Ndo wapi hapo Ubaya ubaya?
Au tukija via private kuna alama gani?
Unashuka Tabata relini halafu unatembea klilomita moja kuelekea St. Mary College, kisha unakata kushoto unatemeba mpaka Ubaya Ubaya, halafu unaingia kulia unashuka bondeni utanikuta mzee mzima niko kaunta mwenyewe nasongesha
Songesha kwanza baadae na vyumba vya mapumziko mafupi , vitahitajika.
Hii ni Pub tu ndugu zangu, maalum kwa Nyama choma, ndizi choma, na mchemsho wa kuku wa kufa mtu, karibuni. Kwa leo pekee yake mimi na Mtambuzi tutakuwa tunawahudumia kwa nyama choma, njoo ushuhudie mwenyewe!
Hatua tano kutoka kwenye Pub kuna gest house na bei yao ni rahisi sana, chapchap buku tano tu, kulala elfu saba....
Kuna jamaa yangu amekuja jana kutoka AR kunipa taff ni bingwa wa nyama choma kule Kwa Moromboo Arusha......!
viburudisho wapo au nakuja nae?
Hauhitaji muhudumu wa ziada toka Jf?
Mimi nipo,
Na Sihitaji malipo