Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
I agree with this problem inakuja cost, hawa jamaa wanachofanya ni kupunguza gharama kwa ku-impair standard. wangelweza kutengeza secured network, na kuagiza high speed printers na kufanya kuwa ni lazima kila shule inunue au hata ikopeshwe kama shart la kusajiliwa na baraza. Tatizo linakuja, Internet, Kama baadhi ya wizara na idara nyeti hazina internet na sometimes updates zinafanyika mara moja kwa mwaka unatarajia nini. Hapa cha kufanya ni kuinvest kwenye elimu na sio siasa kama wanavyofanya watawala wetu.
Kila kitu cha msingi kina gharama. Tanzania tunapenda njia nyepesi na rahisi kutafuta ufumbuzi au kutatua matatizo ndio maana wanafunzi na wazazi nao wanatafuta njia fupi ku-wini hali halisi ya maisha Tanzania!
Dawa ni kuwa na computer centers wanafunzi wanakwenda fanya mitihani. Mtihani huu utakuwa mmoja tu kujua kama wanafunzi wana uelewo au hawana. Huko mashuleni, maksi zao na GPA zibakie huko huko pamoja na mitihani ya mwisho ambayo ni ya ama shule, kanfda au mkoa. Watakapofika kwenye exam center wakitumia namba ya mtu binafsi ya mtihani , akishaingiza jina na namba, maswali yanatoka kwa random order kuchanganya masomo yote kila akimaliza swali.
Akitoka hapo ni kijasho, awaambie kina John na Mwaimu swali la nne ni hsabati, akiingia John swali la nne ni Biology!
This will eliminate all the crap ya watu kukariri mambo au kuiba mitihani!