Hakuna sababu ya msingi iliyompeleka jela zaidi ya sifa za kijinga.
Mahakama inaongozwa na sheria sio siasa.
Hakuna sababu ya msingi iliyompeleka jela zaidi ya sifa za kijinga.
Mahakama inaongozwa na sheria sio siasa.
Hakuna sababu ya msingi iliyompeleka jela zaidi ya sifa za kijinga.
Mahakama inaongozwa na sheria sio siasa.
Mkuu a.k.a Mzee!!!
Hivi kati ya yeye Lema na wewe nani anasababu za kijinga hapa?
Waweza kutuambia kuna kosa gani katika kesi ya Lema zaidi ya Police kufanya imagination ya jambo au tukio ambalo halija tokea? wao siku zote ni kukimbila maandamano ndilo kosa kubwa wakisema sababu za kiintelligensia kivipi?
Mara ngapi Police wameruhusu Mikutano na maandamano ya CDM na hukjatokea fujo yoyote iweje leo mtu anatoka Mahakamani mwenyewe una mzushia kesi ya mkusanyiko kuwa ni maandamano hilo lina ingia akilini? Mfano tumekupa wa Byesige na Museven Jana anakwenda kazini kwa miguu ati hurusiwi tembea lakini alitolewa ndani ya masaa 24 sasa ya lema Police wao wameifanya kesi kwa kosa gani hapo kweli wewe waona ni sheria inatizama mkondo wake ??
Na hao Mahakimu wa mahakama watupe Ushahidi wa kusema ile ni kesi au wanataka kufuja kodi za wananchi tu na ku draw attention zisizo na kichwa la miguu, Hii ni Order kutoka kwa watendaji wa juu hapo Arusha na kupata support ya wakuu kutoka Dar na hakuna hata vyombo vya Media kujadili kuiuliuza Police makao makuu kutufafanulia tukio hilo lilikuwaje? Au wao walikuwa wana mtishia Lema Nyau.
My Take;
Mfano wa Lema kwenda jela sasa wapo wana CDM watukutu kuliko Lema mara hamsni yake sasa sijui Police itaweza wazuia hao au? Libya watua walijifunza kufyatua risasi njiani kwenye mapambano na wakamweka chini Gaddafi sijui utasema nao ni wahuni pia sasa NTC ndio imeweka Prime Minister sasa na Tanzania hii nayo imekubali ingawa walikuwa hawataki kwa sababu zao wao wenyewe huku wakijua wao ndio wale wale wa Gadaffi
nimepata habari kuwa walitaka kumlawiti lakini askari magereza wakamuokoa, suruali ilishafika magotini
tusujidanganye kuwa nchi yetu ni ya utulivu na amani hilihali wananchi wake wamejawa na hasira mioyoni mwao. tafsiri ya amani si kwa kumwangalia mtu usoni ila moyoni mwake anafikiria nini. matendo kama haya yanayofanywa na jeshi la polisi hususani wa arusha mpaka kufikia kuita raia panya, maneno aliyoyatumia Ghadafi kwa wananchi wake na akaishia kukumbilia kwenye calvat na kukamatwa kama MBwa.
Wanayatenda haya kwa amri za wakubwa wao lakini wajue ya kwamba bomu wanalotengeneza siku linalipuka hakutakalika. wanaounga mkono hali kama hii ya uonevu na ukandamizaji ndani ya nchi yao hakika si wazalendo wala si sio wapigania haki ya kweli. Ni wanafiki na vibaraka ndani ya nchi yao. Ukiona kijana anashabikia na kuunga mkono hali kama hii hafai kusikilizwa.
WAJUE YA KWAMBA THERE IS NO SITUATION WHICH IS PARMANENT iko siku na wao watakua upande wetu. Kila kitu kina mwisho. hali hii isitukoseshe nguvu wala isitufunge midomo Lema kaonyesha njia na sisi wapenda haki tummunge mkono.
Mimi ni mwanachadema tangu 2005 na ninakipenda sana chama chetu makini CHADEMA. Kama wadau na wenye chama tunachukuliaje jambo alilofanya Mh. Lema kwa kukataa dhamana na kukubali kuingia gerezani?