Mtanzania kwenda anga za juu; gazeti lasema "mwezini"!

Ninavyoelewa Mtanzania ni mtu mwenye uraia wa Tanzania i.e mtu aliyezaliwa UK na baba na mama waUK akachukua Uraia Bongo tunamwita Mtanzania hatumwiti Mwingereza.
Wangesema ni raia wa UAE ambaye ana asili ya TZ nadhani ingekuwa karibu zaidi na ukweli. Kwa hiyo huyo Julius na Mtoto wake hawawezi kujiita Watanzania.

Kwa hiyo mara Julius alipochukua uraia wa Marekani basi uTanzania wake umepotea? Ninavyojua mimi ni kuwa uingereza na uraia wa uingereza ni vitu viwili tofauti. Raia wa uingereza akichukua uraia wa Tanzania, anachopoteza ni uraia wake tu lakini uingereza unabaki pale pale. Vile vile humu ndani wako wenzetu wengi ambao bila shaka wana uraia wa nchi tofauti na Tanzania lakini wako mstari wa mbele kujivunia u-Tanzania wao. Nadhani wakati umefika wa kutofautisha uraia wa Tanzania na u-Tanzania.

Amandla.......
 
Kwa hiyo mara Julius alipochukua uraia wa Marekani basi uTanzania wake umepotea? Ninavyojua mimi ni kuwa uingereza na uraia wa uingereza ni vitu viwili tofauti. Raia wa uingereza akichukua uraia wa Tanzania, anachopoteza ni uraia wake tu lakini uingereza unabaki pale pale. Vile vile humu ndani wako wenzetu wengi ambao bila shaka wana uraia wa nchi tofauti na Tanzania lakini wako mstari wa mbele kujivunia u-Tanzania wao. Nadhani wakati umefika wa kutofautisha uraia wa Tanzania na u-Tanzania.

Amandla.......

Fundi,nadhani ikija kwenye "Legality" Ni LAZIMA uwe raia wa Tanzani kabla hauja declare kuwa wewe ni Mtanzania,kwa mfano kama ni mahakamani,ukaulizwa wewe raia wa wapi,ukasema ni Mtanzania,basi ni lazima uwe na documents zinazoback up your claim.
Kusema tu wewe ni Mtanzania na wakati wewe si Raia wa Tanzania hakuna shida yoyote kama hauna nia ya upotoshaji kwa maslahi flani,ni terminologies tu zinazoweza kutumika coz hakuna technicalities involved. Watu wanaweza kuitwa "African Americans" kwasababu wana asili ya Afrika,lakini ukweli wao ni wamarekani na hata kama ni uwakilishi say wa olympics ama something else,watakuwa wanaiwakilisha marekani na si Afrika,Afrika tunaweza kujivunia kwasababu ya asili ya uafrika ya mwenye achievements,lakini hatuwezi ku claim achievements kuwa ni za Afrika....Kwasababu hiyo basi,huyo mtu anaweza kuwa na asili ya Tanzania lakini hawezi kuwa mwakilishi wa Tanzania kwa kujiita "Mtanzania" kwani si raia wa Tanzania kisheria.
 
Kwa hiyo mara Julius alipochukua uraia wa Marekani basi uTanzania wake umepotea? Ninavyojua mimi ni kuwa uingereza na uraia wa uingereza ni vitu viwili tofauti. Raia wa uingereza akichukua uraia wa Tanzania, anachopoteza ni uraia wake tu lakini uingereza unabaki pale pale. Vile vile humu ndani wako wenzetu wengi ambao bila shaka wana uraia wa nchi tofauti na Tanzania lakini wako mstari wa mbele kujivunia u-Tanzania wao. Nadhani wakati umefika wa kutofautisha uraia wa Tanzania na u-Tanzania.

Amandla.......

FM... ni vizuri kuonesha kile ambacho kinafanywa hapa Marekani... kuna kitu kinaitwa "nationality, ethnic origin, national origin, race n.k" vitu hivyo vyote havifungamani moja kwa moja na uraia wa mtu. Huku nyuma niliwahi kusema kuwa Uraia is a legal concept not an ideological or political position.

