BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Mtoto wa Amin amfagilia Nyerere
Thursday, 09 April 2009 16:29
Na Werema Wikori, Butiama
Majira
Thursday, 09 April 2009 16:29
Na Werema Wikori, Butiama
Majira
ENEO la Mwitongo jana lilikumbusha mauaji ya Vita ya Kagera na kifo cha Mwalimu Nyerere, baada ya mtoto wa Rais wa zamani wa Uganda, Idd Amin, Bw. Jaffer Amin kuwasili kijijini hapa na kukumbatiana na Bw. Makongoro Nyerere mbele ya lango kuu la nyumba ya Mwalimu.
Hali hiyo iliwafanya baadhi ya wakazi wa Butiama akiwemo kulengwa na machozi, hivyo kuashiria jambo juu ya ujio wa mtoto huyo wa Amini akiwa ni wa tatu wa kiume katika familia ya watoto 60 wa mtawala huyo wa zamani wa Uganda.
Akizungumza baada ya kupewa nafasi ya kusalimia wananchi waliojitokeza kumpokea katika maadhimisho hayo ya miaka 30 ya Vita ya Kagera, Bw. Jaffer alisema Afrika ina kila sababu ya kujivunia kumpata kiongozi kama Mwalimu Nyerere.
Bw. Jaffer alisema Mwalimu Nyerere alijenga Tanzania ya umoja, mshikamano na maelewano hatua ambayo sasa inawatambulisha kwa lugha moja ya Kiswahili tofauti na ilivyo kwa nchi nyingine za Afrika.
"Ni ukweli usiopingika Mwalimu Nyerere alijenga umoja na kufanya sehemu zote nilizopita kuja hadi hapa Mwitongo kupokelewa vizuri tofauti na baadhi ya watu walivyofikiri," alisema.
Kwa sababu hiyo alisema safari yake kwa mtu aliyemng'oa Baba yake madarakani ni muhimu katika historia kuanza ukurasa mpya na kusahau yote yaliyopita na kujenga mshikamano wa dhati kwa wao, familia, mataifa hayo mawili na Afrika nzima kuacha kulipizana visasi.
Kwa upande wa mtoto wa Nyerere, Bw. Madaraka alisema jambo hilo liliandaliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) kwa kuwakutanisha kwa pamoja ili kuadhimisha miaka hiyo 30 tangu Vita ya Kagera, limejenga nia ya dhati ya umoja na kufanya sasa vizazi kusahau yaliyotekea wakati huo.
Alisema kutokana na kitendo hicho aliitaka jamii kwa nchi hizi mbili kuangalia upya historia kuwa zimetoka wapi na sasa zinakwenda wapi na kwanini zilifika hapo kwa kupanga maisha mazuri baada ya kuteleza wakati huo.
"Pamoja sasa Tanzania na Uganda ni wamoja. Lakini jambo hili limeongeza nguvu katika uhusiano uliopo na kuzidisha na kuweka nia njema kwa nchi zetu. Nawashukuru sana BBC kwa hatua hii," alisema Bw. Madaraka.
Mtoto wa Amin baada ya kuwasili alipelekwa moja kwa moja katika kaburi la Mwalimu Nyerere ambapo aliweka shada la maua na kushiriki ibada fupi ya dini za Kikristo na Kiislamu.