MTANZANIA yakemewa bungeni

Nikupateje

JF-Expert Member
Dec 22, 2009
1,334
988
Leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali Naibu Spika aliwasomea wabunge kichwa cha habari cha gazeti lililotoka leo ambalo ni MTANZANIA lenye kichwa kisemacho WABUNGE NGUVU YA SODA.

Ndugai alikerwa na habari hiyo kwamba inalidhalilisha bunge japo waandishi wanatumia uhuru wao wa kuhabarisha.

Alisema Bunge ni taasisi inayoheshimiwa na hivyo kuna haja ya kudhibiti uandishi wa aina ile.

Lakini akaongeza kwamba waandishi wanalipinga bunge kwa sababu wabunge wenyewe ndiyo wa kwanza kulipinga bunge lao badala ya kulitetea.

Binafsi sikutaka kusimuliwa nikalikimbilia gazeti hilo na nimeli-scan ili thinkers mjadili.

Scan iko katika page tatu na hivyo kuna document tatu za kudownload yaani Ndugai-01, Ndugai-02 na Ndugai-03.

Nimesita kwanza kuonyesha maoni au hisia zangu ili nisii-bias hii post ili ihukumiwe kwa haki humu JF.

Kazi kwenu.
 

Attachments

  • Ndugai-03.jpg
    Ndugai-03.jpg
    299.9 KB · Views: 181
  • Ndugai-02.jpg
    Ndugai-02.jpg
    386.3 KB · Views: 131
  • Ndugai-01.jpg
    Ndugai-01.jpg
    273.5 KB · Views: 165
Magamba walizoea kusifiwa na magazeti ya RA hata pale ambapo hawakustahili kusifiwa. Nami nime note kuwa magazeti ya new habari corporation yamebadili Stance. Ndugai na wenzake nafikiri haiwakeri hiyo habari ya nguvu ya soda bali trend ya gazeti hilo. Kikubwa wao wapprove otherwise sio kulitisha gazeti. Foka yote kuhusu wizara ya usafirishaji imeishia wapi!!
 
Hata mimi nawaona wabunge kama wamelainika kirahisi sana ila sijaona hlo gazeti likitoa hoja yoyote ya maana zaidi ya kunukuu hoja ya waziri mkuu na wabunge.but hli gazeti linaelekea kubadilika.
 
hacha upuuzi huo .walifungie au wamesubiili boss ya gazeti hilo hayumo mjengoni wanalalamika .wamezoeya vya kunywongwa
 
Labda ni kwasababu ni gazeti la Mtanzania limeandika hivyo... What if lingekuwa Tanzania Daima. Angelisuta hivyo!!??
 
Ni kweli kabisa wabunge ni nguvu ya soda.........wanasema sana lkn mwisho wa siku wanaunga hoja vbila kupinga............wanatoa mazimio ambayo hayatekelezwi na serikali hiyo yote ni nguvu ya soda............wanaamini baada ya kumuumiza fisadi rostam nini kimebaki km sio mkuki kwa nguruwe
 
Leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali Naibu Spika aliwasomea wabunge kichwa cha habari cha gazeti lililotoka leo ambalo ni MTANZANIA lenye kichwa kisemacho WABUNGE NGUVU YA SODA.

Ndugai alikerwa na habari hiyo kwamba inalidhalilisha bunge japo waandishi wanatumia uhuru wao wa kuhabarisha.

Alisema Bunge ni taasisi inayoheshimiwa na hivyo kuna haja ya kudhibiti uandishi wa aina ile.

Lakini akaongeza kwamba waandishi wanalipinga bunge kwa sababu wabunge wenyewe ndiyo wa kwanza kulipinga bunge lao badala ya kulitetea.

Binafsi sikutaka kusimuliwa nikalikimbilia gazeti hilo na nimeli-scan ili thinkers mjadili.

Scan iko katika page tatu na hivyo kuna document tatu za kudownload yaani Ndugai-01, Ndugai-02 na Ndugai-03.

Nimesita kwanza kuonyesha maoni au hisia zangu ili nisii-bias hii post ili ihukumiwe kwa haki humu JF.

Kazi kwenu.

sio mbaya sana kwa magazeti ya fisadi yakiwashughulikia wabunge wa kusinzia.

magamba yamewazidi uzito, sasa wamekuwa legelege kuliko hata serikali yao.
 
Mtanzania na vyombo vingine vya habari havidhililishi na wala havitadhililisha bunge. Watu wanaodhalilisha bunge tena kwa kiwango cha kushangaza ni Ndugai mwenyewe, Spika Anna Makinda, Mabumba na Simachawene. (Mhagama ana nafuu) Hao wakubwa niliowataja wameshindwa kutambua au wameamua kutotambua kuwa Bunge ni mhimili huru wa dola na bunge haliwajibiki kwa serikali ila kwa wananchi walioachagua.

Kwa jinsi ambavyo Ndugai na wenzake (na hasa Ndugai) wamekuwa wanaendesha vikao vya bunge ni wazi kuwa wako hapo kutetea maovu na ufisadi unaofanywa na baadhi ya watu ndani na nje ya serikali. Ni hoja ngapi mbovu zimepitishwa bungeni kwa nguvu ya kiti cha Spika? Bajeti ya Uchukuzi ilionekana kabisa kupwaya na wabunge wengi wa ccm walielekea kuikataa, sasa kama sio nguvu ya soda makelele ya kuikataa yameishia wapi?
 
