Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa wangu...

Ukweli huu usiopingika ni alama dhahiri umesoma sana mwenendo wa huyu mpigania haki mashuhuri katika nchi hii tangu mfumo wa vyama vingi uingie nchini.

Umashuhuri wake zaidi umejionyesha pale watanzania wengi kutomuunga mkono katika hoja zake kivitendo ingawa zinasomeka wazi ni za msingi na muhimu. Pamoja na kuwa peke yake hakukata tamaa amekuwa mpiganaji kuwashinda wale wa vita vya msituni hadi kuitikisa serikali mahakamani na kuishinda mara kadhaa licha ya vitisho kama katika kesi yake iliyomalizika leo kusingiziwa.

Wanasiasa wengi Tanzania hasa vyama vya siasa hawajaonyesha ushirikiano na mpigania haki huyo kwa kile tulichokizoea kukosa umoja kwa vyama vya upinzania hali ambayo imechelewesha hata mageuzi Tanzania tofauti na nchi kadhaa zinazotuzunguka katika kuendesha wimbi la mageuzi ya kweli kwa kukata mzizi wa fitina unaolindwa na watawala kujizatiti kwa kupokezana vijiti kana hatuna wenye uwezo na nafasi ya kufanya hivyo.

Mtikila udhaifu wake pia wa kutowakubali au kuwapa nguvu wanasiasa wenzake katika vyama vya upinzani huenda ni chanzo cha kutopata ushirikiano wa kutosha, hata hivyo sioni kama hoja ya kutompongeza kwa vile ayafanyayo ni mahsusi kwa demokrasia ya kweli katika nchi yetu, kama wastaarabu na waungwana tuna haki ya kumpongeza kwa nguvu moja kwa ushujaa alio nao, kwani amepigania haki za watanzania wote bila kujibakisha hadi kufikia pengine kuhatarisha usalama wake, ila tegemeo lake kama mchungaji ni Mungu pekee.

Naam, histori haitamwacha mtu huyu mashuhuri katika kutetea demokrasia ya kweli nchini mwetu bila woga, bila kukata tamaa, hadi kuishinda serikali mahakamani mara kadhaa kwa nia moja tu kutetea wanyonge wa taifa letu.

Ipo siku utajengwa mnara wa kumbukumbu yake katika kijiji alichozaliwa kiitwacho Milo kando ya mapangano ya milima ya Livingstone huko Upangwani iliyojipindapinda na magenge mengi kuteremkia bonde kuu la ufa huko Ziwa Nyasa ambako wenyewe wa huko ni sawa na nabii hakosi heshima ila katika nchi yake mwenyewe, aka wilayani Ludewa kwa mwanamapinduzi mwenzake Deo Filikunjombe.

Hakika huyo ni shujaa wetu. Sifa nyingi alizonazo mzalendo huyu na ambazo zimeandikwa katika thred hii mara nyingi hutolewa mtu akifa lakini kwa mchungaji zimetolewa kabla hajafa. Mambo haya hutokea mara chahe sana
 
Hakuna mwanasiasa yeyote nchini tangu uhuru ambaye amepigania haki za kiraia na kushinda kama Christopher Mtikila. NInaamini historia itakuja kumkumbuka kama shujaa wa demokrasia kwani pamoja na yote ambayo amepitishwa ameendelea kusimama kudai haki za raia wa Tanzania kwa namna ambayo mahakama zimekuwa upande wake mara ZOTE!

Leo hii napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa mtetezi huyu wa haki za raia. Ni mwanasiasa pekee ambaye amefanikiwa kulazimisha serikali kufanya isiyotaka kufanya na hata ilipokataa kufanya ametuwezesha kuona kuwa serikali haitaki kwa sababu tu haipendi si kwamba hoja ziko upande wake. HE IS MY HERO!

