kapari nesta
Member
- Jul 28, 2015
- 22
- 32
Nawasalimu wote
Nilimuoa mke wangu wakati akiwa na mtoto mkubwa wa darasa la saba, Mimi nimezaa nae watoto wawili, tulifunga ndoa bomani kutokana na utofauti wa dini
Tatizo linaloninyima usingizi ni huyu mtoto wa wife, amekuwa na tabia zisizofaa, wakati tunafunga ndoa makubaliano yalikuwa ni kwamba aje na mtoto wake maana amezoea kuishi nae tangu mchanga.
Baba yake mtoto Alishafariki, nikakubali, miaka minne yote ya sekondari nimekuwa nikiitwa shuleni for serious displinary problems.
Ikiwemo uvutaji bange, hasa alipofika form 3 na kupigana, na kuwa gang leader wa genge lilikuwa linasumbua shuleni kwa utovu wewe nidhamu.
Mwaka Jana huyu mtoto amemaliza form four na alipata zero, baada ya kumaliza shule mwaka jana, tabia yake halisi ndipo ikajitokeza maana alikuwa anashinda nyumbani akisubiri matokeo.
Amekuwa akiuza vitu vya nyumbani mfano alifungua tairi la akiba kwenye gari yangu na ya mama yake akauza, aliiba ndani flat screen na deki zake akaenda kuuza, tulidhani ni vijana wa Mtaani.
Baada ya miezi miwili housegirl akaniambia TV ilichukuliwa na huyu mtoto na akaambiwa angepewa mgao lakini yeye akakataa.
Baadae akaja akaiba motor ya maji ya kupandisha Maji akishirikiana na vijana wa mtaani, ameuza viti vyangu vya plastic zaidi ya Kumi na viwili, alianza kuchukua store kimoja baadae ya kingine, kwa ujumla ameuza vitu vingi sana, achilia mbali simu zetu.
Nimekuwa nikimpa kipigo kizito na kitakatifu kila napogundua kaiba au kafanya tukio, lakini mama yake amekua akiniona mbaya kwa kumuadhibu mwanae, kiasi kwamba ananichunia wiki nzima, hatuongeleshani na ninaambiwa nafanya hivyo kwa kuwa sio mwanangu.
Hata mtoto mwenyewe Mara kadhaa huwa anatamka wazi kwamba usinipige mimi sio mwanao.Sasa nimeshachoka na huyu mtoto na mama yake pia, naishi huku nikificha vitu vyangu nakua sina amani
Wiki tatu zilizopita nilimlaza ndani polisi, baada ya kuiba tsh 500,000 iliyokua kwa bahasha, alipobanwa polisi akakiri na kuonesha ilipo kwa jamaa mmoja Dukani, tangu siku hiyo mama yake kanichunia na tuna ugomvi mkubwa kwa nn nilimpeleka mwanae polisi.
.
Wana Jf nimekata shauri kuacha na na huyu mwanamke ili aondoke na mtoto wake na mimi nibaki na wa kwangu,Nilim treat huyu mtoto kama wa kwangu na kumpa maisha mazuri ili ajione ana baba maana baba yake alifariki long time ago lakini amekua ni kinyume nimetumia njia nyingi bila mafanikio na sasa nimechoka
Ambao hamjaoa msithubutu kabisa kuoa mwanamke aliekwisha kuzaa ni very complicated, mimi nimeyaona, ndugu zangu wengi walipinga mimi nikalazimisha.
Huyu mtoto amesababisha mimi na mama yake kugombana Mara kwa Mara na kufanya ndoa hii kuwa ya mizozo isiyoisha, nimemuomba mama yake atafute pa kumpeleka kama hataki kuishi kulingana na sheria zangu ndani, amedai nimuoneshe pa kumpeleka.
Sasa nitamuonesha majibu kwa kuwatimua, nimeshakata shauri, yaani haya mambo ya familia unaweza kuweuka kwa kweli,inafikia pahala mtoto anauza viatu vya wadogo zake, suti, mapazia, hataki shule hataki chochote.
