Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Zanzibar Spices
Hao wanaokata tamaa kufanya biashara za kilimo niwazee wa simple gum boots kwao sum na adui

Hahaha,nikweli mkuu.
Yaani unakuta mtu analamikaa,ukiagalia changamoto zenyewe ni zakawaida.Wakati huo huo kuna changamoto watu wanakumbana nazo ukiambiwa unaweza kusema kweli hakuna pesa rahisi na wengine hukimbia kabisaa hata kama walikuwa na pesa kidogo ya kuboost.
Ila ukiona shamba la mwenzio limependeza basi unaona kama vile limeletwa na malaika,unaweza kukuta shamba hilo unaloona limependeza,miaka miwili nyuma mwenye shamba alikula hasara kubwa kabla ya kujipanga upya.Sasa unakuta baadhi yetu tunachukulia mafanikio ya kilimo kwa kukuta shamba la mwenzio limenawiri vizuri na kuona kwamba na wewe ukianza tu inakuwa kama hivyo.
Wakulima wana siri kubwa saana,ndio maana raha ya kilimo ni kwamba ingia ucheze rhythm ya wakulima ndio utajua.Unaweza kuchukua hatua zoote lakini kikakupiga vile vile,maana dizasta nyingine za kilimo zinakuwa hazina namna wala formula.

Tena labda niwaambie kitu kimoja,mkulima wa kweli ambae Kilimo kimo kwenye dam yake na dhamira yake ya kweli,basi ni kama TEJA mla Unga au zaidi ya teja mla unga.Maana akili yake,mwenendo wake,maisha yake,yoote yanakua kikilimo kilimo tuu.Anaweza kupoteza mazao shamba lote either kwa Janga la moto au magonjwa ya mimea,lakini unamkuta amekaza,na tabasam linakujia kama vile hana shida vile au hana tatizo.Ila moyo wa Ujasiri wa dhamira ndio unampa faraja.

Sasa kutana na yule anaelima kwa kuona shamba la mwenzie na kutaka na yeye afanikiwe kaka mwenzie kirahisi.Akipata tatizo tuu,basi huwezi amini anachanganyikiwa kabisa.Na anaweza kukitukana kilimo na wakulima wote.
Na wengine huishia kusema kwamba Kazi ya Kilimo cha mashamba lazima uwe mshirikina ili shamba lako lipate mazao mazuri.Yaani ndio akili ya wakulima waigaji.Na unaweza kukuta anapolima yupo peke yake hakuna mwingine Karibu.

Na kama mkulima wa dhati na umeamua kujiripua,basi amini usiamini,kama tatizo likitokea basi usitafute mtu wakukufariji ambae sio mkulima,atakupoteza.
Mkulima hufarijiwa na mkulima mwenzie.Namkulima akipatwa na Tatizo basi wa kwanza kumfikishia ni Mkulima mwenzie.

Sasa unakuta mtu amelima then ikitokea tatizo au hasara anamtafuta mtu ambae mambo hayo sio yake ilimradi tu yeye anaona ndio wa karibu yake,we unategemea nini zaidi ya kwamba atakuambia oyaa we umeona nani kalima hapa Tanzania amefanikiwa,weee vipi acha ujinga wako,we huoni watu wanalima na hawana pa kuuzia,we mjinga sana,nilikuambia mie,na nilikuwa nakuangaliaa unavyohangaika na kulima,watu wanalima kijijini hukoo na sio mjini weee vipi,mjini biashara kijijini kulima,we nimekuambia fungua duka la sim tupige hela,umekalia kilimo.Na upuuzi mwingine teleeee.Sasa na wewe ukiambiwa hivyo,basi ukimkuta mkulima mwenzio amakumbana janga kama lako basi unamwambie the same story za kejeli,mwisho wa siku inakuwa kama vile chain fulani,ya kwamba mie nililima lakini kilimo hakina tija,ni hasara,unapoteza muda na mambo meengi,wakati ukweli ni kwamba Umekimbia kilimo na changamoto zake.

Sasa lazima pia uangalia na watu gani wanaokuzunguuka.
Huwezi kuwa na dhamira ya kulima au kufanya kilimo then ukataka ushauri kwa mtu asie mkulima.Au mtu ambae anasikia tu watu wanalima.Lazima utapata ushauri sio.

