PROFESA KYANDO
Member
- Jul 24, 2012
- 81
- 6
[h=2][/h] Ijumaa, Agosti 24, 2012 05:46 Na Elizabeth Mjatta
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), David Msuya, amekitaka chama chake kubadilisha mfumo wa kumpata Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, ili nafasi hiyo iwe ya kugombea.
Msuya alisema mfumo wa sasa wa kumteua kiongozi huyo wa chama, unawanyima fursa watu wenye uwezo wa kushika nafasi hiyo na matokeo yake nafasi inapwaya.
Mimi nataka nafasi hii iwe ya kugombea kama nafasi nyingine, yaani itangazwe na ikiwa hivyo na mimi nitachukua fomu kwa sababu naona naweza kushika nafasi hiyo, nina uwezo, nataka niingie niondoe mfumo mbovu uliopo.
Sasa hivi mfumo ni mbovu, watu wanaomba kugombea nafasi za uongozi majina yanakatwa hovyo, mimi nipo muda mrefu ndani ya chama toka mwaka 1996, mambo haya hayakuwepo, lakini nashangaa kuona Pius Msekwa kama Makamu mwenyekiti hasemi chochote.
Mimi naona sasa hivi Msekwa amechoka, inabidi nafasi ile aachie vijana kwa sababu nafasi yake ni kubwa, kwani inamwezesha kukutana na Rais, lakini nashangaa sioni kama anafikisha malalamiko ya wananchi kwa rais ili kufanya mabadiliko, alisema Msuya.
Mbali na Msekwa, alisema pia kwamba, wapo pia baadhi ya viongozi wa chama hicho waliopo kisiasa na siyo kwa maslahi ya chama.
Kwa mfano, mtu kama Nape utasema ni kiongozi wa aina gani, Nape ameingia kisiasa zaidi ya utendaji, matokeo yake amekuwa mtu wa kujibu hoja za wapinzani bila kuzifanyia utafiti wa kina.
Wakati mwingine CHADEMA ni wajanja, wanatoa hoja kwa kututega, wanajua kabisa kwamba CCM ni dhaifu, lazima watajibu, alisema Msuya.
Alisema kwamba, alitegemea Nape kama Katibu Mwenezi angeweka mikakati ya kuwafanya vijana wasitoke ndani ya chama, badala yake mwanasiasa huyo anaanza kuzungumzia majina ya watu na kujibu hoja za wapinzani.
Kwa nini Nape asiangalie CHADEMA wanatumia mbinu gani kuwashawishi vijana kujiunga na chama chao, kwa nini asiangalie ni mbinu gani wanazitumia hadi kushawishi watu kujaa kwenye mikutano yao, haya mambo ya kukurupukia hoja aachane nayo na anatakiwa kuangalia mbinu za kukijenga chama, alisema.
Alisema viongozi hao wameshindwa kuwajibika ipasavyo ndani ya chama hadi kukifanya chama kukimbiwa na vijana.
Ushauri wangu ni kwamba, mtu anayeona ameshindwa kukitumikia chama aondoke, akae pembeni na si kukimbilia kwenye vyombo vya habari kuchafua majina ya watu na kujibu hoja bila kuzifanyia utafiti, alisema.
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), David Msuya, amekitaka chama chake kubadilisha mfumo wa kumpata Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, ili nafasi hiyo iwe ya kugombea.
Msuya alisema mfumo wa sasa wa kumteua kiongozi huyo wa chama, unawanyima fursa watu wenye uwezo wa kushika nafasi hiyo na matokeo yake nafasi inapwaya.
Mimi nataka nafasi hii iwe ya kugombea kama nafasi nyingine, yaani itangazwe na ikiwa hivyo na mimi nitachukua fomu kwa sababu naona naweza kushika nafasi hiyo, nina uwezo, nataka niingie niondoe mfumo mbovu uliopo.
Sasa hivi mfumo ni mbovu, watu wanaomba kugombea nafasi za uongozi majina yanakatwa hovyo, mimi nipo muda mrefu ndani ya chama toka mwaka 1996, mambo haya hayakuwepo, lakini nashangaa kuona Pius Msekwa kama Makamu mwenyekiti hasemi chochote.
Mimi naona sasa hivi Msekwa amechoka, inabidi nafasi ile aachie vijana kwa sababu nafasi yake ni kubwa, kwani inamwezesha kukutana na Rais, lakini nashangaa sioni kama anafikisha malalamiko ya wananchi kwa rais ili kufanya mabadiliko, alisema Msuya.
Mbali na Msekwa, alisema pia kwamba, wapo pia baadhi ya viongozi wa chama hicho waliopo kisiasa na siyo kwa maslahi ya chama.
Kwa mfano, mtu kama Nape utasema ni kiongozi wa aina gani, Nape ameingia kisiasa zaidi ya utendaji, matokeo yake amekuwa mtu wa kujibu hoja za wapinzani bila kuzifanyia utafiti wa kina.
Wakati mwingine CHADEMA ni wajanja, wanatoa hoja kwa kututega, wanajua kabisa kwamba CCM ni dhaifu, lazima watajibu, alisema Msuya.
Alisema kwamba, alitegemea Nape kama Katibu Mwenezi angeweka mikakati ya kuwafanya vijana wasitoke ndani ya chama, badala yake mwanasiasa huyo anaanza kuzungumzia majina ya watu na kujibu hoja za wapinzani.
Kwa nini Nape asiangalie CHADEMA wanatumia mbinu gani kuwashawishi vijana kujiunga na chama chao, kwa nini asiangalie ni mbinu gani wanazitumia hadi kushawishi watu kujaa kwenye mikutano yao, haya mambo ya kukurupukia hoja aachane nayo na anatakiwa kuangalia mbinu za kukijenga chama, alisema.
Alisema viongozi hao wameshindwa kuwajibika ipasavyo ndani ya chama hadi kukifanya chama kukimbiwa na vijana.
Ushauri wangu ni kwamba, mtu anayeona ameshindwa kukitumikia chama aondoke, akae pembeni na si kukimbilia kwenye vyombo vya habari kuchafua majina ya watu na kujibu hoja bila kuzifanyia utafiti, alisema.