kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
AFISA mtendaji wa kijiji cha Marambeka wilayani Bunda, mkoani Mara, Kipa Kigombe (52), amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bunda, akituhumiwa kumkata masikio, Shaga Isaka, kwa madai ya kumfumania akifanya mapenzi na mke wake.
Mwendesha mashtaka wa polisi, Inspekta Hamza Mtogwa, aliiambia mahakama hiyo mbele ya hakimu mkazi mfawidhi, Joackim Tiganga, kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Januari 21, mwaka huu majira ya saa 6:30 usiku, katika kijiji cha Marambeka.
Alidai kuwa ofisa mtendaji huyo alimfumania Shaga Isaka (20), mkazi wa kijiji hicho, akifanya mapenzi na mke wake aitwaye Mariamu Kipa (22), baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.
Mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa mtuhumiwa baada ya kupata taarifa hizo aliamua kufuatilia na ndipo alipofanikiwa kuwakuta wagoni wake ndani ya nyumba wakifanya mapenzi.
Inadaiwa kuwa baada ya ofisa mtendaji huyo kumfumania kijana huyo, alimshambulia kwa kipigo na kutaka kumkatakata kwa panga lakini wananchi waliofurika katika eneo hilo walimzuia lakini alifanikiwa kuyakata masikio ya mlalamikaji.
Kwa mujibu wa Inspekta Mtogwa, mtuhumiwa aliamua kufanya kitendo hicho kwa madai ya kutaka kumuachia alama mgoni wake ili liwe fundisho kwake na kwa watu wengine wanaotembea na wake wa watu.
Afisa Mtendaji huyo amekana mashtaka yake na yuko nje kwa dhamana.
Mwendesha mashtaka wa polisi, Inspekta Hamza Mtogwa, aliiambia mahakama hiyo mbele ya hakimu mkazi mfawidhi, Joackim Tiganga, kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Januari 21, mwaka huu majira ya saa 6:30 usiku, katika kijiji cha Marambeka.
Alidai kuwa ofisa mtendaji huyo alimfumania Shaga Isaka (20), mkazi wa kijiji hicho, akifanya mapenzi na mke wake aitwaye Mariamu Kipa (22), baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.
Mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa mtuhumiwa baada ya kupata taarifa hizo aliamua kufuatilia na ndipo alipofanikiwa kuwakuta wagoni wake ndani ya nyumba wakifanya mapenzi.
Inadaiwa kuwa baada ya ofisa mtendaji huyo kumfumania kijana huyo, alimshambulia kwa kipigo na kutaka kumkatakata kwa panga lakini wananchi waliofurika katika eneo hilo walimzuia lakini alifanikiwa kuyakata masikio ya mlalamikaji.
Kwa mujibu wa Inspekta Mtogwa, mtuhumiwa aliamua kufanya kitendo hicho kwa madai ya kutaka kumuachia alama mgoni wake ili liwe fundisho kwake na kwa watu wengine wanaotembea na wake wa watu.
Afisa Mtendaji huyo amekana mashtaka yake na yuko nje kwa dhamana.