Mtoto albino awafukuza waliokata mkono wake

mdau wetu

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
548
58
MLEMAVU wa ngozi aliyekatwa mkono wake wa kulia na watu wasiojulikana, Kulwa Lusana (16), amesimulia alivyojikuta akiwafukuza wavamizi hao, huku akilia na kuwaomba wamrudishie mkono wake.

Kulwa ametoa maelezo hyao Polisi jana na kuongeza kuwa juhudi hizo za kudai kurudishiwa mkono wake, hazikuzaa matunda, kwani wakataji hao walizidi kutokomea gizani na kumuacha akitapatapa.

Baada ya kupoteza matumaini ya kuupata mkono wake, Kulwa alisimulia kwamba akiwa anagugumia kwa maumivu makali, alikimbilia kwenye nyumba ya baba yake ambapo aligongana naye mlangoni na wote kuanguka chini.

Mlemavu huo alifanyiwa unyama huo juzi saa 7 usiku katika Kijiji cha Mbizi, Kata ya Segese wilayani Kahama katika Mkoa wa Shinyanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Diwani Athumani alisema watuhumiwa hao walivunja mlango na kuingia ndani kwa albino huyo na kuanza kumshambulia na kumjeruhi sikio na baadaye wakakata mkono wake wa kulia na kuondoka nao.

Kwa mujibu wa Kamanda Athumani, albino huyo alipiga kelele ya kuomba msaada kwa baba yake, Lusana Nkola ambaye hata hivyo wakati akitoka katika harakati za kumuokoa mtoto wake huyo, alipigwa jiwe kichwani akaanguka chini.

Alisema baada ya kufanyiwa unyama huo, watu hao waliufunga mkono huo kwenye mfuko na kuanza kukimbia nao na kutokomea pasipo julikana na kumuacha albino huyo akigugumia kwa maumivu makali.

Kutokana na tukio hilo, Polisi inamshikilia Petro Nkola mkazi wa kijiji cha Mtukula Runzewe wilayani Bukombe ambaye ni baba mdogo wa mlemavu wa ngozi, Kulwa Lusana (16).

Hata hivyo, Kamanda Athumani hakutaka kueleza kwa undani sababu za kumshikilia baba huyo zaidi ya kufafanua kuwa ni kwa mahojiano zaidi na uwezekano wa kuwapata watuhumiwa wengine waliotoroka na mkono wa mlemavu huyo.

Kulwa kwa sasa yupo katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama akiuguza jeraha lake na hali yake inaendelea vizuri.

Kamanda Athumani aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa watu wote watakaowadhani kuwa ni washiriki wa tukio hilo la kinyama alilofanyiwa mtoto huyo.

Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku chache tu baada ya mlemavu mwingine wa ngozi, Adam Robert (14) kujeruhiwa kwa kukatwa na sime mkono wa kushoto na kunyofolewa vidole vya mkono wa kulia huko katika Kijiji cha Nyaruguguna wilayani Geita, mkoani Mwanza.

Katika tukio hilo la Geita, baba mzazi na mama wa kambo wa mtoto huyo, wanashikiliwa kwa tuhuma hizo.
 
MLEMAVU wa ngozi aliyekatwa mkono wake wa kulia na watu wasiojulikana, Kulwa Lusana (16), amesimulia alivyojikuta akiwafukuza wavamizi hao, huku akilia na kuwaomba wamrudishie mkono wake.

Kulwa ametoa maelezo hyao Polisi jana na kuongeza kuwa juhudi hizo za kudai kurudishiwa mkono wake, hazikuzaa matunda, kwani wakataji hao walizidi kutokomea gizani na kumuacha akitapatapa.

Baada ya kupoteza matumaini ya kuupata mkono wake, Kulwa alisimulia kwamba akiwa anagugumia kwa maumivu makali, alikimbilia kwenye nyumba ya baba yake ambapo aligongana naye mlangoni na wote kuanguka chini.

Mlemavu huo alifanyiwa unyama huo juzi saa 7 usiku katika Kijiji cha Mbizi, Kata ya Segese wilayani Kahama katika Mkoa wa Shinyanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Diwani Athumani alisema watuhumiwa hao walivunja mlango na kuingia ndani kwa albino huyo na kuanza kumshambulia na kumjeruhi sikio na baadaye wakakata mkono wake wa kulia na kuondoka nao.

Kwa mujibu wa Kamanda Athumani, albino huyo alipiga kelele ya kuomba msaada kwa baba yake, Lusana Nkola ambaye hata hivyo wakati akitoka katika harakati za kumuokoa mtoto wake huyo, alipigwa jiwe kichwani akaanguka chini.

Alisema baada ya kufanyiwa unyama huo, watu hao waliufunga mkono huo kwenye mfuko na kuanza kukimbia nao na kutokomea pasipo julikana na kumuacha albino huyo akigugumia kwa maumivu makali.