Ukweli ni kuwa amewapita kwa mbali sana wale wanasiasa wetu ambao labda majina yao ni maarufu sana na ambao wanaonekana ni maarufu; siyo tu Mtikila anazungumza anachozungumza bali anafanya pia anachozungumza. Of course, haiondoi ukweli mwingine wa mapungufu yake au siasa zake lakini ukweli ni kuwa kila alipojaribiwa na watawala amewashinda. Rekodi yake ya ushindi kwa miaka ishirini na ushee sasa inasimama kama ushahidi wa ushujaa wake.

Inasikitisha haijatokea wanasiasa wengine wa upinzani hata mara moja kuwa sehemu ya kesi zake au kuonekana wanajiingiza kama friends of the court (amicus curiae) kuonesha wanaunga mkono hoja zake.

When it comes to the 'walking' Mtikila does the walk!

Kuna wakati Marando alijitolea kumtetea mahakamani wakati ule Mtikila akiwa mahabusu keko kwa kosa la uchochezi wa machinga kugoma kuondoka kariakoo kupisha wahindi wafanye biashara zao bila kubughudhiwa na watanganyika. Muulize Marando kilichompata.
Tatizo sio hoja za mtikila tatizo lipo katika kuaminiana. Yeye mwenyewe mtikila hamuamini mwanasiasa mwingine na wanasiasa wengine hawamuamini Mtikila.
Napenda sana ujasiri wa Mtikila na hoja zake. Binafsi kuna kitu kimoja tu kilinifanya nimdoubt, pale nilipojua wana mahusiano ya kuazimana pesa na yule jamaa wa DOWANS, KAGODA nk.
 
Kuna wakati Marando alijitolea kumtetea mahakamani wakati ule Mtikila akiwa mahabusu keko kwa kosa la uchochezi wa machinga kugoma kuondoka kariakoo kupisha wahindi wafanye biashara zao bila kubughudhiwa na watanganyika. Muulize Marando kilichompata.
Tatizo sio hoja za mtikila tatizo lipo katika kuaminiana. Yeye mwenyewe mtikila hamuamini mwanasiasa mwingine na wanasiasa wengine hawamuamini Mtikila.
Napenda sana ujasiri wa Mtikila na hoja zake. Binafsi kuna kitu kimoja tu kilinifanya nimdoubt, pale nilipojua wana mahusiano ya kuazimana pesa na yule jamaa wa DOWANS, KAGODA nk.
Mwanakijiji hamfahamu huyu jamaa vizuri.
 
Umeniwahi...Isingekuwa njaa basi leo hata EPA angekuwa kesha tuwakilisha vizuri ... I realy admire his attitude!

Kwa sifa alizomwagiwa inawezekana ndie aliye tufumbua macho ishu za RICHMOND,TANGOLD,MEREMETA na DEEP GREEN.na amesha wahi kutoa matamko ya mara kwa mara kuhusiana na ufisadi huu.na ameshawahi kufungua kesi kuhusiana na ubadhirifu/ufisadi wa mali za umma
 
  • Thanks
Reactions: Ame
I am a teacher by profession and I can tell you that we do have home schooling. It has been shown that students whose parents care about education perform better than their peers. For, environments play a big part in child or student development.

1995 kulikuwa na suala na mgombea huru. Na nchi za wahisani zilishinikiza serikali kuangalia uwezekano wa kubadilisha katiba hili kuruhusu mgombea huru.

Ghafla bin vuu, NCCR, CHADEMA (wakati huo ikiwa bado CCM B) na CUF wakakubali kuingia kwenye uchaguzi bila marekebisho ya katiba. Na matokeo yake ni hasara kubwa kwa taifa.

But if your parents love school that is not home schooling to my understanding, perhaps it has to do with environment or inspiration, culture and genetics. In home schooling you are taught by your personal teacher from kindergarten to university degree. Only very rich kids can afford home schooling, because they want to teach their children about their business.