Kuwa raia wa nchi fulani kuna maana umetimiza matakwa fulani ya kisheria. Lakini national origin ya mtu fulani haitegemei uraia wake. Mtu anaweza kuwa ni Muiraq (national Origin) na akawa Raia wa Marekani au kinyume chake.

Kinachogombanisha watu ni kuchanganya "uraia wa nchi mbili" (dual citizenship) na mchanganyiko wa vitu hivyo hapo juu na uraia. Mtu mwenye uraia wa nchi mbili ametimiza masharti ya uraia wa nchi hizo mbili.

Tatizo ni kuwa kwa Tanzania mtu hawezi kuwa na uraia wa nchi mbili kwa sasa. Wapo wanaofikiria wana uraia huo lakini kisheria hawapo kwa sababu Tanzania haitambua dual citizenship (isipokuwa kwa watoto ambao bado hawajaukana uraia wa wazazi wao hadi wafikishe miaka 18).
 
The recurrent seismic movement of dual citizenship is in search of its way for ecstatic resurrection as in the thriller of Wacko Jacko.
 
Lakini mimi nafikiri watu wamechanganya mambo kwa kutokana na uelewa mdogo wa kiuandishi.

Gazeti la serikali ya Tanzania yaani Daily News lenyewe limesema kwamba huyu bwana ni "Ugandan based business man"- yaani anaishi na kufanya biashara zake Tanzania lakini anatokea Uganda, fuatilia link hii http://www.dailynews.co.tz/

Raisi Kikwete amempa bendera ya Tanzania kutokana na yeye kutaka kumshukuru mama yake ambae alizaliwa Mwanza nchini Tanzania "tribute" kwa kuingia na abiria wengine kwenye hio ndege ya angani ya Virgin Galactic.

Halafu gazeti lingine nalo nimezidi kuchanganya watu na habari yake kwamba huyu bwana ni mwarabu kutoka Arabuni kwamba na anafanya biashara zake mjini Dubai.

My take ni kwamba huyu bwana si Mtanzania na wala hana haki ya kuwa mtanzania ila yupo Tanzania kwa sababu mama yake alizaliwa na anatoka Tanzania.

Sijui hizi "spining" ni kwa manufaa ya nani.
 
Kwa hiyo mara Julius alipochukua uraia wa Marekani basi uTanzania wake umepotea? Ninavyojua mimi ni kuwa uingereza na uraia wa uingereza ni vitu viwili tofauti. Raia wa uingereza akichukua uraia wa Tanzania, anachopoteza ni uraia wake tu lakini uingereza unabaki pale pale. Vile vile humu ndani wako wenzetu wengi ambao bila shaka wana uraia wa nchi tofauti na Tanzania lakini wako mstari wa mbele kujivunia u-Tanzania wao. Nadhani wakati umefika wa kutofautisha uraia wa Tanzania na u-Tanzania.

Amandla.......

Habari inasema ni Mtanzania, sio ana Utanzania. Julius amepoteza kuitwa Mtanzania, kwa hiyo hii habari iko off.
Huo Utanzania sijui ni nini?

Kama inaamaanisha ana asili ya TZ basi sawa, otherwise huo Utanzania nadhani uko kwenye individual basis, kuna wanaojivunia na wasioutaka kabisa huo Utanzania. Labda hata Mwingereza aliyeishi miaka mingi Bongo tunaweza tukasema ana Utanzania, its open to interpretation nadhani.
 
Nchi ishakuwa ya kihuni...kila mtu anaruhusiwa kuonana na rais tuuuu...hata kama reason inachanganya watu...kama hivi..ona sasa kila kitu hovyo.Wapunguze ungeni usio na tija kwa nchi yetu...kwenda kumuona rais ili kupunguza habari za mwongo kwenye nchi.
 
(CNN) -- "By blood, I am Albanian. By citizenship, an Indian. By faith, I am a Catholic nun. As to my calling, I belong to the world."

 
Wabongo kwa ku piggyback wireless signal za wenzetu!

Obviously hatuna chombo cha kwenda mwezini, lakini tunataka kumpa bendera apige picha na kutangaza utalii wa Tanzania.

Tena rais ndiye anayesema, utafikiri anapiga soga Msoga!
 
