Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

...nikibadilisha hiyo pesa ya madafu kuwa Stg (£) ya malkia nitapata approx £5,000 tu,....

kuna bidhaa yeyote (hot-cake!) inayohitajika sana Tanzania, ambayo upatikanaje wake ni wa tabu huko?
 
...Vipi mambo ya Tenda jamani, maana kumbukumbu zangu kwenye magazeti ya nyumbani unakuta leo kuna tenda ya ku supply maharage jeshini, mara kesho tenda ya ku supply stationaries Muhimbili, mara tenda ya kuendesha mgahawa wa CBE...

biashara ya tenda (zabuni) mnaionaje wadau?

Mbu, mtaji wako ni mdogo na biashara za tender zinataka pesa zaidi ya hizo 10m. Ukitegemea tender unaweza kulaza familia kwa njaa na kupata maisha magumu kwani hao serikali kuwasupply si tatizo lakini wakati wa malipo utazungushwa hadi utoe rushwa. Kwa tabia hio mara ya kwanza na ya pili utafanya biashara. Lakini mara ya tatu sija ukawekwa kwa list ya mafisadi maana baada kuzungushwa sana ulipo supply mara ya kwanza na pili basi nawe unakuwa sugu na unaanza kusupply hewa upate pessa za bure nk. Mambo ya tender usiyafikirie nakushauri.
 
...Vipi mambo ya Tenda jamani, maana kumbukumbu zangu kwenye magazeti ya nyumbani unakuta leo kuna tenda ya ku supply maharage jeshini, mara kesho tenda ya ku supply stationaries Muhimbili, mara tenda ya kuendesha mgahawa wa CBE...

biashara ya tenda (zabuni) mnaionaje wadau?

Mkuu, sorry niliahidi kukushauri ukikanusha kuwa kukukwapua hizo pesa na umefafanua vizuri. Kaka so far watu wengi wametoa ushauri. Wewe pia umetoa wazo lako la tender, etc. Miaka ya nyuma nikiwa Bongo nilifungua company na kazi zangu kubwa zilikuwa supplies. Ni kweli kazi hii inalipa sana lakini upataji kazi wake ni nimgumu sana. Unatakiwa kuwa na network ya uhakika. Pia kwa supplies hiyo pesa ni ndogo kwani unaweza pata kazi ya kwanza ukatakiwa utumie say 15m na malipo yakaje say 3 weeks after say 3 weeks. Kwa namna hiyo kama huna 'rescue plane' yaani mtu wakukupa pesa kiasi chochote unachotaka muda wowote itakushinda. Ninauzoefu nayo mkuu nilifanya japo kwangu tatizo ilikuwa kupata kazi kwani nilikuwa na rescue plane anytime nikitaka pesa nikaonyesha LPO jamaa fasta ananiwezesha.

Kwakuongezea ushauri wawakuu, mi nakushauri kama unaweza kakodi ha kadhaa Dodoma ulime Zabibu soko guaranteed na Breweries mkuu
 
Mie naona Mbu uwekeze kwenye mfumo wa maji safi kule bongo, nenda sehemu ambazo hawana maji ya bomba na ukachimbe visima vya kutumia mota ya umeme ili wapate maji safi badala ya kuchota maji kwenye madimbwi. Hiyo pesa unaweza kuchimba visima 5, hapo utasaidia wananchi wenzako. Unaweza kurudisha pesa yako, iwapo utafanya kila ndoo ya maji ni shs 100.


Good idea japo sijui atachimba katika ardhi/viwanja vya nani hivyo visima. Waweza pia kuchezea kamari, ukaibuka bilionea!
 
...Vipi mambo ya Tenda jamani, maana kumbukumbu zangu kwenye magazeti ya nyumbani unakuta leo kuna tenda ya ku supply maharage jeshini, mara kesho tenda ya ku supply stationaries Muhimbili, mara tenda ya kuendesha mgahawa wa CBE...

biashara ya tenda (zabuni) mnaionaje wadau?


utajaribu pia..ila its not guranteed.
Hiyo itabidi uwe unaangalia matangazo ya tenda.....
( kwani ulishawahi ku supply chochote mahali? Kama hujawahi inaweza ikawa ngumu kupata.)
 
wajameni eeh, nimebahatika "kupata" mahala ka-Mtaji. Ni kiasi cha shs. milioni kumi tu, (10,000,000/=) za Kitanzania.

