Msitu wa pande

Hivi si ndo huu msitu ambao Kamanda Zombe, alituhumiwa Kuwauwa wale wafanyabiashara wa madini toka MAHENGE?
 
Kwakweli unahitajika kufyekwa kabla haujamaliza kufyeka wa TZ wengi wasio na hatia.
Nchi kama ya Hitla na Idd AMINI Inatisha sana.

Tz mh!
 
Ofisi zote za Serikali (kama vile Wizara) ziamishiwe huko ili tupunguze msongamano mjini kwani huo msitu hauna tija kwa wananchi zaidi ya kuwa machinjio ya Binadamu wasio na hatia.
 
Tuuingize katika kitabu cha GUINNESS BOOK.Maana unamatukio ya ajabu na yakutisha
 
Magwepande na Pande ni sehemu mbili tofauti.

Pande ni Bagamoyo
Hapana, si kweli, pande na mabwepande zinapakana..., kama watokea bunju b, unaanza kwanza mabwepande pande, ukiendelea mbele kdg unaanza msitu wa pande na kuna bango kubwa wameandika pande game reserve,,,

Ile barabara ya vumbi ukiendelea nayo utapita katikati ya msitu, na inaenda kutokea makabe then from makabe hadi mbezi mwisho(morogoro road)..., kuna njia nyingine pia inatokea mapinga pale darajani en route to bmoyo.., na nyingine inatokea kijiji cha zinga bagamoyo,, hii hutumiwa sana na watu wa magendo ya kutoka zanzibar kwa majahazi.., hii ya zinga sio rasmi na ni mbovu hutumika kukwepa road block ya pale mapinga, then wanakuja kuibukia bunju b
 
Wajenge vituo vya watoto yatima vya kutosha, huduma za kijamii zipelekwe pia.
 
Back
Top Bottom