Na pindi linapotokea tatizo au hasara yoyote kwenye Kilimo,basi kuwa mbali sana na familia na ndugu na jamaa katika taarifa au tathmini ya kilimo chako.Nalisema hilo kwa kuwa nimewahi kuliona kwa Mwenzangu.Yaani alilima kwa kukodi sehem,basi alipopata tatizo ndugu zake ndio walikuwa wakwanza kumlaumu na kumkatisha tamaa kwa maneno ya kejeli,maana wakati analima na alipokuwa amefanya maamuzi hayo,walitokea ndugu zake waliotaka walipiwe ada za vyuo vya ufundi,wengine walitaka mitaji,na wengine kesi za ajabu ilimradi walijua ndugu yao alipata hela ya Udalali wa kiwanja.
Basi alipopatwa na tatizo la ng`ombe kukata njia na kufamia shamba,basi huwezi amini walishangilia ile mbaya.Yaani jamaa unamuonea huruma,maana mie nililima Pilipili na yeye alilima Nyanya.
Maana mbaya zaidi hakujua ni mifugo ya nani,maana hakukuwa mtu shambani muda ule.Sasa kumbe jamaa mmmili wa ng`omber wale alikuwa mstaarabu,kama wiki mbili hivi wakulima wenzie tukajiunga na kufanya tathmini kujua nani alifanya hivyo.Na tukaweza kumjua,na alikuwa mzee wa Kiarabu na alilipa pesa ya mazao kamili.Na wakati huo tulikuwa tumechangishana pesa kama ujirani mwema kama majirani ili alime tena.
Baada ya kumpata mmiliki wa mifugo hiyo,Basi jamaa hajaamini kama anaweza kulipwa Nyanya za mwezi na nusu kwa pesa kamili.Tumekuwa nae kama ndugu.Na anasema kwamba haamini kama ndugu zake walikuwa na kinyongo namna ile ila baada ya tukio ndio alijua.
Na alipotata hizo pesa alikaa kimyaa,wao wakaona amefulia,kumbe shamba tulimchagia upya na pesa za kuliwa mazao alilipwa pesa nzuri kweli.Na alichofanya ni kwamba alikodi shamba sehem nyingine na ni mkulima wa level nzuri sana kwa ukanda wetu ule,na shamba hili la ziada alilokodi hakuna ndugu hata mmoja analolijua zaidi ya sie,jamaa yeye ameenda mbali zaidi maana hata mkewe hajui,aisee ana hasira kweli kwa yaliyomkuta.

Sasa rafiki wa Mkulima ni mkulima mwenzie,ni bora rafiki mkulima mwenye roho mbaya kuliko ndugu ambae sio mkulima mwenye roho nzuri,maana hawa ni rahisi sana kubadilika muda wowote na kukatishana tamaa pale unapopatwa na tatizo.Lakini mkulima wa kweli atakuwa na roho mbaya lakini atakupa njia tu,then mbele utajiongoza mwenye.

Ujumbe kwa Vijana wa Kiume,Inasikitisha sana wanawake ndio wanoongoza kuwa na roho ngumu,na masugu balaa kwenye kilimo hasa ufugaji.Idadi yao inakuwa kwa kasi saana na katika kila kina mama wastan 10 ambao ni wakulima ni wawili tu ndio utakuta wamekimbia changamoto za kilimo au ufugaji,ila kwa wavulana kati 10 unaweza kukuta 7 au sita wamekimbia kilimo au ufugaji hicho.
Na hii inaonekana kwamba kina mama wanaamini kwamba kesho nayo ni siku,mie nikiona sehem la Shamba au mifugo yupo mwanamama,basi huwa hata siulizi najua hapo huyo ni milionea mtarajiwa.Yaani masugu sana aisee.Na pia wepesi sana kufuata ushauri na wengi wa kinamama sio watu wa kubahatisha ndio maana wengi wanafanikiwa.

