Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
Niwapatie background kidogo: Gazeti la Jumatano la Raia mwema lilipata matangazo toka Hazina kuhusu masuala haya ya malipo ya walimu na hivyo likachapisha matangazo hayo na ndiyo msingi wa email hii:
Mwandishi bulogu yake: kijana; nyegerage, karibuni, hiki ndo kijiwe chetu sema utakachokusema!!
My Take:
Natumaini Raia Mwema watachapa hiyo barua.
Ninyi mnaojifanya kukosoa mafisadi, iweje leo mnatutapeli? inakuwaje mnatuuzia gazeti ambalo asilimia 90 ni tangazo? ni kweli mimi kama msomaji nilienda kibandani kununua tangazo au gazeti lenye habari na makala makini za kusoma na kuelewa?
mimi kijana mtanzania, jobless wenyewe mnatuita wasaka tonge, najiandaa wikinzima ili jumatano niweze kununua gazeti lenye makala na busara za waandishi lukuki nilizozizoea, naiingia kibandani na kuona gazeti limetuna, furaha ikanijaa kwamba labda jumatano hii kuna makala za nguvu, kumbe ni tangazo?
hivi hamuoni aibu kutuuzia robo gazeti na robotatu ikiwa ni tangazo tu? natambua mnafanya biashara. sawa. lakini kama mmeona leo kuna matangazo ya kuwalipa hela nyingi na yanayolazimika kuathiri utendaji wenu, kwa nini msitoe gazeti bure au kupunguza bei angalau kwa leo tu ili na sisi tusipoteze hela yetu kununua visivyotuhusu? kwa nini msituandikie juu kwamba gazeti lenu leo hii halina makala za waandishi mliowazoea na badala yake kuna tangazo ili tusiingie mkenge?
mmeniuzunisha sana na sikuamini kama pesa inaweza kununua utu wenu.
na kama mnajifanya kuwa watu huru katika masuala ya demokrasia kama makala ya LULa inavyomdai DPP, basi chapisheni barua yangu hii kwenye gazeti. vinginevyo nitajua kwamba wengi tunaojifanya wasafi sio wasafi bali tunatumia makosa ya wengine kutajirika na kupata umaarufu wa reja reja.
acheni kutafuta utajiri wa haraka wa kutuonyesha habari za kushtushwa (shocking news) juu ya gazeti wakati ndani ni matangazo tu. nimesikitishwa sana, nimefedheheswa sana na sikuafiki kitendo chenu hiki.
Mwandishi bulogu yake: kijana; nyegerage, karibuni, hiki ndo kijiwe chetu sema utakachokusema!!
My Take:
Natumaini Raia Mwema watachapa hiyo barua.