Nchi ishakuwa ya kihuni...kila mtu anaruhusiwa kuonana na rais tuuuu...hata kama reason inachanganya watu...kama hivi..ona sasa kila kitu hovyo.Wapunguze ungeni usio na tija kwa nchi yetu...kwenda kumuona rais ili kupunguza habari za mwongo kwenye nchi.

Hivi ni kweli hakuwa na muda wa kufungua Kongamano la kimataifa la usomaji pale Chuo Kikuu Cha DSM japo inasemekana alialikwa afanye hivyo ila eti siku hiyo hiyo alikuwa na muda wa kukutana na supastaa wetu wa mpira wa kikapu pale Ikulu?
 
Habari inasema ni Mtanzania, sio ana Utanzania. Julius amepoteza kuitwa Mtanzania, kwa hiyo hii habari iko off.
Huo Utanzania sijui ni nini?

Kama inaamaanisha ana asili ya TZ basi sawa, otherwise huo Utanzania nadhani uko kwenye individual basis, kuna wanaojivunia na wasioutaka kabisa huo Utanzania. Labda hata Mwingereza aliyeishi miaka mingi Bongo tunaweza tukasema ana Utanzania, its open to interpretation nadhani.

Naona kiswahili kinakupiga chenga. Matumizi ya neno m-Tanzania na u-Tanzania yanategemea 'context'. Hauwezi kusema 'akajivunia m-Tanzania'. Neno m-Tanzania linatokana na u-Tanzania. Swali langu kwa kifupi lilikuwa, je m-Tanzania ni yule mwenye asili ya Tanzania ( u-Tanzania) au ni kwa yule ambae ana uraia wa Tanzania peke yake? U hyphenated citizenship ni suala lingine. African-American, Irish-American, Italian-American, Asian-American, Jewish-American wote ni raia wa marekani lakini wanajiita hivyo kuonyesha asili yao. Hawa ingawa ni raia wa nchi hiyo hawasiti kudai uhusiano maalum na nchi zao za asili. Irish-Americans walikuwa ndiyo wachangiaji wakubwa wa I.R.A, Jewish-Americans wana hakikisha kuwa Israel inabaki kuwa na uhusiano maalum na Marekani, Italian-Americans wanajivunia vyakula vyao n.k. Vile vile nchi zao za asili hazichelei kudai sehemu ya sifa ambazo mtu wao anazopata huko kwenye nchi ambayo yeye ni raia wake. Mhindi-mmarekani anaposhinda Nobel Prize basi India na yenyewe inajionea fahari.

Sisi kwetu hilo hatuna. Kwa vile tunachanganya u-Tanzania (ethnicity) na uraia wa Tanzania basi akija mtu ambae hatumwoni anaelekea kwenye hiyo tafsiri yetu hata kama asili yake ni Tanzania tunamsinga anapojiita au anapoitwa mtanzania. Na hili limejitokeza kwenye hii taarifa. Jamaa mkazi wa Dubai, pengine raia wa Uingereza lakini mama yake ni au alikuwa m-Tanzania basi akiitwa m-Tanzania tunaanza kuona mushkeli. Binafsi sioni tatizo la mtu yeyote mwenye asili ya Tanzania kujiita m-Tanzania hata kama ana uraia wa nchi nyingine. Huyu akiulizwa uraia wake hata siku moja hatajibu ni Tanzania lakini kwa nini azuiwe kusema yeye ni m-Tanzania wa asili?

Amandla......
 
Naona kiswahili kinakupiga chenga. Matumizi ya neno m-Tanzania na u-Tanzania yanategemea 'context'. Hauwezi kusema 'akajivunia m-Tanzania'. Neno m-Tanzania linatokana na u-Tanzania. Swali langu kwa kifupi lilikuwa, je m-Tanzania ni yule mwenye asili ya Tanzania ( u-Tanzania) au ni kwa yule ambae ana uraia wa Tanzania peke yake? U hyphenated citizenship ni suala lingine. African-American, Irish-American, Italian-American, Asian-American, Jewish-American wote ni raia wa marekani lakini wanajiita hivyo kuonyesha asili yao. Hawa ingawa ni raia wa nchi hiyo hawasiti kudai uhusiano maalum na nchi zao za asili. Irish-Americans walikuwa ndiyo wachangiaji wakubwa wa I.R.A, Jewish-Americans wana hakikisha kuwa Israel inabaki kuwa na uhusiano maalum na Marekani, Italian-Americans wanajivunia vyakula vyao n.k. Vile vile nchi zao za asili hazichelei kudai sehemu ya sifa ambazo mtu wao anazopata huko kwenye nchi ambayo yeye ni raia wake. Mhindi-mmarekani anaposhinda Nobel Prize basi India na yenyewe inajionea fahari.

