mtihani mzito

Likasu

JF-Expert Member
Jan 18, 2011
843
405
Habari zenu wanaJF. Wife leo kapigiwa simu, unajua mambo ya wivu nikauliza aliyepiga simu ni nani ? Akasema kwa kuwa nataka kujua aliyepiga simu tubadilishane simu (pamoja na line zake) yeye achukue ya kwangu na mimi nichukue ya kwake kwa muda wa wiki moja. Ameng'ang'ania hilo swala na mimi nina vimeo kwenye simu yangu yaani sijui la kufanya kujiepusha na hili. Msaada wa mawazo unahitajika kuninasua katika hili.
 
Imenibidi nicheke. Unatikisa kiberiti!!! Pole badilishana halafu ndoa iishie hapo.
 
Bro asante sana kwa kunichekesha. Tangu asubuhi nilikuwa busy sana sijafurahi hata mara moja. Kwa mara ya kwanza naingia humu nimepata nafasi ya kucheka. Copy harakaharaka namba za simu za vimeo wako, wajulishe yanayojiri ili wasikupigie wala kukutumia message wiki hii. Halafu kubali mbadilishane. Au una vimeo vingi kiasi cha kutojua namba zao zote?
 
Pole kaka. Umeyachokoza mwenyewe, mpe line yako tu yaishe.
 
Bro asante sana kwa kunichekesha. Tangu asubuhi nilikuwa busy sana sijafurahi hata mara moja. Kwa mara ya kwanza naingia humu nimepata nafasi ya kucheka. Copy harakaharaka namba za simu za vimeo wako, wajulishe yanayojiri ili wasikupigie wala kukutumia message wiki hii. Halafu kubali mbadilishane. Au una vimeo vingi kiasi cha kutojua namba zao zote?
ushauri huu nimeupenda
 
hahahahahah lol
dahhh kuna vichekesho
kweli dunia hii

nway mie naona
ununue line mpya halafu
weka number za marafiki wa kiume
za kike unaziweka kama za dada, mama
shangazi wifi n.k halafu unawa txt wote
kuwajulia hali ukipata message kama 40 hivi
hiyo ndio number utakayompa mkeo...
hahahah lol
 
Bro asante sana kwa kunichekesha. Tangu asubuhi nilikuwa busy sana sijafurahi hata mara moja. Kwa mara ya kwanza naingia humu nimepata nafasi ya kucheka. Copy harakaharaka namba za simu za vimeo wako, wajulishe yanayojiri ili wasikupigie wala kukutumia message wiki hii. Halafu kubali mbadilishane. Au una vimeo vingi kiasi cha kutojua namba zao zote?

mmmhh kuna wengine
wata txt makusudi
kugombana tu a mkeo au
kumjulisha hayuko peke yake
hata hao Vimeo hawataki kujiona
second hand mmmhhhhhh
 
hivi kumbe ukiwa nyumba ndogo unakuwa 2nd class citizen? niliona wababa wanasifia hapa nikajua dili atii,asante kwa kunistua,lol!
mmmhh kuna wenginewata txt makusudi kugombana tu a mkeo au kumjulisha hayuko peke yakehata hao Vimeo hawataki kujiona second hand mmmhhhhhh
 
unahofia vimeo vyako,badilisha simu akupe ugonjwa wa maisha. mla vya watu vyake LAZIMA viliwe,mpe simu hiyo na ww ujionee utamu wa ngoma
Habari zenu wanaJF. Wife leo kapigiwa simu, unajua mambo ya wivu nikauliza aliyepiga simu ni nani ? Akasema kwa kuwa nataka kujua aliyepiga simu tubadilishane simu (pamoja na line zake) yeye achukue ya kwangu na mimi nichukue ya kwake kwa muda wa wiki moja. Ameng'ang'ania hilo swala na mimi nina vimeo kwenye simu yangu yaani sijui la kufanya kujiepusha na hili. Msaada wa mawazo unahitajika kuninasua katika hili.
 
mwambie una simu za ofisi unatarajia,hilo la kubadilishana simu halitawezekana kwa sasa!! Usiwe unatingisha kiberiti bila kujipanga...l.o.l
 
Kweli tumeumbwa na ubinafsi uliopitiliza,ukiona ivo ujue anajua unafanya nini hapo ndo kapatia njia ya kujua uaminifu wako kwake.
 
ama kweli m.me hata umuimbie nyimbo zote kabla ya kulala,umbembeleze,umuogeshe bado hatoridhika.why?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom