Mtikisiko sakata la elimu bure: Wakuu wa shule wagoma kuchukua mgao wa serikali, mambo yamekwama!

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Sakata la elimu ya bure kama inavyonadiwa na serikali ya CCM linaweza kuisambaratishia mbali elimu ya Tanzania kama serikali itaendelea kuja na misimamo iliyo nayo sasa!

Mashule mengi mambo yamesimama, wakuu wa shule wanapewa shilingi 30000 hadi 2000 as Kitanzania kuendesha shule!

Mathalan shule moja iliyopo Manyara mkuu wa shule amepewa 2000 kuendesha gharama zote za mambo ya utawala ikiwemo kununua vitendea kazi! Kabla ya sera 'mbovu' ya CCM kutekeleza elimu bure, shule hiyo 90% ya waalimu wake walikuwa wa kujitolea huku wakilipwa na michango ya wazazi. Kwa sasa shule hiyo imebaki na mkuu wa shule pamoja na waalimu wawili wote wakiwa ni wa masomo ya arts baada ya wale wa kujitolea kuachishwa na sera ya "elimu bure" kwa sasa wanafunzi wanaingia madarasani kutazama tu kuta za shule na paa huku wakiifaidi vilivyo elimu bure bila gharama! Huo ni mfano mmoja miongoni mwa shule lukuki sana ambazo siwezi kuziorodhesha hapa kutokana na muda ila zinaonekana na kila mtu!

Asilimia 90 ya shule zote Tanzania zimekwama kwa kiwango cha juu kuliko kawaida! Hizo asilimia 10 zilizobaki zimeamua kujiendesha na kuipuuzilia mbali sera ya midomoni ya CCM ya elimu bure! Wazazi wameamua kushikamana na waalimu kuendesha shule zao ili watoto wao wafanikiwe!

Mtihani matokeo yakiwa mabaya mawaziri watakutana kutoa matamko na kutisha waalimu pamoja na kutekeleza ile kauli yao ambayo mimi sipendi kuitumia ya majipu! Ila CCM ikumbuke kuwa hao 10% walioipuuza sera ya CCM watakuwa tofauti sana hawa ni pamoja na wale wa shule binafsi wanaojiendesha! Wale 90% watoto watarudi nyumbani huku ndani ya 'visiku ' vichache serikali ikitoa matamko kutafuta mchawi! Baada ya hapo ni biashara itaendelea kama kawaida!

Shule hazifundishi mambo hayaendi na muda unasonga! NECTA watatoa mtihani kwa hao wa shule za wale kutoka 10% za walioipuuza sera mbovu ya CCM, watatoa kwa wale 90% wanaofaidi 'elimu bure ya kutazama kuta za madarasa pamoja na mapaa' Pia watatoa mtihani huohuo kwa akina Feza schools na st. Marian na wengineo! NECTA itawapima katika mzani mmoja!

Mheshimiwa Simbachawene endelea kutoa matamko!

Waziri wa elimu na naibu waendelee kuhubiri elimu bure! Huko mashuleni itatekelezwa ila "Mchimba kaburi haingii yeye"

Elimu bure ingetekelezeka kama kungekuwa na misingi thabiti lakini siyo haya maigizo yaliyokithiri yanayoendelea kwa sasa!

Unampa mkuu wa shule shilingi 3000 aendeshe shule huku ukimpa matamko yanayopishana masikioni mwake Eti ole wako ufanye hivi ole wako itokee vile ole wako sijui nini.....!


Narudia tena "mchimba kaburi humtia mtuwe"
 
Sakata la elimu ya bure kama inavyonadiwa na serikali ya CCM linaweza kuisambaratishia mbali elimu ya Tanzania kama serikali itaendelea kuja na misimamo iliyo nayo sasa!

Mashule mengi mambo yamesimama, wakuu wa shule wanapewa shilingi 30000 hadi 2000 as Kitanzania kuendesha shule!

