To be honest, hii picha inasikitisha na inatoa ujumbe mkubwa sana kuhusu jamii tunamoishi!! Ukimwangalia mtoto aliyebebwa ana afya njema, ni msafi na amevaa viatu, kwa hiyo hawa sio masikini wa kupindukia.
Ila mtoto aliyembeba anaonekana mchafu na asiye na matumaini katika maisha. Sura yake inaelezea masaibu mengi aliyonayo katika maisha.
Nikifikiria kwa haraka haraka ni kwamba mtoto huyu aliyembeba mwenzake atakuwa analelewa na mama wa kambo, ama ni yatima aliyekosa mwelekeo wa maisha na kuambulia kupewa ajira ya watoto. Usishangae kwa Tanzania kwamba mtoto huyo aliyembeba mwenzake akawa ni ''housegirl'' wa mtu anayefanya kazi ofisini na amesoma shule kabisa !