MUNGU ULIEHAI,UTUPE NA UTUJAALIE NA SIE TUNAOTAKA KULIMA ZAIDI NA TUNAOTAKA KUANZA KILIMO, MOYO WA UVUMILIVU WA CHANGAMOTO ZA KILIMO,NA PIA MUNGU UTUPE MAAMUZI SAHIHI YA AINA YA KILIMO KULINGANA NA DHAMIRA HUSIKA.UTUONGOZE KATIKA UAMINIFU KWAKO NA KUAMINI KWAMBA WEWE NDIO MSIMAMIZI WA KILA JAMBO TUNALOAMUA NA NDIO MUONGOZAJI WAKILA JAMBO LINALOKUWA.NA PIA NDIO MTATUZI WA KILA TATIZO AU CHANGAMOTO INAYOTOKEA KWA KUTOA NJIA SAHIHI YA UTATUZI NA FARAJA,TUNAKUOMBA UTUKINGE NA KUKUKOSEA KWA KULAUMU MATOKEO HASI KATIKA MAISHA,ILA TUELEKEZE KATIKA IMANI KWAMBA TUTAMBUE HUO WOTE NI UFALME WAKO KATIKA MAJARIBU,UTUJAALIE TUSHINDE MAJARIBU BILA KUKUKOSEA KWA JINA LAKO NA UTUKUFU WAKO WA MILELE."AMEEN"
 
hii ya kukopesha nayo dili san shida kuwapata wateja, ukitangaza watakuja wengi na itapelea,

anza na watumishi wenzio.tumia M4 na riba ya 30% kwa mwezi.hakikisha unakopesha watumishi tu na ufanye siri wasijue watu wengi.collateral ni kadi yake ya bank na vyeti vya shule kama atakopa zaidi ya laki 7.
 
Zanzibar Spices
Nimefurahi sana kwa ushauri wako, umenitia moyo sana,nimeanza kuwaza kununua shamba badala ya kukodi ili niweke miundombinu ya kudumu ya umwagiliaji, najua ni ghalama lakini mafanikio yapo baadaye, ubalikiwe mkuu
 
Biashara ya mahindi kwa sasa inalipa sana, tofauti na miaka mingine miezi hii hua inashuka lkn mwaka huu haijashuka, Njombe bei ya mahindi kwa Debe ni TZS 5000 dodo ni zaidi ya 8000. Pia jaribu kucheck ni biashara ya viazi so far kwa Dar inafika 75,000 kwa gunia la kilo 100 na Mtwara 96,000 kwa gunia la kilo 100 (bei ya jumla kwa dalali) wakati bei ya kununulia viazi kwa Njombe ni 50,000 - 55,000 kwa gunia la 100Kg. so unaweza piga mahesabu hapo ukisafirisha gunia 120 au 100 za kilo 100 unatengeneza sh ngapi kwa trip moja.
Ukipeleka trip 3 unalipa mkopo wote kwa mkupuo!!!!!

mkuu kwa njombe elf 50 ni bei ya mjini vijijini ni 35-45 kulingana na kiazi chenyewe.
 
Hongereni kwa mnao to a MAWAZO yenu mazuri

vipi umepata kitu hapa e?
mimi nimeboleshwa kwa wazo nililo kua nalo kwa kuwa nitaanza mwezi wa tisa mwanzoni walio nishauri kukopesha sitafanya hivyo, bari hela nitaitunza tu hadi shamba liwe wazi nianze uwekezaji, pia nafikiria kufuata viazi mviringo tarime na kuleta hapa na mwanza angalau kwa kujaribu nianze na gunia tano ili nione soko likoje nipelekako
 
Mkuu una mawazo mazuri sana kwa kutafuta uushauri wa kibiashara ila Mimi nakushauri yafuatayo chagua moja.
1.Tafuta washauri wa biashara ambao siku hizi wako wengi.
2.Jichunguze we we una kipaji au uwezo gani halafu anzia hapo.Fundi,Mkulima,Mwandishi n.k
3.Jaribu biashara yenye mtaji mdogo halafu uone matokeo take ndio utapata picha ya biashara kubwa itakuwaje.Usione aibu hata nyanya toka kariakoo kauze mtaani kwenu uone,au SAMAKI toka ferry uza uone.Usisahau anza na mtaji mdogo mfano 120,000
 
Mnao niomba niwakopeshe mpango hasa nn utapeli au? siwezi kopesha mtu nisie mjua,Tena mnatumia ID ambazo sijawahi kuziona jf, dah. .
 