Mathalan shule moja iliyopo Manyara mkuu wa shule amepewa 2000 kuendesha gharama zote za mambo ya utawala ikiwemo kununua vitendea kazi! Kabla ya sera 'mbovu' ya CCM kutekeleza elimu bure, shule hiyo 90% ya waalimu wake walikuwa wa kujitolea huku wakilipwa na michango ya wazazi. Kwa sasa shule hiyo imebaki na mkuu wa shule pamoja na waalimu wawili wote wakiwa ni wa masomo ya arts baada ya wale wa kujitolea kuachishwa na sera ya "elimu bure" kwa sasa wanafunzi wanaingia madarasani kutazama tu kuta za shule na paa huku wakiifaidi vilivyo elimu bure bila gharama! Huo ni mfano mmoja miongoni mwa shule lukuki sana ambazo siwezi kuziorodhesha hapa kutokana na muda ila zinaonekana na kila mtu!

Asilimia 90 ya shule zote Tanzania zimekwama kwa kiwango cha juu kuliko kawaida! Hizo asilimia 10 zilizobaki zimeamua kujiendesha na kuipuuzilia mbali sera ya midomoni ya CCM ya elimu bure! Wazazi wameamua kushikamana na waalimu kuendesha shule zao ili watoto wao wafanikiwe!

Mtihani matokeo yakiwa mabaya mawaziri watakutana kutoa matamko na kutisha waalimu pamoja na kutekeleza ile kauli yao ambayo mimi sipendi kuitumia ya majipu! Ila CCM ikumbuke kuwa hao 10% walioipuuza sera ya CCM watakuwa tofauti sana hawa ni pamoja na wale wa shule binafsi wanaojiendesha! Wale 90% watoto watarudi nyumbani huku ndani ya 'visiku ' vichache serikali ikitoa matamko kutafuta mchawi! Baada ya hapo ni biashara itaendelea kama kawaida!

Shule hazifundishi mambo hayaendi na muda unasonga! NECTA watatoa mtihani kwa hao wa shule za wale kutoka 10% za walioipuuza sera mbovu ya CCM, watatoa kwa wale 90% wanaofaidi 'elimu bure ya kutazama kuta za madarasa pamoja na mapaa' Pia watatoa mtihani huohuo kwa akina Feza schools na st. Marian na wengineo! NECTA itawapima katika mzani mmoja!

Mheshimiwa Simbachawene endelea kutoa matamko!

Waziri wa elimu na naibu waendelee kuhubiri elimu bure! Huko mashuleni itatekelezwa ila "Mchimba kaburi haingii yeye"

Elimu bure ingetekelezeka kama kungekuwa na misingi thabiti lakini siyo haya maigizo yaliyokithiri yanayoendelea kwa sasa!

Unampa mkuu wa shule shilingi 3000 aendeshe shule huku ukimpa matamko yanayopishana masikioni mwake Eti ole wako ufanye hivi ole wako itokee vile ole wako sijui nini.....!


Narudia tena "mchimba kaburi humtia mtuwe"




Mkuu wakuu wa shule hawawezi kuigomea serikali.
 
Watu Watamkumbuka Mh Lowassa. Huyu Bwana Alikuwa na Maono na Mipango Thabiti ya Kulivusha Taifa Kutoka Chini Kwenda Juu.

Sasa Tunaona Madhara ya Kutokuwa na Mipango, na Kuendelea Kufanya Mambo kwa Kukurupuka Bila Kufanya Upembuzi Yakinifu, kabla ya Kufanya Jambo.
 
Mtoa mada embu punguza mihemko, unachoongea yawezekana ni sawa lakini weka wazi. Jukwaa hili ni la kuelimisha, kukosoa na kufahamisha umma ni kitu gani kinaendelea wapi na katika sector ipi. Acha kujionyesha kama uko against na sera ya elimu bure. Ninachoweza kusema, unapoanzisha jambo na ukaanza kulitekeleza, tegemea changamoto kadha zitajitokeza. Changamoto sio ushetani wala kushindwa kwa sera husika bali zinahitajika kufanyiwa kazi ili mambo yasonge mbele, umetoa mfano wa shule kupewa shilingi 2000, wahusika wanasikia na wanafuatilia, umesema 90% ya shule hazikupewa mgawo, this is sound like liars, jimboni kwangu karibu shule nyingi zimepata mgawo kulingana na idadi ya wanafunzi sasa hizo takwimu zako ziweke sawa ili zisaidie kulipatia ufumbuzi tatizo hilo. This is not non starter, ni changamoto ambazo hata mawaziri husika wameshazizungumzia.
 
