Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Kikao hicho kimefanyika lini na wapi?Mtoto wa Rashid Kawawa na mbunge wa CCM Zainab Kawawa amelia machozi katika kikao cha wabunge wa CCM na kusema hii siyo CCM ya baba yake aliyoijua na kwamba hii ni CCM inayoelekea kuzimu kwa vitendo vya ubadhirifu wa mawaziri wake.
Katika hali ya kushangaza wakati akiangua kilio hicho alisema vijana wote aliosoma nao na marafiki zake wanamzomea na kumshangaa kuwa CCM.
Hali hiyo ilisababisha wabunge wenzie ndani ya kikao hicho kupatwa simanzi kubwa na wengine nao walionekana wakifuta machozi.
Source:RAI