Mtikila akataa hakimu tena

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,082
Monday, 14 June 2010 20:54 0diggsdigg

Tausi Ally na James Magai

KWA mara nyingine tena Mwenyekiti wa Chama Cha Demokratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila anayekabiliwa na kesi ya uchochezi amemkataa hakimu mwingine tena wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mchungaji Mtikila amechukua uamuzi huo wa kumuomba hakimu huyo Genivitus Dudu kujitoa katika kesi yake hiyo siku chake tu baada ya kesi kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa upande wa mashtaka ambao pia ulitolewa kwa njia ya luninga mbele ya hakimu huyo anayemtaka ajitoe Genivitus Dudu.

Dudu ni hakimu wa pili kukataliwa na Mchungaji Mtikila katika kesi hiyo ambayo Mtikila anadaiwa kumwita Rais Kikwete kuwa ni gaidi, huku hakimu mwingine wa tatu, Salome Mwandu akiwa amejitoa mwenyewe.

Katika barua yake aliyomwandikia hakimu Dudu kumtaka ajitoe katika kesi yake hiyo, Mchungaji Mtikila alidai kuwa hana imani na hakimu huyo kwa kuwa hatamtendea haki, huku akimtuhumu kufanya kazi kwa maslahi ya upande wa mashtaka.

Mchungaji Mtikila alitoa mfano wa tuhuma zake kwa hakimu Dudu kuwa alikuwa akijadiliana na upande wa mashtaka kuhusu kesi hiyo bila kuhusisha upande wa utetezi jambo ambalo alisema ni upuuzaji mkubwa wa kanuni ya kisheria ya haki na usawa.

Hoja nyingine aliyoitoa Mtikila katika barua yake hiyo ya kutokuwa na imani na hakimu huyo alidai kuwa amekuwa akikataa maombi yake hasa pale wakili wake, Mpale Mpoki alipoomba kesi hiyo iahirishwe angalau kwa muda wa wiki moja ili waweze kujadiliana na kujiandaa kwa ajili utetezi.

“Kosa linadaiwa kutendeka mwaka 2007, hivyo si rahisi kwa mtu yeyote kukumbuka kila kitu kichwani, lakini ulikataa vikali kukubalkiana na ombi hilokwa maslahi ya haki” anasisitiza Mtikila katika barua yake hiyo na kuongeza’

“Wakili wangu alipinga kupokewa kwa mkanda wa video kwa kuwa alikuwa hajaona kilichomo ndani kama ilivyo mantiki kwamba mtu anaweza akakubali au akakataa kitu baada tu ya kujua kilichomo, lakini ulikataa kuuchezesha mkanda huo ili kumpa nafasi ya kukubali au kukataa mkanda huo usipokewe”.

Pia Mtikila anamlalamikia hakimu huyo kwa kutupilia mbali pingamizi aliloliweka kupitia kwa wakili wake juu ya kupokelewa kwa maelezo yake anayodaiwa kuyatoa polisi (caution statement) na mkanda wa video ambavyo viliwasilishwa mahakamani hapo kama sehemu ya ushahidi katika kesi hiyo , lakini pia jakimu huyo alikataa .

Kabla ya kumkataa hakimu Dudu jana, Mtikila pia alishawahi kumkataa Hakimu Waliarwande Lema kwa madai kuwa hana imani naye akidai kuwa hataweza kumtendea haki kwa sababu ameonyesha kuwa na kisirani na ukatili dhidi yake., ndipo kesi hiyo ikapangwa Hakimu Salome Mwandu.

Hata hivyo Hakimu Salome naye alitangaza kujitoa katika kesi hiyo siku hiyo hiyo kwa maelezo kuwa awali alikuwa na kesi nyingine ya Mtikila hivyo kama angeendelea kuisikiliza kesi hii kulikuwa na uwezekano wa haki ikaonekana haijatendeka.

Katika kesi hiyo Mtikila anadaiwa kuwa Oktoba 21, mwaka jana maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Ilala, jijini Dar es Salaam Mtikila alitoa maneno ya uchochezi yenye dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.

Inadaiwa kuwa alitoa maneno hayo ya uchochezi kuwa ‘Papa alikuwa na mgeni ambaye ni gaidi, ninaomba niseme haya kwasababu ninasema mimi, Rais Kikwete ni gaidi.