Sisi kwetu hilo hatuna. Kwa vile tunachanganya u-Tanzania (ethnicity) na uraia wa Tanzania basi akija mtu ambae hatumwoni anaelekea kwenye hiyo tafsiri yetu hata kama asili yake ni Tanzania tunamsinga anapojiita au anapoitwa mtanzania. Na hili limejitokeza kwenye hii taarifa. Jamaa mkazi wa Dubai, pengine raia wa Uingereza lakini mama yake ni au alikuwa m-Tanzania basi akiitwa m-Tanzania tunaanza kuona mushkeli. Binafsi sioni tatizo la mtu yeyote mwenye asili ya Tanzania kujiita m-Tanzania hata kama ana uraia wa nchi nyingine. Huyu akiulizwa uraia wake hata siku moja hatajibu ni Tanzania lakini kwa nini azuiwe kusema yeye ni m-Tanzania wa asili?

Amandla......

Hehe mbona unataka kuforsi kingi mzee? Wapi nimesama anajivunia m-Tanzania?
Ninachosema mimi ni Mtanzania ni ntu mwenye uraia wa Tanzania, ukiwa na uraia wa nchi nyingine wewe sio Mtanzania tena. Unaweza ukawa na Utanzania bado, lakini si Mtanzania. Yaani Mtanzania ni technical term inayomaanisha una Uraia wa Tanzania.

Pia hizo nchi nyingi ulizozitaja zinaruhusu uraia wa nchi mbili, kwa Mwingereza anayechukua uraia wa marekani haachi kuwa Mwingereza, tofauti na sisi ambao tunaambiwa tunataka kula kotekote, halafu akifanikiwa tunadai Mtanzania!
 
Hehe mbona unataka kuforsi kingi mzee? Wapi nimesama anajivunia m-Tanzania?
Ninachosema mimi ni Mtanzania ni ntu mwenye uraia wa Tanzania, ukiwa na uraia wa nchi nyingine wewe sio Mtanzania tena. Unaweza ukawa na Utanzania bado, lakini si Mtanzania. Yaani Mtanzania ni technical term inayomaanisha una Uraia wa Tanzania.

Pia hizo nchi nyingi ulizozitaja zinaruhusu uraia wa nchi mbili, kwa Mwingereza anayechukua uraia wa marekani haachi kuwa Mwingereza, tofauti na sisi ambao tunaambiwa tunataka kula kotekote, halafu akifanikiwa tunadai Mtanzania!

Habari inasema ni Mtanzania, sio ana Utanzania. Julius amepoteza kuitwa Mtanzania, kwa hiyo hii habari iko off.
Huo Utanzania sijui ni nini?

Kama inaamaanisha ana asili ya TZ basi sawa, otherwise huo Utanzania nadhani uko kwenye individual basis, kuna wanaojivunia na wasioutaka kabisa huo Utanzania. Labda hata Mwingereza aliyeishi miaka mingi Bongo tunaweza tukasema ana Utanzania, its open to interpretation nadhani.

Hatubishani. Tunajaribu kufahamishana. Haya si maneno yako mwenyewe?