Nipeni mapendekezo nizi invest wapi, kivipi na matarajio ya faida.
(i.e biashara gani inalipa (plus location), kwa muda gani, na SWOT analysis zake)

10 million unataka kufanya biashara ndogo ndogo?
 
10 million unataka kufanya biashara ndogo ndogo?
...naaaaaaaaaam, haba na haba inshaallah nitakijaza kibaba, nami nijekuwa mjasiriamali kamili. Hata Mzee Mengi alianzia na zile peni za Bairo, na Bakhressa alianzia na lamba lamba, kisha mikate...

...hivi Quemu ndio wewe QM aka QuickMover?

Naam kaka ndio mimi.

Nafikiri ile biashara Billboards niliizungumzia tu kama mfano. Sidhani kama nilikuwa naifuatilia.

...Gotcha Bro,...Nikiwa mitaa ya Bongo, zile Billboards siku zote zinanikumbusha ule mjadala miaka miwili iliyopita;

" https://www.jamiiforums.com/habari-hoja-mchanganyiko/4131-home-place-you-dont-whant.html "
 
...naaaaaaaaaam, haba na haba inshaallah nitakijaza kibaba, nami nijekuwa mjasiriamali kamili. Hata Mzee Mengi alianzia na zile peni za Bairo, na Bakhressa alianzia na lamba lamba, kisha mikate...



...Gotcha Bro,...Nikiwa mitaa ya Bongo, zile Billboards siku zote zinanikumbusha ule mjadala miaka miwili iliyopita;

" https://www.jamiiforums.com/habari-hoja-mchanganyiko/4131-home-place-you-dont-whant.html "

Good luck bro, Dah usinikumbushe Mengi alikuwa na peni zake zinaitwa (A)laska kitu kama hicho dah walimu wamechapia sana wanafunzi kwenye viganja.
 
Nilipoingia ktk ufugaji wanyama,rafiki yangu aliamua kufanya risk assessment(analysis) ya mradi ule,akaona ni hatari tupu kuufanya.Nilipoingia tena ktk mradi wa miti (ya mbao/poles) jamaa yangu yule akafanya tena risk analysis yake. Miradi yote ninaendelea nayo. Nikamwambia tena nataka kuanza ufugaji wa nyuki,jamaa yangu bado anasisitiza juu ya usalama wa mtaji wake. Watz/waliopata elimu kidogo au sana biashara za kibongo hawaziwezi. Ukianzisha biashara fulani bongo utakaa nayo siku mbili halafu utaanza kupata photocopy nyingi hatua mbili kutoka ulipofungua wewe.

Umeshapewa ushauri mwingi tu na wanajf,ingia tu mambo mengine mbele kwa mbele.
 
Watu wengine bana?......every single coin has value, and therefore anything with value is possible to increase its value at increasing rate!.....10m is a lot of money wa jameni!


Labda kama mtu ana dhana potofu "biashara" ni nini, anaweza kudhani vinginevyo.
Put all that money in one basket is not the way to go; especially for someone entering into business venture as a newbie.
 
kaka kagombee ubunge, nakuhakikishia zinatosha sana kuukwaa. Kwa mwezi utakuwa unazalisha si chini ya milioni 7 x mwaka mmoja (miezi 12)= 74 milioni. hHiyo pia izidishe miaka 5 (miezi 60)= 7 x 60 = 420 milioni.

situation anaysis ya mradi: Kama utajitosha kupitia CCM hali itakuwa kama ifuatavyo: wekeza kiasi cha milioni tano za kuwahonga wajumbe wa NEC ofcoz wapo kama 216 hivi (wadau mtanisahihisha), jitahidi kila mjumbe alau apate elfu hamsini. Hapa kuna uwezekano mkubwa wa kupita kama ni kijana mpya japo inategemea na jimbo unalotaka kugombea. Kwa ushauri wangu achana na majimbo yenye majina maana inaweza kukufika ya Bwana Mnyika pale ubungo. Kama wewe ni mchaga basi kazi ni ndogo nenda katufute jimbo lolote pale arusha, manyara na hata moshi (achana na majimbo ya ndesamburo na dr slaa hawa wameshapita muda mrefu tu).

Jitahidi kuwahonga wenyeviti na makatibu wa ngazi ya wilaya hasa wale wa CCM na jumuiya ya vijana kama utapanga kugombea kupitia chama hicho. Pia huna haja ya kuzungumka mikoa mingi wewe deal na wale wa ngazi yako ya mkoa. Tena ushauri wangu nenda mikoa ya kusini kama huna hakika sana maana kule wabunge wengi wanahali mbaya si unajua jinsi walivyoshindwa kuwaunganisha vijana kule matokeo yake wote wanauza viatu na maji huku dar.