Lakini pia for your information tu, mgombea huru hawezi kushinda, na hata akishinda, it is nearly impossible to govern, hata awe nabii au mtume au nobel Laurent, especially in the third world country. Kwa sababu ni vigumu to appeal to all people of different backgrounds. Advantage ya chama or institution is that everyone can be represented in away. Hili swala la mgombea binasfi may be is just for democracy and socio-political experiments for the west.
 
Well said Mzee Mwanakijiji, lakini itafikia wakati historia itamweka sehemu anapohusika, hasa hii hypnosis [kiini macho] cha muungano kitakapo tatuliwa; Nataka nikufahamishe tu Mzee Mwanakijiji kwamba Mtikila ni SHUJAA WA TANGANYIKA, na ADUI WA TANZANIA yenye muundo mbovu wa kiutawala (muungano wenye misingi mibovu na ya ovyo), ndio maana kwa sasa amefifia; Lakini yote yatageuka with the RESURRECTION of our state of Tanganyika; Kwa kushirikiana na waelewa wengine wengi tu kama kina Tundu Lissu na wengineo, ipo siku tutafanikiwa; Ni bahati mbaya tu the fact kwamba he is a reverend imechangia sana jamii kupotoshwa kuhusu Mtikila na hivyo shujaa huyu kutopewa attention yenye uzito uliostahili wakati ukweli ni kwamba harakati zake zimekuwa very secular;

Long live Christopher Mtikila, umeteseka sana kwa kupigania haki yetu ya KIKATIBA, ingawa tulipumbazwa sana tukudharau kama vile wewe ni CHIZI NA MCHOCHEZI; Tumeshatenga pumba na mchele, na tutaendeleza pale ulipoishia na nina uhakika ipo siku watakaobaki katika mapambano watafika;

well presented mchambuzi. kwangu mimi mtikila ni shujaa anayepigania haki za kikatiba kwa kutumia nguzo ya MAHAKAMA....... MABADILIKO MAZURI NI YALE YANAYOKUBALIANA KUTOKEA KWENYE NGUZO ZOTE TATU, YAANI..S.EREKALI...BUNGE NA MAHAKAMA...... BILA MTIKILA THEN MHIMILI HUU WA MSINGI UNGEKUWA UMELALA...LONG LIVE MCHUNGAJI MTIKILA!
 
Ni MTIKILA ndiye aliyeweza kuondoa udhalimu wa CCM uliokuwa unavitaka vyama vyote vya siasa kuomba kibali cha kufanya mkutano kutoka kwa Mkuu wa Wilaya. Si rahisi mtu kuwa mzuri kwa 100% lakini nakubali kuwa mchango wa Mtikila katika ujenzi wa demokrasia na kuondoa utumwa wa CCM, kamwe hauwezi kubezwa na yeyote anayejua tulikotoka, tukiwa chini ya makucha ya serikali gandamizi ya CCM.

Mtikila ameisoma katiba vyema na kuielewa,ni mtu anayefahamu haki zake,lakini mbinafsi sana.Mtu anayeyumbishwa kwa mlungula hata iwe vipi hawezi kuwa hero wangu.Toka alipopokea ile pesa ya RA na ushahidi ukawekwa,pamoja na kule Tarime alipotumika hadi akapopolewa mawe,sina imani naye.However kwenye kupambana kuhusu haki flani flani na kesi dhidi ya serikali yupo fit.Isipokuwa mara zote ni issue zake binafsi na hazionyeshi benefits kwa general public.
 
