Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Wahenga walisema kuishi kwingi kuona mengi. Nimesikia kisa kimoja huko Arusha cha ajabu sana ambapo mtoto wa miaka 14 (form 2) kapewa mimba na mzungu mwenye miaka 48. Huyu binti alikuwa hajui kwamba ana mimba ila mama yake aliona dalili za ujauzito kwa mwanae akamuweka chini na kuanza kumdadisi. Hapo ndo alipokiri kwamba ana mahusiana na babu mzungu wa miaka 48 anayeendesha biashara ya utalii jijini Arusha. Kichekesho ni kwamba haka kabinti kaliahidiwa CL na blackberi. Mama mtu akawa hajui CL ni nini hadi pale marafiki zake walipomwambia kwamba CL ni viatu. Anyway mzungu kasepa makwao baada ya msako mkali wa polisi. Wanamama wenzangu zungumzeni na watoto wenu mapema. hiki kitoto kicheche kilikuwa kinashinda kwenye internet usiku na mchana kumbe anatafuta makubwa kumzidi kimo kwenye mitandao na kutamani kuwa navyo. Wazazi wake wabebeshwe lawama. wewe tanzania, watoto wadogo hivyo unawaacha na computer 24/7 hivyo si ndo mambo ya kutafuta mambo ya watu wazima ya CL na blackberi ?