Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,618
- 154,955
COLORADO,Marekani
MTOTO wa kiume raia wa hapa mwenye umri wa miaka 14 anadaiwa kuwaua wazazi wake kwa kuwapiga risasi baada ya kuagizwa kufanya kazi ndogondogo za nyumbani.
Kwa mujibu wa nyaraka za mahakama, mtoto huyo, John Caudle, alikuwa amekasirika kwa siku mbili baada ya kuambiwa na wazazi wake kusafisha chumba chake na kuchambua maharage.
Imeelezwa kuwa baada ya hasira na kusongwa na mawazo zaidi mtoto huyo alimtwanga risasi mama yake, Joanne Rinebarger (38), wakati akiangalia televisheni na kisha kumtwanga risasi ya kisogoni baba yake wa kambo aliyetajwa kwa jina la Tracy wakati akirejea kutoka kazini.
Nyaraka hizo zimeeleza kuwa Caudle alidai kuwa baada ya kufanya mauaji hayo alicheza michezo usiku kucha wakati maiti za wazazi wake zikiwa zimelala sakafuni.
Katika nyaraka hizo za mahakama imeelezwa kuwa ilipofika asubuhi mtoto huyo aliendesha gari la baba yake hadi shuleni ambapo walimu wanasema alikuwa akionekana mwenye furaha kabla ya ndugu zake kuzikuta maiti nyumbani kwao katika eneo la Fairplay, Colorado.
Imeelezwa kuwa licha ya kuwa na umri huo mdogo, Caudle amefunguliwa mashitaki ya mauaji kama watu wazima.
Nyaraka hizo za mahakama zimeeleza kuwa Caudle alidai sababu iliyomfanya kumpiga risasi mama yake, Joanne Rinebarger ni kwa kuwa hakutaka kufanya kazi za nyumbani.
MTOTO wa kiume raia wa hapa mwenye umri wa miaka 14 anadaiwa kuwaua wazazi wake kwa kuwapiga risasi baada ya kuagizwa kufanya kazi ndogondogo za nyumbani.
Kwa mujibu wa nyaraka za mahakama, mtoto huyo, John Caudle, alikuwa amekasirika kwa siku mbili baada ya kuambiwa na wazazi wake kusafisha chumba chake na kuchambua maharage.
Imeelezwa kuwa baada ya hasira na kusongwa na mawazo zaidi mtoto huyo alimtwanga risasi mama yake, Joanne Rinebarger (38), wakati akiangalia televisheni na kisha kumtwanga risasi ya kisogoni baba yake wa kambo aliyetajwa kwa jina la Tracy wakati akirejea kutoka kazini.
Nyaraka hizo zimeeleza kuwa Caudle alidai kuwa baada ya kufanya mauaji hayo alicheza michezo usiku kucha wakati maiti za wazazi wake zikiwa zimelala sakafuni.
Katika nyaraka hizo za mahakama imeelezwa kuwa ilipofika asubuhi mtoto huyo aliendesha gari la baba yake hadi shuleni ambapo walimu wanasema alikuwa akionekana mwenye furaha kabla ya ndugu zake kuzikuta maiti nyumbani kwao katika eneo la Fairplay, Colorado.
Imeelezwa kuwa licha ya kuwa na umri huo mdogo, Caudle amefunguliwa mashitaki ya mauaji kama watu wazima.
Nyaraka hizo za mahakama zimeeleza kuwa Caudle alidai sababu iliyomfanya kumpiga risasi mama yake, Joanne Rinebarger ni kwa kuwa hakutaka kufanya kazi za nyumbani.