Kama utahiji kujua mikakati ya uchaguzi usipate shida, napatikana kwa gharama za kiasi cha milioni moja tu namaliza kazi ya kukuwekea sawa wajumbe wa halmashauri kuu. Wale wa wa jimbo wasikuumize kicha dawa ni kuwafuata kata kwa kata afu tunawaweka kwapani wajumbe wa kamati ya siasa mchezo kwisha. Tuwasiliane kwa private chat hapa hapa JF. Jambo muhimu la kuzingatia: Mfanyabiasha mzuri bni yule anayechukua HATARI katika kuwekeza. Kila la kheri.

Hii kiboko!!

Bila shaka Mkuu huko Bongo, ni uzoefu wa siasa halisi za bongo. Ni projects za walio wengi na hasa tunapoelekea 2010 na zinalipa!.
 
Hii kiboko!!

Bila shaka Mkuu huko Bongo, ni uzoefu wa siasa halisi za bongo. Ni projects za walio wengi na hasa tunapoelekea 2010 na zinalipa!.

"project ya ubunge" 10m.? haitoshi kitu..na kumbuka ni patapotea pia.
halafu nadhani hii idea inakinzana na tunacho advocate hapa JF - si tunataka kupambana na ufisadi? au?
 
Jenga Choo ya kulipia eneo la Kariakoo. Utakuwa na uhakika wa kurejesha gharama zako ndani ya muda mfupi kama ifuatavyo:

Wateja - Akina mama (200 * 100/= * 30days) = 600,000/=
- Akina baba (150 * 100/= * 30days) = 450,000/=
- Watoto/vijana/wanafunzi (200 * 100/= * 30days) = 600,000/=
JUMLA KWA MWEZI 1,650,000/=

Kwa mwaka (19,800,000), kwa miaka kumi (198,800,000/=).

Yaani baada ya miaka kumi utakuwa millionea mkubwa sana, na usisahau kurudi hapa JF na kutushukuru.

NB: Kumbuka, uzuri mmoja kwa biashara hii, haina suala la mvua wala kiangazi. Kila siku biashara inaenda.
 
Last edited:
Jenga Choo ya kulipia eneo la Kariakoo. Utakuwa na uhakika wa kurejesha gharama zako ndani ya muda mfupi kama ifuatavyo:

Wateja - Akina mama (200 * 100/= * 30days) = 600,000/=
- Akina baba (150 * 100/= * 30days) = 450,000/=
- Watoto/vijana/wanafunzi (200 * 100/= * 30days) = 600,000/=
JUMLA KWA MWEZI 1,650,000/=

Kwa mwaka (19,800,000), kwa miaka kumi (198,800,000/=).

Yaani baada ya miaka kumi utakuwa millionea mkubwa sana, na usisahau kurudi hapa JF na kutushukuru.

NB: Kumbuka, uzuri mmoja kwa biashara hii, haina suala la mvua wala kiangazi. Kila siku biashara inaenda.

hii tofauti ya bei kwa akina mama/baba inatokana na nini????
 
Bei ni ile ile Tsh. 100/=, mistake imefanyika kwenye assumption ya akinababa watakao tumia huduma hiyo kwa siku. Anyway fanya 200 badala ya 150.
 
Nilipoingia ktk ufugaji wanyama,rafiki yangu aliamua kufanya risk assessment(analysis) ya mradi ule,akaona ni hatari tupu kuufanya.Nilipoingia tena ktk mradi wa miti (ya mbao/poles) jamaa yangu yule akafanya tena risk analysis yake. Miradi yote ninaendelea nayo. Nikamwambia tena nataka kuanza ufugaji wa nyuki,jamaa yangu bado anasisitiza juu ya usalama wa mtaji wake. Watz/waliopata elimu kidogo au sana biashara za kibongo hawaziwezi. Ukianzisha biashara fulani bongo utakaa nayo siku mbili halafu utaanza kupata photocopy nyingi hatua mbili kutoka ulipofungua wewe.

Umeshapewa ushauri mwingi tu na wanajf,ingia tu mambo mengine mbele kwa mbele.

...haswaa!... hapo umemnena kila kitu. Shukrana sana Malila, nimepokea michango ya kutosha (mawazo), ilobakia sasa ni utekelezaji! Shukran.
 
Back
Top Bottom