Ni MTIKILA ndiye aliyeweza kuondoa udhalimu wa CCM uliokuwa unavitaka vyama vyote vya siasa kuomba kibali cha kufanya mkutano kutoka kwa Mkuu wa Wilaya. Si rahisi mtu kuwa mzuri kwa 100% lakini nakubali kuwa mchango wa Mtikila katika ujenzi wa demokrasia na kuondoa utumwa wa CCM, kamwe hauwezi kubezwa na yeyote anayejua tulikotoka, tukiwa chini ya makucha ya serikali gandamizi ya CCM.
Nakubaliana na wewe mkuu.Ni kweli kila binadamu ana mapungufu yake.Ila ya kupokea mlungula si mazuri kabisa.Je ina maana kama angepewa pesa za kutosha angetulia?Ni maswali mengine ya kujiuliza,ndo maana wengine licha ya ku admire juhudi zake,bado tuna fall short of calling him a hero_Otherwise nakubaliana kabisa kuwa ana nafasi yake.Just kama ilivyokuwa kwa Mrema nk.Tulishawajadili hao wote humu ndani kwasana tu.
 
Mzee hapa usiende mbali sana; Mtikila ni shujaa wa demokrasia kama nilivyoonesha hapo juu tu kidogo. Kwamba, ni Mtanzania pekee aliyekataa sheria ambazo zilikuwa zinambagua na akaenda mbele na kuzipa changamoto kwa kutumia mfumo ule ule. Nguvu zake za hoja zimeshinda mara nyingi kuanzia mwaka 1993. Ameweza kufanya kwa kweli kile ambacho kimetushinda wengi wetu. Kumshika ng'ombe mapembe na kumuweka zizini. Historia ya siasa za Tanzania haiwezi kabisa kuandikwa bila kumtaja Mtikila na mchango wake katika kukuza haki za kiraia.

Ni shujaa wangu kwa namna ya pekee kwa sababu ni mtu mmoja ambaye ni mbishi na asiyeheshimu watawala na ving'ora vyao. Tena yeye hakuanzia na kina Kikwete tu kaanza na kina Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete. Hana huruma kabisa na wala hana heshima mbele zao. Hakuna mwanasiasa mwingine aliyethubutu hivyo. Of course, siwezi kusema ndiye mwanasiasa ninayemhusudu zaidi katika Tanzania la hasha na wala hafikii kwa mbali wale ninaowahusudu kama wanasiasa. Yeye kwenye eneo moja he has done better and greater than any other politicians. Na huwa wanasema "give the devil his due" au tunavyosema "mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni" (japo sielewi kwanini wamnyonge kama anayo haki).

Mtikila alivyoumbuliwa na Rostam was classic lakini yenyewe haiondoi ukweli wa anachosimamia. Nimesoma wengi wamemfutilia mbali ati kwa vile alimuomba Rostam fedha kama deni na Rostam akampa. Kinachonishangaza sana na nimewasoma wengi hapa wakirudia hilo la Rostam kumpa fedha Mtikila na limeniacha na maswali. Watu wameamini kabisa bila kuhoji wala kujiuliza kama Rostam alisema kweli na kama alisema ukweli wote wa suala la fedha zile. Na wengi wanakumbuka kabisa alichosema Rostam lakini wachache (sijaona hadi hivi sasa hata mmoja) anayekumbuka majibu ya Rostam juu ya madai ya kupewa fedha Rostam. Lakini cha kushangaza zaidi ni kuwa watu wanasahau kuwa Rostam ndiye aliyejiuzulu (kama wengine tulivyoitisha) kwa kuwa kashfa za ufisadi zilikuw zimemzidia! Sasa huyu Rostam kwa wengine amegeuka mara moja mtu wa kumtolea mfano?

