Msivunje Muungano-Dr Billal

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Written by Nasikia kichefuchefu nikikumbuka muungano // 06/02/2012 // Habari // 46 Comments

BILALI-564x272.jpg
Na John Gagarini, Kibaha
Makamu wa raisi wa Jamhuri ya Muungano amewataka Watz wasikubali kuuvunja Muungano kwa kupitia marekebisho ya katiba mpya.Aliyasema hayo jana Mlandizi Kibaha Vijijini wakati wa sherehe za kutimiza miaka 35 za kuzaliwa CCM Mkoa wa Pwani na kusema kuwa Watanzania wanapswa kudumisha Muungano na wasikubali kurubuniwa na wanasiasa wasioitakia mema nchi.
Alisema kuna baadhi ya wanasiasa wanataka kutumia marekebisho hayo kutaka kuvunja Muungano na kuleta USULTANI jambo ambalo si zuri kwani Muungano umeleta mambo mazuri na kikubwa kikiwa ni amani iliyopo. "Kama mtu anakuja kuwaambia mvunje Muungano kwa kupitia marekebisho ya katiba msikubaliane naye, kwani haitakii mema nchi yetu kqwani amani na upedo vimedumu kwa kupitia Muungano hivyo tusikubali kudanganywa: alisema Dk. Bilal


Angalia hapa SMZ mkakati wao.


Vijana Zanzibar kuajiriwa uarabuni




Vijana Zanzibar kuajiriwa uarabuni

Imeandikwa na Khatib Suleiman, Zanzibar; Tarehe: 6th February 2012 @ 15:15 Imesomwa na watu: 157; Jumla ya maoni: 0


NCHI za Kiarabu zikiwemo Oman, Qatar pamoja na Kuwait zimekubali kutoa ajira kwa vijana
wa Zanzibar katika nchi hizo.

Waziri wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Ajira na Ushirika wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Haroun Ali Suleiman alisema hayo mwishoni mwa wiki na kueleza kuwa nchi hizo zimekubali kutoa ajira na mipango ya kusaini makubaliano hayo ipo katika hatua za mwisho.
Haroun alisema viongozi wa nchi hizo tayari wamefanya mazungumzo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa lengo la kuwapatia ajira zenye maslahi bora vijana wa Zanzibar.
"Kimsingi tumekubaliana na wenzetu hawa wa nchi za Kiarabu kutupatia ajira kwa vijana wa Zanzibar ambapo makubaliano yapo katika hatua za mwisho," alisema Haroun na kuongeza kuwa lengo la SMZ ni kuhakikisha vijana wanapata ajira lakini zenye mazingira mazuri yenye heshima.
Aidha, aliitaja mikakati mingine itakayozalisha ajira ni kuimarishwa kwa vyama vya ushirika pamoja na vyama vya kuweka na kukopa (Saccos) kwa makundi ya wanawake.
"Tayari tumeanza kusajili zaidi ya vyama vya ushirika 3,000 pamoja na Saccos ambazo matumaini yetu makubwa zitazalisha ajira kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanawake," alisema Waziri huyo.
 
Taminal mpya wa International Airport Zanzibar umezaminiwa na NCHI za kiarabu,sasa najiuliza uwarabu huo usultani anao uwongea huyu muheshimiwa ni upi ? Mbona haya maneno hayaongei akiwa zanzibar ambako wananchi hawataki muungano.
 
Kama ni uarabuni ni kazi za u housegirl/boy..waarabu . Ni wabaguzi hasa...

Wawaulize walio huko wanaishije
 
Anautaka Muungano ili kulinda Cheo chake,tofauti na Muungano hana chake huyo
Pamoja mkuu! nilikuwa na mawazo hayohayo. Alivyotoswa na NEC ya ccm miaka ile bahada ya Salmin kutaka awe mbadala wake alikuwa anaponda mfumo mzima wa muungano, Sasa hivi anapigiwa saluti anausifia muungano!
 
Pamoja mkuu! nilikuwa na mawazo hayohayo. Alivyotoswa na NEC ya ccm miaka ile bahada ya Salmin kutaka awe mbadala wake alikuwa anaponda mfumo mzima wa muungano, Sasa hivi anapigiwa saluti anausifia muungano!
Anajipendekeza
 
..wazanzibari wanaopinga muungano wanapaswa kupaza sauti zao ndani ya bunge la muungano.

..tatizo wabunge wa ZNZ na wananchi wa kawaida wa ZNZ wakishafika huku Tanganyika wanapagawa na opportunities wanazozipata.

..labda niwape mfano wa Hamad Rashid Mohamed. sasa hivi anahangaika huku Tanganyika kuleta wawekezaji ktk masuala ya ujenzi wa nyumba na uzalishaji mbolea. Hamad Rashid angebaki ZNZ asingeweza kupata mradi wa kutapeli kama huo.

