Mtaji wa (tzs ) millioni 4 unaweza kuanzisha biashara gani? Naomba msaada wadau wa biashara.

Samahani kama ntakukwaza coz sijui imani yako.Biashara ya kibanda cha kiti moto inalipa vizuri sana hata ukiwa na mtaji wa milioni 2 tu.Hakikisha unapata vijana wawili sharp na eneo lisilo rasmi saana na iwe ni kwenye viunga vya mji kama uko Dar namaanisha maeneo kama Tabata,Ukonga ambayo mahitaji ni makubwa ila outlets bado ni chache na hayana imani kali wengi.Ukipata eneo la kibanda hata kama utalipa elfu 50 kwa mwezi ukapata na friza ya mtumba ya laki 2 kwa ajili ya kutinzia then jiko la gezi linaweza kukugharimu laki moja na structura ya kuuzia mathalani lako 2 au 3 hivi coz haipaswi kuwa rasmi sana though hygiene iwe ni driving factor.

Hii una uhakika wa kuwa unaiona hela yako kila siku na kuamua ipi irudi na ipi usevu au utanue biashara zaidi.
hili neno kwa hela hiyo inatosha kuweka na kinywaji cha kushushia na itakulipa tuu.
 
biashara ya mazao inahitaji mtaji kubwa
sanasana kwenye0gunia 1 unaweza kujikuta unalilia 3000-5000 hapo mazao yapo
juu msimu kama0huu hakuna faida, kwahiyo hapo inabidi ununue mazao mengi
 
fafanueni basi.kivipi?mazao gani?wapi?

kama unamdau kanda ya kati.... Kuna zao linaitwa ALIZETI... Hili hukuhakikishia faida mara tatu ya mtaji wako... Unanunua kwa wakulima kipindi kama hiki cha mavuno unaweka store hadi iadimike then unaikamua mafuta,mashudu unauza... Tafuta more infos sbt hili zao
 
hiyo pesa inatosha sana nduguyangu but be creativity kila utakachofanya wapo wanafanikiwa nawanao fail so muhimu ni kuwa wa kipekee tu lolote lile utafanikiwa cha msingi ni kuangalia eneo na biashara unayoifanya basii!!!!!
 
kuwa makini na hao wanaokwambia njoo sehemu fulani au nicheki kwenye email yangu,wanaweza kukupa dili za kukulamba huo mtaji wako. hata kama ni mia mbili ni yako,achana na hao watahabishaji wanaokwambia huo ni mshahara wa mwezi au haitoshi.nani kawaambia mtaji ni pesa tu?kuna akili,ujuzi na nguvu pia ni mtaji.
 
Thanks , kwa ushauri wako wa dhati. wangeweka wazi biashara gani sio kwaajili yangu tu bali kwa watu wengine wenye shida kama yangu waone.
 
Wadau what matters is not how much you have,but how do u spend the litle you have.4million ni pesa nyingi sana.Unapasawa kuchagua aina ya biashara amboyo mtaji huo unakidhi.Mfano wa biashara hizo ni:
-fundua duka la usambazaji mikate.
-huduma za MPESA/TIGO PESA/ZPESA NA AIRTEL MONEY.
-Mradi wa ufugaji kuku wa nyama,endapo unaeneo lenye kukidhi mradi huo.
-BBQ na huduma kama ziambatanozo na biashara hii.
-Tafuta vijana waaminifu ununue mashine za kutengeneza bisi maeneo yaliyo na watu wengi.
-Nunua Mchele msimu wa uvunaji uulete DSM utauza baada ya miezi miwili au mitatu na utatengeneza faida.
NB Shughuri hizi na nyingine nyingi zinafana zikitendwa na mtu asiye nia makuu kwa haraka,pia zingatia uwezo wako utokao ndani ya moyo wako.usifanye biashara usiyo na furaha nayo eti kisa wengi tumekushauri hivyo.Ni jukumu lako wewe na mwenzi wako kuchagua nini mfanye mkizingatia mazingira yanayo wazunguka.


nakutakia ushindi na mafanikio tele pale utakapo ridhia shughuri ya kufanya,nami niliwahi pita huko lkn sasa nimeinuka,Mungu atakuinua na wewe songa mbele pasipo hofu.
 
