli ni kiongozi makini, atamjibu Lowassa kwa umakini mkubwa na kumwambia kuwa serikali imekuwa ikichukua maamuzi magumu kama kuhakikisha kuwa viongozi wakubwa wakiwemo mawaziri wanaohusishwa na kashfa za ufisadi wanalazimishwa kujiuzulu nafasi zao za uongozi kwenye serikali na chama.
Pinda inabidi aseme sasa serikali imefikia uamuzi mgumu wa kuiruhusu TAKUKURU iwachunguze kikamilifu na kuwafikisha mahakamani viongozi wote wa zamani waliojiuzulu kutokana na tuhuma za ufisadi. Hii ni pamoja na kuwafikisha mahakamani viongozi wa umma wenye utajiri wa mashaka (unexplained wealth) ili waeleze utajiri wameupata kwa njia zipi halali.
Je, Mtoto wa Mkulima yuko tayari kupambana na fisadi Lowassa? Jibu tutapata Ijumaa wiki hii!