Kutokana na tukio hilo, Polisi inamshikilia Petro Nkola mkazi wa kijiji cha Mtukula Runzewe wilayani Bukombe ambaye ni baba mdogo wa mlemavu wa ngozi, Kulwa Lusana (16).

Hata hivyo, Kamanda Athumani hakutaka kueleza kwa undani sababu za kumshikilia baba huyo zaidi ya kufafanua kuwa ni kwa mahojiano zaidi na uwezekano wa kuwapata watuhumiwa wengine waliotoroka na mkono wa mlemavu huyo.

Kulwa kwa sasa yupo katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama akiuguza jeraha lake na hali yake inaendelea vizuri.

Kamanda Athumani aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa watu wote watakaowadhani kuwa ni washiriki wa tukio hilo la kinyama alilofanyiwa mtoto huyo.

Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku chache tu baada ya mlemavu mwingine wa ngozi, Adam Robert (14) kujeruhiwa kwa kukatwa na sime mkono wa kushoto na kunyofolewa vidole vya mkono wa kulia huko katika Kijiji cha Nyaruguguna wilayani Geita, mkoani Mwanza.

Katika tukio hilo la Geita, baba mzazi na mama wa kambo wa mtoto huyo, wanashikiliwa kwa tuhuma hizo.



hivi watanzania, hii aibu ya kuua albino itaisha lini??????????????????????????? hivi inaingia akilini kweli??????????????????? shame on you all wenye mawazo ya kishirikina. Bwana na awafunue akili zenu
 
Waganga wa kienyeji wanajulikana na wanatumiwa na baadhi ya wenye uchu wa mali na baadhi ya wenye uchu wa madaraka.
 
hivi zile kesi za walio ua albino zilizo kuwa zinendelea wkt ule
ziliishia wapi?? au ndio ziliishia juujuu tu???
ingetolewa adhabu kali kwa wanao fanya uhalifu huo labda ingesaidia
kukomesha vitendo hivi.
 
hivi zile kesi za walio ua albino zilizo kuwa zinendelea wkt ule
ziliishia wapi?? au ndio ziliishia juujuu tu???
ingetolewa adhabu kali kwa wanao fanya uhalifu huo labda ingesaidia
kukomesha vitendo hivi.

mkuu walipata adhabu ya kifungo cha maisha,lakini wa2 hawakomi na hawana huruma.
 
hivi watanzania, hii aibu ya kuua albino itaisha lini??????????????????????????? hivi inaingia akilini kweli??????????????????? shame on you all wenye mawazo ya kishirikina. Bwana na awafunue akili zenu

ni aibu kweli, kule kenya jokes za albino huwa wanaambiwa kuwa watapelekwa tanganyika!
 
kuna walakini ktk uhusika wa wakubwa ktk hili
ngekuwa jaji nawahukumu kuuwa kwa kupigwa mawe
tena mbele ya halaiki bila kusubiri JK kusaini hati ya kifo
inakera na kuuma kwauamini ushirikina
 
inatisha jmn na inasikitisha Mungu awarehemu nakuwafungua fahamu zao hawa watu mweee!
 
Haina haja ya kuwapeleka huko
mahakamani na nyie mnamkata kiungo kimoja baada ya kingine ndo wajue maumiv wanayoyapata wenzao pumbav kabisa!
Ni kama wale wanaopiga wenzao nondo yaani ushirikina ni jambo la hovyo sana.na hawa waganga nao ua kabisa ndo chanzo cha uhayawani huu
 
hii mijitu ya kanda ya ziwa (shinyanga na mwanza) ilifaa wayahamishe yote wapelekwe either kwa alshabab maana inatutia aibu ya karne wabongo au serikali wahamishe watu wa kusini na kaskazini na kuwapeleka huko na wao kuwapunguza mikoa mingine ili kudilute tabia zao za hovyohovyo
 
hii mijitu ya kanda ya ziwa (shinyanga na mwanza) ilifaa wayahamishe yote wapelekwe either kwa alshabab maana inatutia aibu ya karne wabongo au serikali wahamishe watu wa kusini na kaskazini na kuwapeleka huko na wao kuwapunguza mikoa mingine ili kudilute tabia zao za hovyohovyo

masaburi yao hawa si ndo wanauaga
vikongwe wenye macho mekundu!
Hivi huyu kijana anaeuwa!!
Anakumbuka kuwa nayeye anaelekea ukikongwe?so nayeye
huko mbele auwawe??
Pmbav kabisa alaaaa.
 
labda ni dawa za kumaliza kesi za mafisadi maana hukumu inasusua sana na adhabu ni ndogo, dawa ni kuwapiga mawe hadi kufa
 
Back
Top Bottom