Dual citizenship inafanya kazi kama nchi zote mbili zinautambua. Muingereza anayechukua uraia wa Tanzania anapoteza uraia wa Uingereza lakini si uingereza wake. Ndiyo maana uingereza kuna mjadala mkubwa wa nani ni muingereza. Je, mtu mweusi ambaye ni raia wa uingereza ana haki ya kujiita muingereza? Kwa mtazamo wa NF, hapana, maana kwao uingereza ni ethnicity. Hata nchi nyingine zina mtazamo huo. Kwa mfano, raia wa India ambaye pia ana uasili wa nchi hiyo hata akichukua uraia wa nchi nyingine hapotezi uhindi wake ( hapa najua nitashambuliwa na watu makini). Huyu akirudi kwenye asili yake na kujiita mhindi hamna atakaemshangaa. Uhindi kwa hali hiyo ni tofauti na uraia wa India. Sonia Gandhi ni raia wa India lakini si mhindi. Yeye anahesabika kama mtaliano aliye raia wa India. Ninavyoona mimi, sisi huu u-Tanzania tunautumia selectively. Huyu Thakkar u-Tanzania wake umetia shaka kutokana na rangi yake wakati Julius hata akija na kitabu chake bluu na kujiita m-Tanzania hatutamshangaa. Ninavyoona mimi tuna haja ya kujadili na kutafuta maana hasa ya u-Tanzania na kuangalia kama hii definition ya kisheria ambayo wengine mnaisisitizia ina nafasi katika nchi ambayo inazidi kuwa ya mchanganyiko. Ni mjadala tu na si kingine.

Amandla......
 
Hatubishani. Tunajaribu kufahamishana. Haya si maneno yako mwenyewe?

Dual citizenship inafanya kazi kama nchi zote mbili zinautambua. Muingereza anayechukua uraia wa Tanzania anapoteza uraia wa Uingereza lakini si uingereza wake. Ndiyo maana uingereza kuna mjadala mkubwa wa nani ni muingereza. Je, mtu mweusi ambaye ni raia wa uingereza ana haki ya kujiita muingereza? Kwa mtazamo wa NF, hapana, maana kwao uingereza ni ethnicity. Hata nchi nyingine zina mtazamo huo. Kwa mfano, raia wa India ambaye pia ana uasili wa nchi hiyo hata akichukua uraia wa nchi nyingine hapotezi uhindi wake ( hapa najua nitashambuliwa na watu makini). Huyu akirudi kwenye asili yake na kujiita mhindi hamna atakaemshangaa. Uhindi kwa hali hiyo ni tofauti na uraia wa India. Sonia Gandhi ni raia wa India lakini si mhindi. Yeye anahesabika kama mtaliano aliye raia wa India. Ninavyoona mimi, sisi huu u-Tanzania tunautumia selectively. Huyu Thakkar u-Tanzania wake umetia shaka kutokana na rangi yake wakati Julius hata akija na kitabu chake bluu na kujiita m-Tanzania hatutamshangaa. Ninavyoona mimi tuna haja ya kujadili na kutafuta maana hasa ya u-Tanzania na kuangalia kama hii definition ya kisheria ambayo wengine mnaisisitizia ina nafasi katika nchi ambayo inazidi kuwa ya mchanganyiko. Ni mjadala tu na si kingine.

Amandla......

Habari kwani inasemaje? Si inasema Mtanzania kwenye headline kabisa? Sielewi unachojaribu kusema hapo labda.
Ilitakiwa iseme Raia wa UAE mwenye asili ya Tanzania, au mwenye "Utanzania".

Mtanzania ni mtu mwenye uraia wa Tanzania, zaidi ya hapo italeta ubaguzi tu. Hao NF sijui ni nani, labda utusaidie.

Mhindi ni kama Mchaga au Mpogoro vile haibadiliki ukibadili uraia.

U-tanzania ni subjective, hakuna strict definition kuna mtu atasema mpaka uzaliwe TZ, kuna mwengine atasema hata kama umezaliwa nje na wazazi watanzania, na mimi nitasema hata kama umekaa TZ miaka mingi utakuwa na Utanzania.
 
Habari kwani inasemaje? Si inasema Mtanzania kwenye headline kabisa? Sielewi unachojaribu kusema hapo labda.
Ilitakiwa iseme Raia wa UAE mwenye asili ya Tanzania, au mwenye "Utanzania".

Mtanzania ni mtu mwenye uraia wa Tanzania, zaidi ya hapo italeta ubaguzi tu. Hao NF sijui ni nani, labda utusaidie.

Mhindi ni kama Mchaga au Mpogoro vile haibadiliki ukibadili uraia.