"He is a terrorist ".
Ilidaiwa kuwa siku hiyo, Mtikila alitoa maneno mengine ya uchochezi ambayo yalikuwa na chuki na dharau ambayo yangeweza kusababisha watu kukosa imani na serikali yao.

Aidha, Mhungaji Mtikila pia anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kwamba: uteuzi wa "Jakaya Kikwete siku zote unaongozwa na imani yake ya dini kutekeleza malengo yake ya kusilimisha nchi....''
Mtikila akataa hakimu tena
 
According to the Oxford Advanced Learner's Dictionary, sedition consists of words or actions intended to make people oppose the state. In Mtikil'as case, he uttered words intended to make people oppose the President. Does the prosecution take Kikwete to be the state?

Article 18 of the Constitution of the United Republic of Tanzania allows every Tanzanian the right to express an opinion. It is entirely within the constitutional rights of Mtikila for him to express his opinion that JK is a terrorist and a religious bigot. That is asking people to oppose the President, not the state.

How could it be sedition for a politician like Mtikila to express his views about the President?
 
According to the Oxford Advanced Learner's Dictionary, sedition consists of words or actions intended to make people oppose the state. In Mtikil'as case, he uttered words intended to make people oppose the President. Does the prosecution take Kikwete to be the state?

Article 18 of the Constitution of the United Republic of Tanzania allows every Tanzanian the right to express an opinion. It is entirely within the constitutional rights of Mtikila for him to express his opinion that JK is a terrorist and a religious bigot. That is asking people to oppose the President, not the state.

How could it be sedition for a politician like Mtikila to express his views about the President?

Mkuu, so according to your expression of constitution and realities about politic, mtikila being a politician, it is his constitutional right?
Case is dismissed!!!
 
Inadaiwa kuwa alitoa maneno hayo ya uchochezi kuwa ‘Papa alikuwa na mgeni ambaye ni gaidi, ninaomba niseme haya kwasababu ninasema mimi, Rais Kikwete ni gaidi.

"He is a terrorist ".
Ilidaiwa kuwa siku hiyo, Mtikila alitoa maneno mengine ya uchochezi ambayo yalikuwa na chuki na dharau ambayo yangeweza kusababisha watu kukosa imani na serikali yao.

Aidha, Mhungaji Mtikila pia anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kwamba: uteuzi wa "Jakaya Kikwete siku zote unaongozwa na imani yake ya dini kutekeleza malengo yake ya kusilimisha nchi....''
Mtikila akataa hakimu tena

Hayo maneno ni lame at any standards or/and rate.

Kumuita rais kuwa ni gaidi au mdini si kitu cha kufumbia macho, maana maneno kama hayo yanaweza kuchukuliwa na watu wasio na busara kuleta vurugu na kusababisha uvunjifu na mkoroganyiko wa amani.
 
Hayo maneno ni lame at any standards or/and rate.

Kumuita rais kuwa ni gaidi au mdini si kitu cha kufumbia macho, maana maneno kama hayo yanaweza kuchukuliwa na watu wasio na busara kuleta vurugu na kusababisha uvunjifu na mkoroganyiko wa amani.

Sedition means an illegal action inciting resistance to lawful authority and tending to cause the disruption or overthrew the government.With that definition, Mtikila is caught in the web! Tuache ushabiki.
 
Hapa wanatakiwa wataalamu wa lugha kutoa maana ya neno 'gaidi' na 'ugaidi'. Yawezekana yana maana zaidi ya moja kutokana na 'context' yanapotumika!
 
Sedition means an illegal action inciting resistance to lawful authority and tending to cause the disruption or overthrew the government.With that definition, Mtikila is caught in the web! Tuache ushabiki.

Where did you get your definition of sedition from? I quoted mine from the (authoritative) Oxford Advanced Learner's Dictionary. Sedition has to do with organizing opposition to the state rather than opposition to the President.

Opposition politicians like Mtikila, are expected to bring down the president. It is at best politics, and at worst defamation, to express an opinion that the president is a terrorist and a religious bigot. It is not sedition.

Sedition is a sin against the state. It is not a sin against the President.
 
Back
Top Bottom