Lakini jambo jingine la kushangaza ni kuwa wapo watu hapa wanataka tuamini kuwa ukiwa na njaa usiombe chakula- hata kwa adui yako! Kwamba kwa vile mtu fulani ni adui yako wa kisiasa basi kama yuko katika uwezo wa kukusaidia usikubali msaada wake? Ya kweli haya? Lakini huyo huyo adui siku ya msiba wako atakuja na kutoa pola na watu watapokea? Hatujafika mahali pa uadui wa aina hiyo (japo labda wapo wanaomini kuwa iwe hivyo). Kwamba kwa vile Mtikila anampinga Rostam (na alifanya hivyo hata baada ya kupokea hizo fedha) basi Mtikila hapaswi kupokea msaada kutoka kwa Rostam? Really? Ni nani kati yetu ambaye watoto wakiwa wakiwa wagonjwa au yeye mwenyewe ambaye akiletewa msaada na adui yake hatopokea hasa kama ni msaada ambao kweli unaweza kumsaidia? Leo hii mimi binafsi kuna watu ambao tunatofauti kubwa sana za kisiasa (na labda wanniweka kama adui yao) sasa kweli unafikiria nikimkuta kaanguka au kaumia basi nitamwambia "ukome" ati kwa sababu ya tofauti za kisiasa? Well, siwezi kusema kuhusu wao lakini siwezi kushangaa kuwa wapo watu ambao wanaweza kusema kuwa adui yangu wa kisiasa kapatwa na baya basi akome na akomege!! Lakini watu wenye dhamiri hawawezi kufanya hivyo? Kuna mtu ameuliza Mtikila alienda kuomba fedha za nini kwa Rostam? Wengi wameshasema hapa kuwa Mtikila anaishi maisha ya dhiki kulinganisha na wengi tu sasa tunajuaje wakati huo kweli maji yalikuwa shingoni? Wanasema "angekufa kiume tu ndio aombe msaada kwa Rostam"?

Kuna uadui ambao kweli mtu hata kumpa maji unaweza usimpe lakini huu wa kisiasa sidhani. Ni kweli kinadharia ningeweza kusema Mtikila asingemwomba Rostam msaada na Rostam asingempa Mtikila msaada. Lakini sisi ni nani wa kusema kuwa asingeombwa na yule asingeomba? Wapo watu katika historia ambao katika ugumu wa shida waliomba msaada wa maadui zao nao wakasaidiwa na kuopolewa. Wakati wa vita ya pili ya dunia kuna mifano mingi ya matendo ya kibinadamu kati ya maadui wengi tu. Wapo waliojitoa mhanga kusaidia maadui zao bila kubadilisha uadui uliopo. Ndio ubinadamu wetu.

Sorry nimeenda kuzama kidogo kwenye hili maana limenikumbusha kisa cha rafiki yangu mmoja ambaye aliporudi nyumbani miezi kadhaa nyuma alijikuta ananyimwa usafiri wa gari pale alipojaribu kuitetea CCM. Watu wanakumbuka ya CUF na CCM kule Pemba kabla ya "maridhiano" ambapo watu hata kuzikana walikuwa hawazikani kisa "huyu CCM" na hyule ni "CUF". Tusiache siasa zetu zifikie huko.
Mzee mwanakijiji, pengine nawe umelitumia neno HERO pasipo kupima uzito wake maana haiwezekani mtu anayetafuta umaarufu kwa kupingana na serikali ili mradi yeye apate kunufaika tumwite hero. Ni kesi ngapi alizoshinda ambazo zimewafaissisha wananchi ama kuleta mageuzi nchini..Kama swala la mahakama basi wapo majambazi kina Massawe ambao hata kesi zao hazifiki mahakamani ikidhihirisha wameishinda serikali ya Nyerere, Mkapa na hata Mwinyi.

Sintoweza kumpa mtu utukufu huo kwa kushinda kesi mahakamani kwa ushenzi wake. Kuna watu wanamwita EL hero kwa sababu katushinda ktk kesi zote na leo tunamlipa mabillioni Dowans wakati Symbion ikilipwa pia pasipo mkataba mpya, wengine walimwita hero yule Jizi lilowashinda Polisi akiitwa Nyau, yaani mtu yeyote anayeweza kuiibia serikali huitwa hero.
Sintoweza kumwita FISADI yeyote kuwa hero kwa sababu tu anaikomoa serikali wakati ukweli unabakia kwamba wanaoumizwa sii viongozi wa CCM bali wananchi walipa kodi - Mtanisamehe..
 