U-tanzania ni subjective, hakuna strict definition kuna mtu atasema mpaka uzaliwe TZ, kuna mwengine atasema hata kama umezaliwa nje na wazazi watanzania, na mimi nitasema hata kama umekaa TZ miaka mingi utakuwa na Utanzania.

ASHISH Thakkar anatarajia kuwa Mtanzania wa kwanza kwenda mwezini wakati atakapofanya safari hiyo mwakani.

Mtanzania huyo, ambaye ni chotara wa Kiingereza alienda Ikulu jijini Dar es salaam jana kumueleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu safari yake na kumuaga.

Thakkar, ambaye mama yake ni mzaliwa wa Mwanza na baba Uingereza, alimwambia rais kuwa anajisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika, na hasa Tanzania kwenye safari hiyo ya angani.
Kichwa cha habari kinasema Mtanzania kuandika...... Hata kabla ya kubadilishwa kilisema mtanzania. Habari inaongezea kuwa yeye ni chotara, mama yake akiwa mzaliwa wa Mwanza ( ambayo si uthibitisho wa uraia wake maana sisi mfumo wetu wa uraia ni jus sanguinis na si jus soli kama Marekani)) na baba yake ni mzaliwa wa Uingereza (ambayo nayo si uthibitisho wa uraia wake maana nao waingereza mfumo wao ni kama wetu). Habari zilizoletwa baadae zinamzungumzia kama mkazi wa Dubai, ambayo tena haina uhusiano wowote na uraia wake. Hata katika uwakilishi wake, taarifa inasema atajivunia kuwa mwakilishi wa Afrika halafu Tanzania. Tangu lini uwakilishi informal kama huo umehusika na uraia? Kwa mfano Aliaune Damala Bouga Time Puru Nacka Lu Lu Lu Badara Akon Thiam ( Akon) ni mmarekani lakini anajivunia asili yake ya Senegal. Anabeba bendera ya nchi ya wazazi wake kila aendako. Wycleaf Jean ni mmarekani lakini anabeba bendera ya nchi ya asili yake, Haiti. Utaona mpaka sasa hakuna mahali palipozungumzia uraia wake bali uasili wake. Kwa vile mwandishi wa habari hii aliamua kumuita m-Tanzania basi wengine walihoji hilo wakidai kama unavyodai wewe kuwa m-Tanzania ni yule mwenye uraia wa Tanzania peke yake. Mimi msimamo huu ndiyo nimeuhoji kwa sababu sioni kwa nini mtu mwenye asili ya u-Tanzania asijiite m-Tanzania hata kama ni raia wa nchi nyingine. Huko ughaibuni vyama vingi vya wa-Tanzania vinabebwa na wa-Tanzania wasio raia wa Tanzania. Ninachosema mimi ni kuwa wakati umefika wa kutofautisha kati ya u-Tanzania wa asili na ule wa uraia. Mtu yeyote mwenye asili ya Tanzania awe na haki ya kujiita mTanzania bila kujali uraia wake. Kwangu mimi mtu mwenye asili ya Tanzania ni yule ambae angalau mmoja wa wazazi wake alikuwa m-Tanzania wa kuzaliwa. Na wale wenye uraia wa kuomba nao watakuwa na haki hiyo vile vile ingawa haki hiyo haitaenda kwa watoto wao ambao hawakuzaliwa Tanzania na si raia wa Tanzania. Sasa huo ubaguzi unaodai uko wapi?


Mhindi si kama mchaga au mpogoro. Hao ni sawa na wapunjabi, wagujarati, watelugu, wakannada, wakonkani, wamalayalam, wamarathi, watamil, wabengali n.k. Uhindi kama u-Tanzania ni jumuisho la makabila yote ya India.



Na NF ni kifupi cha British National Front. Taarifa zake za ziada utazipata hapa:[ame="http://en.wikipedia.org/wiki/British_National_Front"] http://en.wikipedia.org/wiki/British_National_Front[/ame]


Sasa kama unataka mjadala tuendelee lakini kama ni biashara ya kupimana vifua, mimi huko simo.


Amandla........
 
Na wasiwasi sana na huu uandishi wa kishabiki, akiambiwa anakwenda mwezini na yeye anarukia bila ya kuchunguza
 
Back
Top Bottom