habarini za mda huu,
nimekopa milion saba na nilicho panga kufanya kimekwama, nataka niitunze hela kwa mda wa miezi mine hadi sita, ndo nii-ingize kwenye mpango, lengo ilikua kuwekeza ktk kilimo, nilikuwa nimepata ekari nne za kukodi lakini kaniomba nisubiri kidogo atoe mazao yake na nitaikodi kwa miaka kadhaa, nimefikiria niiweke ktk fixed acount kwa mda huo, nishaurini kama kuna cha zaidi cha kufanya tofauti na nilivyo waza, kwani hata vifaa vya umwagiliaji nimesitisha kununua, pia mkopo huu nimeukopa kama mtumishi.
karibuni.

pole sana kwa yaliyokukuta,usiitumie hiyo pesa hata senti tano,weka kwenye fixed a/c hilo salio wakati undmsubiri atoe hayo mazao yake.
 
Nimeshafanya baadhi ya matumizi Tena nilibahatika,badala ya kukodi nimenunua heka mbili kwa laki nane tu, shamba liko site nzuri heka moja na nusu nitakuwa na lima na nusu nitajenga mabanda ya kuku, tayari nimenunua waterpump na pipe zake ila sio za drip, nazan nikivuna nitaendelea kujipanga ngoja nisitupe yote huko. nione maendeleo kwanza
 
Nimeshafanya baadhi ya matumizi Tena nilibahatika,badala ya kukodi nimenunua heka mbili kwa laki nane tu, shamba liko site nzuri heka moja na nusu nitakuwa na lima na nusu nitajenga mabanda ya kuku, tayari nimenunua waterpump na pipe zake ila sio za drip, nazan nikivuna nitaendelea kujipanga ngoja nisitupe yote huko. nione maendeleo kwanza

Hongera sana kwa hatua uliyopiga.
 
Hongera sana kwa hatua uliyopiga.

Asante mkuu, ninashida na mtu mwenye uzoefu, drip irrigation, tank la lita ngapi linaweza kumwagilia heka moja kwa mara moja kwa zao kama nyanya au tikiti, yaani masaa matatu, hiki ndio ninacho kitafuta kwa sasa, wauzaji hawaelewi vizuri nataka mkulima mzoefu.
 
Asante mkuu, ninashida na mtu mwenye uzoefu, drip irrigation, tank la lita ngapi linaweza kumwagilia heka moja kwa mara moja kwa zao kama nyanya au tikiti, yaani masaa matatu, hiki ndio ninacho kitafuta kwa sasa, wauzaji hawaelewi vizuri nataka mkulima mzoefu.

Kuna thread moja ya kilimo cha green house humu nadhani huyo mama aliyeanzisha thread ile anaweza kukusaidia, umeshawahi iona? Nadhani pia wataalam wengine kama kina Zanzibar Spices watakuja kukusaidia.....Mimi nazidi kukuombea ufanikiwe katika kila jambo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ungekuwa sio mwajiriwa ningekushauri hiyo hela ungenunua mahindi maana mwaka huu hii bidhaa ni issue sana!
Ungefanya hivi mil3 ungekusanya mahindi na kustore na m4 ungeanza mchakamchaka wa kuchukua mahindi shamba na kuleta mjini mpaka mavuno yatakapoisha utakuwa umezalisha m3 kutoka kwenye hii4mil. Baada ya miezi4 hadi5 mahindi ya stock yangekuzalishia m6-9 nyingine.
Hiyo hela usiiweka fixed a/c haitakusaidia coz ni ndogo sana. Na wala usiipeleke direct kwenye mradi wa shamba utadunda.
Hela ya mikopo midogo km hiyo unatakiwa uingize kwenye short term liquidity projects na sio miradi patapotea km kilimo. Otherwise utalipia mkopo hewa mkuu!!
This advise is based from my own experience.


Hili bonge la wazo mkuu..mm nilianza na mtaji wa 2.mil baada ya kuacha kaz sehemu moja hiv..sasa nina mtaji wa 12mil
tafuta area nzur chukua maind sindika ..pulizia dawa vizur mjini hapa after mavuno kuisha utapiga bao kinooma...coz shamba itakuwa maindi bei juu ww unauza bei wastani tu...unauza maindi mpaka uanahisi kufa wakati fulain...wakati mwingine kuajiriwa ni kufifisha akili kufikiri tu...over
 
Back
Top Bottom