Nashindwa kuelewa watu ambao wanapinga ukweli, mateso na jitihada zote aliyezifanya Rev Mtikila juu ya nchi hii. Na si kweli kuwa mengi aliyafanya kwa merits zake binafsi. Alipoanza siasa 1988 alianza na haki za binadamu.kuanzia wafungwa wa kisiasa (waliofungwa kwa uhaini kwa nia kumpindua mwl Nyerere), freedom of speech, haki ya mikusanyiko, vibali vya mikutano toka kwa mkuu wa wilaya, passport kwenda Zenj, mgombea binafsi etc. leo hii ni nani anayenufaika kama sio watanzania? Waulizeni mnaowaona kuwa ni wana siasa leo hii ni nani aliwakusanya, kuwaunganisha na kuanziasha original NCCR. Mtikila is very far ahead from our normal, average politicians from thinking, analysis, presentation and performance.

Kwa wengi wetu mpigania haki ni yule anaye sukumwa gari lake na watu wengi; ni yule anayesema maneno matamu hata kama hayana real impact kwenye maisha ya mtanzania wa kawaida....Ni yale mambo yanayoleta mhemko zaidi kuliko yale ambayo kwa akili ya kawaida yanaonekana si ya msingi japo hayo ndiyo yanayojenga misingi ya maisha yetu...Kwa haya uliyoyaelezea Mtikila amechora mstari na kujitofautisha na wengi...

Anaweza asisifiwe na anaweza asionje matunda ya anayoyapigania hapa duniani maana wito wake si katika hayo, lakini wengi watabarikiwa na kufanikiwa kupitia hayo mambo ya msingi aliyo ya pigania na huo ndiyo hasa uitwao uchungaji....Mchungaji mwema huyatoa maisha yake kwaajili ya kondoo zake....

Mtikila anajua Mungu pekee ndiye awezaye kupandisha na kushusha..Anaweza kubariki na kulaani naye anauchuchumilia uzima wa milele na stahili zake akianzia hapa duniani na baadaye katika umilele kule mbinguni kwa baba yake!
 
Du, aliniacha hoi pale alipowakatalia polisi kumkamata kwa kosa lingine.
Wadau hii huwa inakaaje maana kamjibu polisi ``WEWE NI WA NGAZI YA CHINI HUWEZI KUNIKAMATA MIMI``
Na polisi alinywea sijaielewa vizuri hii kitu wakuu. MMK msaada please
 
Vizuri umesema HERO WAKO lakini sii wangu miye kwa sababu siku zote anapigania haki yake yeye na sii ya WANANCHI. Kama nguvu hii ageiweka ktk kupigania haki za wananchi bila shaka kama sio mwaka 1995 basi 2000 angechukua nchi..MTIKILA ni Mbinafsi, mtu anayependa sana kutetea na kulinda maslahi yake kama mgombea..
Mtikila is my HERO! Mbinafsi ni wewe mkuu! Manake huoni anachokipigania Mtikila! Sasa hivi hatuombi tena kwa Dc kufanya mikutano! Kesi ya mgombea binafsi si haki binafi ya Mtikila bali haki hiyo ni ya kila mwananchi!.....
 
Mtikila is my HERO! Mbinafsi ni wewe mkuu! Manake huoni anachokipigania Mtikila! Sasa hivi hatuombi tena kwa Dc kufanya mikutano! Kesi ya mgombea binafsi si haki binafi ya Mtikila bali haki hiyo ni ya kila mwananchi!.....
Bila shaka kama umeniona mimi Mbinafsi siwezi kupinga maana wewe ndiye unayenijua vizuri kama mimi navyomjua Mtikila. Na nani kakwambia Mtikila ndiye alosababisha sheria ya mikutano ifanyike pasipo kibali cha Dc?..
 