Taja shule gani.
Magufuli katumbua jipu.Michango ilikuwa miradi ya kifisadi ya walimu wakuu na kamati za shule ila tutafika tu.Taratibu.
Ni vizuri anayesema hizo pesa ni ndogo atoe ushahidi kwa kuonyesha mchanganuo wa matumizi ya shule husika.Je ni kwa ajili ya kununua vifaa kama chaki? Chaki ni shilingi ngapi kwa mwezi? Je ni kwa ajili ya kununulia peni za walimu za kusahihishia? Ni shilingi ngapi? Vifaa vingi hutolewa na wizara kama vitabu nk WAO KAMA SHULE Matumizi hasa ni yepi? Waweke bayana na yachambuliwe kama yastahili yagarimiwe na shule yenyewe,halmashauri au wizara.

Mtu akileta mchango humu wa kubeza alete na mchanganuo wa kuna gharama gani na kapewa kiasi gani
 
[QUOTEJFK wabongo, post: 15143166, member: 316399"]Ndugu hata uandike kwa kupiga samasoti sera zinazotekelezwa sasa ni za CCM. Makala yako ina mapungufu makubwa ya taarifa na maarifa kwa ujumla.[/QUOTE]
Kwani mimi nimeandika makala! Mimi sera hiyo hainiathiri kwa chochote maana naitambua na nimeshaipuuza! Tusubiri tuone atakayelia na kucheka na huu ushabiki wako!!!
 
Ndugu hata uandike kwa kupiga samasoti sera zinazotekelezwa sasa ni za CCM. Makala yako ina mapungufu makubwa ya taarifa na maarifa kwa ujumla.
sio kila kitu kupinga tu, hata makala ikiwa na mapungufu wazo kuu ni ka kweli 100%
 
Sakata la elimu ya bure kama inavyonadiwa na serikali ya CCM linaweza kuisambaratishia mbali elimu ya Tanzania kama serikali itaendelea kuja na misimamo iliyo nayo sasa!

Mashule mengi mambo yamesimama, wakuu wa shule wanapewa shilingi 30000 hadi 2000 as Kitanzania kuendesha shule!

Mathalan shule moja iliyopo Manyara mkuu wa shule amepewa 2000 kuendesha gharama zote za mambo ya utawala ikiwemo kununua vitendea kazi! Kabla ya sera 'mbovu' ya CCM kutekeleza elimu bure, shule hiyo 90% ya waalimu wake walikuwa wa kujitolea huku wakilipwa na michango ya wazazi. Kwa sasa shule hiyo imebaki na mkuu wa shule pamoja na waalimu wawili wote wakiwa ni wa masomo ya arts baada ya wale wa kujitolea kuachishwa na sera ya "elimu bure" kwa sasa wanafunzi wanaingia madarasani kutazama tu kuta za shule na paa huku wakiifaidi vilivyo elimu bure bila gharama! Huo ni mfano mmoja miongoni mwa shule lukuki sana ambazo siwezi kuziorodhesha hapa kutokana na muda ila zinaonekana na kila mtu!

Narudia tena "mchimba kaburi humtia mtuwe"

MKuu hizi Tarakimu ulizoandika ni sahihi au ni makosa ya kiuandishi tu?????

Mfano 30000 na 2000!!!!!!

Maana ikiwa ni pesa ya kitanzania kiasi kupewa shule ni hatari!!!!!!!

Endapo kama umekosea naomba rekebisha habari isomeke vizuri na endapo kama ni sahihi iache tuelewe kiasi hicho.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Elimu bure ni mkombozi kwa wanyonge, kama kuna changamoto basi zifanyiwe kazi lakini siyo kuitupa idea moja kwa moja
 
Mkuu ni vizuri ukataja na majina ya shule hizo ili wadau waweze kujua,ikiwezekana kuchukua hatua,lakini kwa kusema tu,"shule Fulani" inapunguza uzito wa tatizo, ni mtazamo wangu tu!!!

Huyo jamaa ni kitengo cha propaganda, inaweza kuwa kweli lakini pia ni kisiasa zaidi.
 
Watu Watamkumbuka Mh Lowassa. Huyu Bwana Alikuwa na Maono na Mipango Thabiti ya Kulivusha Taifa Kutoka Chini Kwenda Juu.

Sasa Tunaona Madhara ya Kutokuwa na Mipango, na Kuendelea Kufanya Mambo kwa Kukurupuka Bila Kufanya Upembuzi Yakinifu, kabla ya Kufanya Jambo.
Never ever kumkumbuka huyo
 
Back
Top Bottom