nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
Chanzo: Raia Mwema
WAKATI Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikisubiri matokeo ya kamati teule ya rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, habari zinasema kwamba Rais Jakaya Kikwete anajipanga kuingia katika uchaguzi wa mwakani bila ya mtandao 'uliomsaidia' mwaka 2005 kwa vile amegundua unaweza kumponza. Hiyo inafuatia mtafaruku ndani ya CCM unaoelezwa unachochewa zaidi na Katibu Mkuu wake, Yusuf Makamba kwa upande mmoja, mivutano ya makundi ndani ya mtandao wa 2005 na mfumo wa Rais wa kuchelea kuwaudhi baadhi ya watu, Raia Mwema imeambiwa.
Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya watendaji wa karibu na Rais zinaeleza kuwa, hakuna uwezekano wowote kwa Rais Kikwete kubwaga manyanga katika Uchaguzi Mkuu mwakani na ameanza harakati za kujihakikishia kurejea Ikulu, akikwepa rekodi ya kuwa Rais aliyekaa madarakani muda mfupi kuliko masharti ya Katiba.
Taarifa za kiintelijensia zinaeleza kwamba tayari Kikwete amekwisha kuanza kufanya mikakati ya chini kwa chini ikiwa ni pamoja na kuandaa makundi ya vijana ambao wameanza kuahidiwa nafasi kadhaa za kisiasa na kiutendaji baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010 kama njia ya kuwafanya wawe watiifu kwake..."
kwa maoni yangu JK HAWEZI KUINGIA KWENYE UCHAGUZI BILA KUTEGEMEA HIVI VIKUNDI NA BADALA YAKE AKATUMIA MAKADA WA PALE MAKAO MAKUU ILI KUEOUSHA KULIPANA FADHILA HUKO MBELENI, je taifa linamuhitaji Rais mwenye ubia na wakora bado ?
WAKATI Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikisubiri matokeo ya kamati teule ya rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, habari zinasema kwamba Rais Jakaya Kikwete anajipanga kuingia katika uchaguzi wa mwakani bila ya mtandao 'uliomsaidia' mwaka 2005 kwa vile amegundua unaweza kumponza. Hiyo inafuatia mtafaruku ndani ya CCM unaoelezwa unachochewa zaidi na Katibu Mkuu wake, Yusuf Makamba kwa upande mmoja, mivutano ya makundi ndani ya mtandao wa 2005 na mfumo wa Rais wa kuchelea kuwaudhi baadhi ya watu, Raia Mwema imeambiwa.
Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya watendaji wa karibu na Rais zinaeleza kuwa, hakuna uwezekano wowote kwa Rais Kikwete kubwaga manyanga katika Uchaguzi Mkuu mwakani na ameanza harakati za kujihakikishia kurejea Ikulu, akikwepa rekodi ya kuwa Rais aliyekaa madarakani muda mfupi kuliko masharti ya Katiba.
Taarifa za kiintelijensia zinaeleza kwamba tayari Kikwete amekwisha kuanza kufanya mikakati ya chini kwa chini ikiwa ni pamoja na kuandaa makundi ya vijana ambao wameanza kuahidiwa nafasi kadhaa za kisiasa na kiutendaji baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010 kama njia ya kuwafanya wawe watiifu kwake..."
kwa maoni yangu JK HAWEZI KUINGIA KWENYE UCHAGUZI BILA KUTEGEMEA HIVI VIKUNDI NA BADALA YAKE AKATUMIA MAKADA WA PALE MAKAO MAKUU ILI KUEOUSHA KULIPANA FADHILA HUKO MBELENI, je taifa linamuhitaji Rais mwenye ubia na wakora bado ?