Najua cha kufanya
Nilimuoa mke wangu wakati akiwa na mtoto mkubwa wa darasa la saba, Mimi nimezaa nae watoto wawili, tulifunga ndoa bomani kutokana na utofauti wa dini
Tatizo linaloninyima usingizi ni huyu mtoto wa wife, amekuwa na tabia zisizofaa, wakati tunafunga ndoa makubaliano yalikuwa ni kwamba aje na mtoto wake maana amezoea kuishi nae tangu mchanga.
Baba yake mtoto Alishafariki, nikakubali, miaka minne yote ya sekondari nimekuwa nikiitwa shuleni for serious displinary problems.
Ikiwemo uvutaji bange, hasa alipofika form 3 na kupigana, na kuwa gang leader wa genge lilikuwa linasumbua shuleni kwa utovu wewe nidhamu.
Mwaka Jana huyu mtoto amemaliza form four na alipata zero, baada ya kumaliza shule mwaka jana, tabia yake halisi ndipo ikajitokeza maana alikuwa anashinda nyumbani akisubiri matokeo.
Amekuwa akiuza vitu vya nyumbani mfano alifungua tairi la akiba kwenye gari yangu na ya mama yake akauza, aliiba ndani flat screen na deki zake akaenda kuuza, tulidhani ni vijana wa Mtaani.
Baada ya miezi miwili housegirl akaniambia TV ilichukuliwa na huyu mtoto na akaambiwa angepewa mgao lakini yeye akakataa.
Baadae akaja akaiba motor ya maji ya kupandisha Maji akishirikiana na vijana wa mtaani, ameuza viti vyangu vya plastic zaidi ya Kumi na viwili, alianza kuchukua store kimoja baadae ya kingine, kwa ujumla ameuza vitu vingi sana, achilia mbali simu zetu.
Nimekuwa nikimpa kipigo kizito na kitakatifu kila napogundua kaiba au kafanya tukio, lakini mama yake amekua akiniona mbaya kwa kumuadhibu mwanae, kiasi kwamba ananichunia wiki nzima, hatuongeleshani na ninaambiwa nafanya hivyo kwa kuwa sio mwanangu.
Hata mtoto mwenyewe Mara kadhaa huwa anatamka wazi kwamba usinipige mimi sio mwanao.Sasa nimeshachoka na huyu mtoto na mama yake pia, naishi huku nikificha vitu vyangu nakua sina amani
Wiki tatu zilizopita nilimlaza ndani polisi, baada ya kuiba tsh 500,000 iliyokua kwa bahasha, alipobanwa polisi akakiri na kuonesha ilipo kwa jamaa mmoja Dukani, tangu siku hiyo mama yake kanichunia na tuna ugomvi mkubwa kwa nn nilimpeleka mwanae polisi.
.
Wana Jf nimekata shauri kuacha na na huyu mwanamke ili aondoke na mtoto wake na mimi nibaki na wa kwangu,Nilim treat huyu mtoto kama wa kwangu na kumpa maisha mazuri ili ajione ana baba maana baba yake alifariki long time ago lakini amekua ni kinyume nimetumia njia nyingi bila mafanikio na sasa nimechoka
Ambao hamjaoa msithubutu kabisa kuoa mwanamke aliekwisha kuzaa ni very complicated, mimi nimeyaona, ndugu zangu wengi walipinga mimi nikalazimisha.
Huyu mtoto amesababisha mimi na mama yake kugombana Mara kwa Mara na kufanya ndoa hii kuwa ya mizozo isiyoisha, nimemuomba mama yake atafute pa kumpeleka kama hataki kuishi kulingana na sheria zangu ndani, amedai nimuoneshe pa kumpeleka.
Sasa nitamuonesha majibu kwa kuwatimua, nimeshakata shauri, yaani haya mambo ya familia unaweza kuweuka kwa kweli,inafikia pahala mtoto anauza viatu vya wadogo zake, suti, mapazia, hataki shule hataki chochote.
Najua cha kufanya