Najua unaweza kudharau lakini biashara ya mkaa inalipa sana huwezi kukosa faida ya hadi laki kwa siku.
 
umechukua wamzi mzuri kufanya utafit kwanza,,,
1.nunua incubator ya kutotolesha yenye mayai 264 ni 1.7milion zpo za bei ndogo
2.fanya biashara ya mazao kutka mkoa ni nzuri km mbeya au sehemu ingine
3.kumbuka kusali upate mwongozo wa mwenyezi mungu
 
Chukua milioni mbili, chukua vibali vya kuvuna miti na kusafirisha njoo huku Liwale... Nunua mbao kwa bei ndogo ya buku kumi

Ukiingiza Dar ni buku 20

Trip zako 5 unakuwa milioneaaaa!!!!!!!!
 
Wadau what matters is not how much you have,but how do u spend the litle you have.4million ni pesa nyingi sana.Unapasawa kuchagua aina ya biashara amboyo mtaji huo unakidhi.Mfano wa biashara hizo ni:
-fundua duka la usambazaji mikate.
-huduma za MPESA/TIGO PESA/ZPESA NA AIRTEL MONEY.
-Mradi wa ufugaji kuku wa nyama,endapo unaeneo lenye kukidhi mradi huo.
-BBQ na huduma kama ziambatanozo na biashara hii.
-Tafuta vijana waaminifu ununue mashine za kutengeneza bisi maeneo yaliyo na watu wengi.
-Nunua Mchele msimu wa uvunaji uulete DSM utauza baada ya miezi miwili au mitatu na utatengeneza faida.
NB Shughuri hizi na nyingine nyingi zinafana zikitendwa na mtu asiye nia makuu kwa haraka,pia zingatia uwezo wako utokao ndani ya moyo wako.usifanye biashara usiyo na furaha nayo eti kisa wengi tumekushauri hivyo.Ni jukumu lako wewe na mwenzi wako kuchagua nini mfanye mkizingatia mazingira yanayo wazunguka.


nakutakia ushindi na mafanikio tele pale utakapo ridhia shughuri ya kufanya,nami niliwahi pita huko lkn sasa nimeinuka,Mungu atakuinua na wewe songa mbele pasipo hofu.

Thanks very much mdau
 
Tafuta frem nzuri lipia miezi sita (Almost 50,000/month) 300,000Fanya finishing ya hali ya juu itakayo cost about 1,000,000Kisha weka furniture za ukweli pamoja na vifaa vya kunyolea, kisha kabidhi kwa vinyozi wawili kila mmoja atakuletea 50,000 kwa wikiWeka mdada mkalii kwa ajili ya mambo ya facial na scrubing.Afu utaja niambia mwenyewe jinsi gani utakavyo mek.
 
Chukua milioni mbili, chukua vibali vya kuvuna miti na kusafirisha njoo huku Liwale... Nunua mbao kwa bei ndogo ya buku kumi

Ukiingiza Dar ni buku 20

Trip zako 5 unakuwa milioneaaaa!!!!!!!!
Hello mdau wa liwale ebu niambie upatikanaji wa vibari ukoje haswa nimeipenda hiyo biashara nilishawahi fanya miaka ya nyuma mikoa ya nyanda za juu kusini

 
kaka biashara nzuri ni ile una idea nayo au unaipenda just like a hobby vile otherwise idea zingine unabidi uzifanyie utafiti wa maana kabla hujaamua ku invest your 4m.....take your time before you commit that cash to nay business.
 
Back
Top Bottom