' Mtambuzi jipe moyo utayashinda'

Mtambuzi pole sana Mkuu,
Pole sana,
Pole sana wewe na familia yote,
ee MUNGU mtambuzi anasema 'sasa imetosha niponye na mabaya yote'.
 
We bwana weee.......... haya mambo kwa binadamu yeyote ni ya kawaida, unajuwa kuna watu wanpata mitihani na hawasemi wako kimya tu.....................

nakumbuka mwaka 2003 kama sikosei ilipotokea ajali ya basi la Msae, nilikuwa naenda kibaha kwa shughuli zangu, nilikuwa nimekaa siti moja na jamaa mmoja ambaye tulitokea kuzoeana na kupiga stori kama kawaida, alionekana kuwa mchangamfu sana kwangu utadhani tunafahamiana kwa siku nyingi. Tulipofika Kibaha, tulishuka na kuagana. nilifika kwa mwenyeji wangu nikaambiwa yuko Tumbi Hospitalini kaenda kumuona mtoto wa dada yake ameungua na maji ya moto, niliamua kwenda huko Tumbi Hospitali ili kumuona mgonjwa, nilipofika nilimkuta yule bwana niliyekuwa nimekaa naye kwenye daladala akiwa pale nje na jamaa watatu wakiongea, nilimfuata na kumuuliza mbona yuko pale. Alinijulisha kwamba amekwenda pale kutambua maiti kwani katika ajali iya basi lam Air Msae amempoteza mkewe na mtoto wake mchanga na mdogo wake wa kike aliyekuwa kidato cha pili,, mkewe alikwenda kujifungua huko Moshi na ndiyo alikuwa anarudi kuungana na mumewe............... hii ina maana kwamba hata hakupata bahati ya kumpakata mwanae akiwa hai ambaye ndiye alikuwa wa kwanza kuzaliwa tangu wafunge ndoa na mkewe mwaka mmoja uliopita!

Nilishangazwa sana na ujasiri wa yule bwana, na nilijifunza mengi kupitia kwake, kwamba pale tunapopata matatizo tusipige mayowe, kuna walio na matatizo zaidi yetu...........................

Pole sana Baba,

Nimefurahishwa sana na ujasiri wako,
Ninashukuru kwa kutupa short story ili nasi tuwe na uvumilivu na mitihani tunayoipata, ni kweli tukipata baadhi ya mitihani tunakata tamaa kabisa na kila kitu na tunaona kwamba sisi ndio tulioonewa, lakini kumbe wapo baadhi ya watu miongoni mwetu wana kila mitihani lakini wanakuwa na subra na kuhimili hiyo mitihani, hata MOLA wetu wa REHMA, anatuambia katika vitabu vyake kuwa, "Hampi mja mtihani isipokuwa anajua SUBRA yake iko vipi, na mtihani huo ataushinda vipi", na wale waliokuwa na subra na kutegemea rehma kutoka kwa yeye aliyejuu ndio mfano wako, na wale wanaoshindwa ndio haooooooooooooo wanakimbilia kwa sangoma.
Hii inatupa faraja ya kwamba na sisi tujifunze kuwa na subra ktk mitihani tunayopata sio tupige kelele '''''MUNGU weeeeeeeee nimekukosea nini mie, kwa nini ulinileta duniani niteseke''''''''''.

Nina imani kwenye vile ulivyopoteza MUNGU atakuletea vingine vilivyo bora.





 
Matukio kama hayo ni mitihani kwa Mungu, yanapima imani. Jipe moyo mungu yu pamoja nanyi, epuka usije ukamkufuru muumba.
 
Back
Top Bottom