Butola
JF-Expert Member
- Jan 19, 2010
- 2,290
- 756
RIP Abdallah Ramadhani
Continue Resting in Peace mate!Herri Makange
Rejea
RIP Abdallah Ramadhani
Wanabodi,
Mtangazaji nyota wa Channel Ten, Abdallah Ramadhani, amefariki dunia leo kwa ajali ya gari huko Msumbiji akirejea nchini Tanzania kutokea Afrika Kusini, alikofuata Prado yake.
Habari hizi ni kwa mujibu wa taarifa ya habari ya Channel Ten ya saa moja usiku.
Huu ni msiba mwingine kwa Mtangazaji wa Channel Ten kupoteza maisha kwa ajali ndani ya kipindi cha chini ya miaka miwili. Herri Makange alimtangulia. Wote wameacha wajane na mtoto mmoja.
Abdalah Ramadhani alikuwa ni mmoja kati ya watangazaji wachache wa Channel Ten ambaye alikuwa ni ever smilling.
Poleni sana wanafamilia, Channel Ten na wanahabari kwa ujumla kumpoteza kijana huyu mahiri aliyekuwa amechipukia vizuri kwenye umahiri akielekea kwenye kubobea.
Mungu aipumzishe roho ya Abdalah Ramadhani, mhala pema peponi, apumzike kwa amani -Amen.
RIP Abdalah Ramadhani.