Tatizo kubwa la wazazi kususa kuwapeleka watoto shule na kulipia michango ya shule ni matokeo mabovu ya mitihani ya kidato cha nne. Shule zipo katika mazingira magumu yasiyo rafiki ya kielimu, wanafunzi ufaulu unaanzia Daraja la nne na waliobaki wote sifuli. Matokeo ya namna hii hayawezi kumshawishi mzazi kuingia ghalama za kumsomesha mwanae kwani waliomaliza maisha yao hayatofautiani na wale walioishia darasa la saba. Ni wakati wa kutafakari na kuchukua hatua stahili.