Wambandwa
JF-Expert Member
- Dec 3, 2006
- 2,249
- 830
Mtoto kaingia meli ya wagiriki huyo..haya sasa,..yetu macho..slaa + mtikila...atatoka kweli?
Lazima atoswe higj seas!
Mtoto kaingia meli ya wagiriki huyo..haya sasa,..yetu macho..slaa + mtikila...atatoka kweli?
Mtoto kaingia meli ya wagiriki huyo..haya sasa,..yetu macho..slaa + mtikila...atatoka kweli?
Tena kwa kuwa yeye RIZ1 ni Mwanasheria asiajili wanasheria wengine ajisimamie au ashirikiane na Masha,wanaweza kushinda.ni kama hadith za sungura na fisi..sungura(dr na rev) lazima ashinde tu
Tena kwa kuwa yeye RIZ1 ni Mwanasheria asiajili wanasheria wengine ajisimamie au ashirikiane na Masha,wanaweza kushinda.
Kuwa mwanasheria hakumaanishi unajua kila kitu. Hakumaanishi unazijua sheria zote. Kwanza hakuna mtu anayezijua sheria zote. Pia hakumaanishi unaweza kushinda kesi yoyote ile iliyoko mbele yako.
Ushindi wa kesi unategemeana na mambo mengi sana na si cheti cha kuhitimu kozi ya sheria chuo kikuu na hatimaye kujiita au kuitwa mwanasheria.
In all honesty lawyers are really not what they are cracked up to be.
Huyu kijana amehitimu uanasheria au alikuwa anahudhuria madarasa tu?
Acha upunga wewe! Kwanini unaleta udini? Madrasa inaingiliana vp na Ridhiwan? Ucpende kuingiza wizi wa m2 na dini,who told u kwamba uislamu unaenda na wizi?
MWENYEKITI wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila, amemtaka mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwan Kikwete, kwenda mahakamani ndani ya siku saba alizosema vinginevyo atakwenda yeye kushtaki kutokana na utajiri alionao kwani ni kosa la jinai.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Mchungaji Mtikila alisema kwa taratibu za kisheria Ridhiwan anapaswa kuwapa kwanza ‘Demand Note Letter'( barua ya kuwataka wamwombe radhi au kufuta kauli zao) yeye na Dk. Willibrod Slaa.
"Ikiwa Ridhiwan hatafanya hivyo nitajipanga kwenda mahakamani kuwaeleza Watanzania namna mtoto huyo alivyo ni bilionea kupindukia kwa kumiliki mali nyingi zikiwemo fedha za Watanzania ambazo ni mabilioni katika akaunti zake, kampuni ya malori 150 na ya ujenzi pamoja na ghorofa za kupangisha," alisema Mtikila.
Kwa mujibu wa Mtikila, hawezi kuthibitisha kwa vielelezo aliyoyasema wakati alipokutana na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki iliyopita kuhusu utajiri wa mtoto huyo wa Rais kama hatapelekewa barua hiyo.
"Yawezekana Ridhiwan anazungumza maneno asiyoyafahamu kisheria na yeye tunasikia ni mwanasheria, kama unamtaka mtu akuombe radhi na kama akishindwa utampeleka mahakamani…maneno hayo kisheria huenda na demand note letter, sasa yeye hajatufikishia je tujipeleke? Alihoji Mchungaji Mtikila.
Alieleza kuwa kama kweli Ridhiwan ni mwanasheria na anazifahamu sheria, siku ile aliyozungumza na waandishi wa habari angekuwa na barua hizo mkononi tayari kwa kuwapelekea na kusubiri matokeo yake.
"Sasa naamini kwamba ni kweli Ridhiwan hajui sheria na kama angezifahamu, ningeshapata barua yangu mapema kwa kuwa anayafahamu makao makuu ya DP pale Ilala Msikitini na kama hazifahamu ofisi hizo angeniletea nyumbani kwangu Mikocheni B tuko jirani."
Juzi Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, naye alimtaka Ridhiwan kwenda mahakamani haraka kwa kuwa yaliyozungumzwa na kinywa chake yana ukweli.
Baada ya tamko hilo la Dk. Slaa siku chache baadaye Ridhiwan alizungumza na waandishi wa habari na kutoa siku saba kwa Dk. Slaa na Mtikila akiwataka kukanusha tuhuma walizomtupia au kuthibitisha kwa vielelezo, vinginevyo angewaburuza mahakamani kwa kumchafua yeye na familia yake.
Mwanzoni mwa wiki hii Ridhiwan aliwataka Watanzania wasimhukumu kwa kumuona akiendesha magari ya bei ghali na wazipuuze kauli zinazotolewa na wanasiasa hao wa upinzani kwamba ni za uongo.
Ridhiwan alikaririwa na vyombo vya habri akisema, "Hapa mjini jamani tunaishi kimjini si kila kitu unachomuona nacho mtu ni cha kwake."
Alisema yeye si bilionea kama wanavyodai wanasiasa hao, na kutaja mali zake kuwa ni shamba la ekari 1.5 lililoko Bagamoyo, gari aina ya Toyota Cami na akaunti katika benki za Stanbic na NBC na CRDB.
Tanzania Daima
Acha upunga wewe! Kwanini unaleta udini? Madrasa inaingiliana vp na Ridhiwan? Ucpende kuingiza wizi wa m2 na dini,who told u kwamba uislamu unaenda na wizi?
neno sterling unajua maana yake?Haya Mkuu sijui Sterling atakuwa nani katika sinema hii na title yake sijui itakuwa ni ipi.
Sidhani kama alikurupuka mkuu. Lazima alipata ushauri kwa wakubwa, na Docs nyingi zitakua zimebadilishwa.