Du Mtikila noma, kaniacha hoi zaidi pale alipowadindishia polisi kumkamata akiwaambia ni wa cheo cha chini hawazi kumkamata yeye .POLISI WALINYWEA NA HAWAKUMKAMATA.
Wadau nimeshindwa kuelewa Mtikila anaubavu gani hadi anatunisha msuli kiasi hicho .
Mwenye kunijuza tafadhali naomba nielewe maana polisi walitaka kumkamata wakimwambia ana kesi nyingine ya kujibu ila akawatunishia misuli.
 
Mzee Mwanakijiji hoja yako kuna watu hawajaielewa au imewakasirisha au imeowaondoa "mashujaa" wao kwenye orodha ya mashujaa wanaoweza kusifiwa wakiwa wangali hai. Kwangu mimi Mtikila amekuwa ni shujaa wa kweli kwenye kupigania haki za Msingi za Raia. Nakumbuka jinsi alivyoweza kumtetea mgombea mwenza wake 2005 asienguliwe kwa hoja kwamba Zanzibar hakuna magereza badala yake kuna vyuo vya mafunzo kwa hiyo mgombea mwenza wake habanwi na kipingele kinachosema mgombea asiwe amefungwa zaidi ya miezi sita. kwa hoja ya Mtikila ni kwamba Zanzibar watu hawafungwi jela bali wanapelekwa vyuo vya mafunzo.


Mzee Mwanakijiji hoja yako hapa ni kwamba Mtikila anaweka "Precedence" itakayosaidia wote wafuatao kupata haki yao mahakamani kwani tayari Kesi za Mtikila zitatumiwa kama Kesi rejea! Kwa watu wanaojua mifumo ya utendaji wa sheria wanajua kwa undani umuhimu wa haya anayoyafanya Mtikila!!
 
I am a teacher by profession and I can tell you that we do have home schooling. It has been shown that students whose parents care about education perform better than their peers. For, environments play a big part in child or student development.

1995 kulikuwa na suala na mgombea huru. Na nchi za wahisani zilishinikiza serikali kuangalia uwezekano wa kubadilisha katiba hili kuruhusu mgombea huru.

Ghafla bin vuu, NCCR, CHADEMA (wakati huo ikiwa bado CCM B) na CUF wakakubali kuingia kwenye uchaguzi bila marekebisho ya katiba. Na matokeo yake ni hasara kubwa kwa taifa.

Nakubaliana na wewe mkuu.Ni kweli kila binadamu ana mapungufu yake.Ila ya kupokea mlungula si mazuri kabisa.Je ina maana kama angepewa pesa za kutosha angetulia?Ni maswali mengine ya kujiuliza,ndo maana wengine licha ya ku admire juhudi zake,bado tuna fall short of calling him a hero_Otherwise nakubaliana kabisa kuwa ana nafasi yake.Just kama ilivyokuwa kwa Mrema nk.Tulishawajadili hao wote humu ndani kwasana tu.

ndo maana jamaa is not politically successful, critics zake hazina direct impact kwa mlala hoi kama mlala hoi. Mtikila is the by professional a lawyer, kwa hiyo how could you separate the fact kwamba what is doing is for professional benefits au kutetea wanyonge? Kama yeye ni hero kweli akaishitaki serikali kwa kushindwa kufikisha umeme vijijini. Anachokifanya Mtikila ni professional practices which synonymous is his carrier or carrier enrichment!!
 
umeniwahi...isingekuwa njaa basi leo hata epa angekuwa kesha tuwakilisha vizuri ... I realy admire his attitude!

hujui aliyoyapigania ila kwakuwa hupendi thread ikupite utaandika tu hata ugoro.
 
umeniwahi...isingekuwa njaa basi leo hata epa angekuwa kesha tuwakilisha vizuri ... I realy admire his attitude!
hujui aliyoyapigania. Ila kwakuwa hupendi thread ikupite hata ugoro utaandika
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom