MPIGA ZEZE
JF-Expert Member
- May 16, 2011
- 2,539
- 2,296
Na hili ni swali la papo kwa papo kwa Mhe waziri Mkuu, Dkt Kayanza Pinda.
Zama za kale wahenga walinena kwamba ngoma ikipigwa Unguja, Bara hucheza (enzi zile za utawala wa Waarabu, Unguja ndicho kilikuwa kitovu cha utawala na uchumi). Hapana ubishi, zama hizi za leo tunaishi katika dunia tandawazi. Tanzania haiwezi kujidanganya kuwa ni kisiwa, na mintaarafu ukweli huu ni kwamba ngoma ikipigwa Washington, DC, dunia nzima hucheza! Huko DC moto unawaka. Janga la kiuchumi la kutengenezwa liko jikoni. Wademokrati na Warepablikani wameshikana koo juu ya kupandisha paa la deni la taifa (national debt ceilling). Wasipoafikiana ifikapo Agosti 2, 2011 wataalamu wa uchumi na siasa wanatabiri kwamba taifa la Marekani litakumbwa tena na mporomoko mkali wa kiuchumi kuliko hata ule wa 2008. Na Marekani ikiyumba, dunia nzima inayumba mtikisiko wa pili wa kiuchumi duniani katika kipindi kisichozidi miaka mitano. Serikali za majimbo ya Marekani zimeanza kuchukua tahadhari iwapo janga hili litatokea.
Swali: je serikali yetu ya JMT ina habari kuhusu uwezekano wa kutokea janga hili? Kama jibu ni ndiyo, imechukua hatua gani za tahadhari? Na imeundaaje umma angaa kihisia iwapo janga litatokea? AU tunasubiri mtikisiko utokee halafu tuunde TUME?
Zama za kale wahenga walinena kwamba ngoma ikipigwa Unguja, Bara hucheza (enzi zile za utawala wa Waarabu, Unguja ndicho kilikuwa kitovu cha utawala na uchumi). Hapana ubishi, zama hizi za leo tunaishi katika dunia tandawazi. Tanzania haiwezi kujidanganya kuwa ni kisiwa, na mintaarafu ukweli huu ni kwamba ngoma ikipigwa Washington, DC, dunia nzima hucheza! Huko DC moto unawaka. Janga la kiuchumi la kutengenezwa liko jikoni. Wademokrati na Warepablikani wameshikana koo juu ya kupandisha paa la deni la taifa (national debt ceilling). Wasipoafikiana ifikapo Agosti 2, 2011 wataalamu wa uchumi na siasa wanatabiri kwamba taifa la Marekani litakumbwa tena na mporomoko mkali wa kiuchumi kuliko hata ule wa 2008. Na Marekani ikiyumba, dunia nzima inayumba mtikisiko wa pili wa kiuchumi duniani katika kipindi kisichozidi miaka mitano. Serikali za majimbo ya Marekani zimeanza kuchukua tahadhari iwapo janga hili litatokea.
Swali: je serikali yetu ya JMT ina habari kuhusu uwezekano wa kutokea janga hili? Kama jibu ni ndiyo, imechukua hatua gani za tahadhari? Na imeundaaje umma angaa kihisia iwapo janga litatokea? AU tunasubiri mtikisiko utokee halafu tuunde TUME?