Likasu
JF-Expert Member
- Jan 18, 2011
- 843
- 405
Habari zenu wanaJF. Wife leo kapigiwa simu, unajua mambo ya wivu nikauliza aliyepiga simu ni nani ? Akasema kwa kuwa nataka kujua aliyepiga simu tubadilishane simu (pamoja na line zake) yeye achukue ya kwangu na mimi nichukue ya kwake kwa muda wa wiki moja. Ameng'ang'ania hilo swala na mimi nina vimeo kwenye simu yangu yaani sijui la kufanya kujiepusha na hili. Msaada wa mawazo unahitajika kuninasua katika hili.