Jamani wambunge wa ccm ndo nguvu ya soda ndo walipitisha ile bajeti. Cdm na nccr walipinga vikali labda na wake zao wadogo cuf,udp na Tlp ndo waliunga nadhani hawa ndo nguvu soda.
 
wabunge wa ccm unafiki mtupu, wanatenda tofauti na wasemavyo, mchana wanakataa rushwa usiku wanachukua
mimi naona kelele zile ilikuwa ni vitisho kwa katibu mkuu awatengee bahasha zao la sivyo wammwage hawakuwa na lolote makele kama povu la soda
 
Mimi pia gazeti hili lilianza kunishangaza baada ya kuanza kwenda kinyume na serikali kumbe bos wao kawaambia waharibu tu.hizi ndiyo changamoto kwa bunge na serikali,watu husema ukizoea kusifiwa jiandae pia na kuzomewa.
 
Leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali Naibu Spika aliwasomea wabunge kichwa cha habari cha gazeti lililotoka leo ambalo ni MTANZANIA lenye kichwa kisemacho WABUNGE NGUVU YA SODA.

Ndugai alikerwa na habari hiyo kwamba inalidhalilisha bunge japo waandishi wanatumia uhuru wao wa kuhabarisha.

Alisema Bunge ni taasisi inayoheshimiwa na hivyo kuna haja ya kudhibiti uandishi wa aina ile.

Lakini akaongeza kwamba waandishi wanalipinga bunge kwa sababu wabunge wenyewe ndiyo wa kwanza kulipinga bunge lao badala ya kulitetea.

Binafsi sikutaka kusimuliwa nikalikimbilia gazeti hilo na nimeli-scan ili thinkers mjadili.

Scan iko katika page tatu na hivyo kuna document tatu za kudownload yaani Ndugai-01, Ndugai-02 na Ndugai-03.

Nimesita kwanza kuonyesha maoni au hisia zangu ili nisii-bias hii post ili ihukumiwe kwa haki humu JF.

Kazi kwenu.

inanikumbusha wakati fulani waandishi wa habari walimhoji mh. kingunge juu ya msimamo wa ccm kufuatia cuf kuchukua majmbo takriban matatu ya marudio ya uchaguzi wa zanzibar majibu ya mh yakawa "ccm haitetereki na haina wasiwasi", kesho yake gazeti likatoka na kichwa cha habari " ccm kuendelea kuuchapa usingizi - kingunge" matokeo yake mh alikuja juu na akawa mkali kwelikweli kwa madawi gazeti lilimnukuu vibaya.
kwa ujumla malalamiko ya ndugai na wenzie ni kutokana na ukweli kwamba bunge letu lipo ni bunge la wanungunikaji zaidi na upande wa pili serikali imebaki ya kujitetea zaidi. kwa msingi huo naomba ndugai aamini kuwa mwandishi alikuwa na maana ya " bunge letu linatabia ya kubana na baadaye kuachia" kitu ambacho hata serikali inafahamu na kuwa first approach bunge litabana lakini mwishoni litaachia"
 
Rostam keshajivua Gamba na yule ni capitalist lengo la Capitalist siku zote nikujilimbikizia nakupata faida zaidi kwahiyo kipindi ajajivua gamba alibenefit kutokana na nafasi yake ndani ya chama nakujipendekeza ndani ya chama so yawezekana kabisa Gazeti lake kama gazeti halikumuingizia faida direct ila faida aliipata kwa njia zingine saiv hana chakupoteza lazima ajenge credibilitý ya watu kuliamini Gazeti ili afanye biashara so hapa policy ya gazeti imebadilika na kwa watu wenye upeo mdogo kama Ndugai ni vigumu sana kuelewa haya mambo.
 
Magazeti ya RA yalibadili mwelekeo siku nyingi japo bado wanagusa gusa tu mambo ya ufisadi ila la msingi nimefurahi kwamba ccm imeongeza adui wakati nguvu zimezidi kupungua na hii ni advantage kwa wanamageuzi
 
huyu KILAZA anatetea kibarua chake hakuna jingine
ni vema akagawa kipato anachopata kumhudumia mkewe aliyemtelekeza badala ya kuwapiga waandishi wanaoandika ukweli
 
New Habari ulikuwa mhimili wa magamba katika sekta ya habari. Walikuwa wapambe wao muhimu kwa kuwa Uhuru na Mzalendo hayanunuliki zaidi ya kuwekwa kwenye maktaba za taasisi za umma. Sasa New Habari imebadili mwelekeo. Tukumbuke Rostam aliinunua ile kampuni kwa lengo la kuisafisha magamba. Akaamua kuuza hisa zake za gazeti alilolianzisha mwenyewe la Mwananchi baada ya kuona mrengo wake haushabihiani na mwanahisa mwenzake Aga Khan. Akasalimu amri, akahamia New Habari kiasi cha kuwakimbiza Jenerali na wenzake.

Sasa madhali New Habari imebadili njia, ashukuriwe sana Allah.

Magamba wanapumulia mashine,
 
Back
Top Bottom