..mwingine ni Mzee Alli Hassan Mwinyi, ana mashamba makubwa makubwa huku Tanganyika. Huwezi kupata pande kubwa la ardhi ZNZ ukalima au ukapangisha kama huku Tanganyika.

..Mohamed Bakhresa naye ametajirika kutokana na biashara zake kuwa na soko kubwa huku Tanganyika. sidhani kama Bakhresa angekuwa hapo alipo bila makampuni yake kuwa na base huku Tanganyika.

..hata ZNZ ya enzi za SULTANI ilineemeka kwa DAMU ya WATUMWA toka Tanganyika, na biashara hiyo ilipokufa ZNZ iliendelea kuneemeka kwa JASHO la WAKWEZI na WAKULIMA toka Tanganyika.

..waZNZ wanaopinga muungano wako nje ya ZNZ au hawajapata kufika huku Tanganyika na ku-explore the opportunities that are available for them.

NB:

..masuala ya muungano yanashughulikiwa na ofisi ya makamu wa raisi.

..katika awamu hii makamu wa raisi, pamoja na waziri mwenye dhamana ya masuala ya muungano, wote ni wazanzibari.
 
Vijana Zanzibar kuajiriwa uarabuni




Vijana Zanzibar kuajiriwa uarabuni

Imeandikwa na Khatib Suleiman, Zanzibar; Tarehe: 6th February 2012 @ 15:15 Imesomwa na watu: 157; Jumla ya maoni: 0


NCHI za Kiarabu zikiwemo Oman, Qatar pamoja na Kuwait zimekubali kutoa ajira kwa vijana
wa Zanzibar katika nchi hizo.

Waziri wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Ajira na Ushirika wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Haroun Ali Suleiman alisema hayo mwishoni mwa wiki na kueleza kuwa nchi hizo zimekubali kutoa ajira na mipango ya kusaini makubaliano hayo ipo katika hatua za mwisho.
Haroun alisema viongozi wa nchi hizo tayari wamefanya mazungumzo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa lengo la kuwapatia ajira zenye maslahi bora vijana wa Zanzibar.
"Kimsingi tumekubaliana na wenzetu hawa wa nchi za Kiarabu kutupatia ajira kwa vijana wa Zanzibar ambapo makubaliano yapo katika hatua za mwisho," alisema Haroun na kuongeza kuwa lengo la SMZ ni kuhakikisha vijana wanapata ajira lakini zenye mazingira mazuri yenye heshima.
Aidha, aliitaja mikakati mingine itakayozalisha ajira ni kuimarishwa kwa vyama vya ushirika pamoja na vyama vya kuweka na kukopa (Saccos) kwa makundi ya wanawake.
"Tayari tumeanza kusajili zaidi ya vyama vya ushirika 3,000 pamoja na Saccos ambazo matumaini yetu makubwa zitazalisha ajira kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanawake," alisema Waziri huyo.

Jamani mnakumbuka wale watanzania waliojiriwa nyumbani kwa OSAMA BIN LADEN wakifundishwa ugaidi? Sasa wamerudi tena kwa sababu wameona wazanzibari wanamoyo wa kujitoa mhanga. Hawa wanakwenda kutuletea ugaidi hakuna kazi.
 
Kama ni uarabuni ni kazi za u housegirl/boy..waarabu . Ni wabaguzi hasa...

Wawaulize walio huko wanaishije

Acha unafiki wako wewe! Mimi naishi warabuni na ninafanya kazi nina miaka kibao huku,hizo kazi unazosema wewe hazipo,mahouse girl au mahouse boy ni wahindi au wafilipino sio wa africa,kaa ujue mwafrica warabuni anathamani kubwa kuliko muhindi,mfilipino au mpakistan,acha umbea wako
 
Jamani mnakumbuka wale watanzania waliojiriwa nyumbani kwa OSAMA BIN LADEN wakifundishwa ugaidi? Sasa wamerudi tena kwa sababu wameona wazanzibari wanamoyo wa kujitoa mhanga. Hawa wanakwenda kutuletea ugaidi hakuna kazi.

Sio kila thread lazima uchangie
 
Acha unafiki wako wewe! Mimi naishi warabuni na ninafanya kazi nina miaka kibao huku,hizo kazi unazosema wewe hazipo,mahouse girl au mahouse boy ni wahindi au wafilipino sio wa africa,kaa ujue mwafrica warabuni anathamani kubwa kuliko muhindi,mfilipino au mpakistan,acha umbea wako

uliwahi Kusikia BBC kile kipindi maalum kampuni flani ilikuwa inawachukuwa mabint Ws kiganda kwenda Iraq wakiwadanganya wanakwenda kufundisha english ... wakaenda kufanywa watumwa wa majumbani .. ma kuna Ile kesi m.mke wa kimombasa alipotupwa toka gorofani na mwajiri wake Dubai mpaka sasa hana uwezo wa kutembea ...

waarabu ni wa baguzi hakuna ... imagine waislam mtume asingekuwa mwarabu sijui kama wangemkubali ... hawana utu wale watu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom