Msisikitike, kuna njia ingine

uporoto01

JF-Expert Member
May 23, 2008
4,700
1,415
Miaka kadhaa iliyopita Kibaki alitaka kufanya hichi anachokifanya sasa Jakaya ya kuandika katiba anayoitaka yeye sasa baadae kutakiwa kuwa na kura ya maoni kuikubali au kukataa njia hii.Wapenda mageuzi wa kweli wakajipanga na kupita nchi nzima kuipinga na kuwashawishi watu waikatae kwa kupiga 'NO' walijulikana kama orange,na upande wa Kibaki wa 'YES' ulijulikana kama ndizi.
Upande wa 'NO' au Orange ulishinda na hivyo kumlazimisha Kibaki kutumia njia ya kuwashirikisha Wakenya wote katika kuandika na kupitisha Katiba hii nzuri waliyoipata sasa.
Kwahiyo ni kujipanga tu wakati wa kura ya maoni kuhamasisha wananchi kuikataa Katiba hii,inawezekana kila mmoja akishiriki kikamilifu.
 
Mimi binafsi kwa maoni yangu naona njia hii ni sahihi zaidi kuliko maandamano ambayo hayana athari ya moja kwa moja kubadili maamuzi haya. Tujipange kuikataa kwenye kura ya maoni na hata ukiongea na watu wengi hawajaafiki uburuzwaji uliotokea.Vote 'NO' to The State House Constitution.
 
Miaka kadhaa iliyopita Kibaki alitaka kufanya hichi anachokifanya sasa Jakaya ya kuandika katiba anayoitaka yeye sasa baadae kutakiwa kuwa na kura ya maoni kuikubali au kukataa njia hii.Wapenda mageuzi wa kweli wakajipanga na kupita nchi nzima kuipinga na kuwashawishi watu waikatae kwa kupiga 'NO' walijulikana kama orange,na upande wa Kibaki wa 'YES' ulijulikana kama ndizi.
Upande wa 'NO' au Orange ulishinda na hivyo kumlazimisha Kibaki kutumia njia ya kuwashirikisha Wakenya wote katika kuandika na kupitisha Katiba hii nzuri waliyoipata sasa.
Kwahiyo ni kujipanga tu wakati wa kura ya maoni kuhamasisha wananchi kuikataa Katiba hii,inawezekana kila mmoja akishiriki kikamilifu.

Tatizo hamsemi kweli,mnadanganya watu sijui kwa faida ya nani? kenya walikataa katiba siyo mswada wa maandalizi ya katiba.chadema wanakataa mswada wa ,maandalizi ya katiba na kwa hakili zenu ndogo mnadhani nyinyi ndo wananchi wanawapenda kuliko ccm na cuf? kama tunapima uwakilishi ndo wingin wa watu wanaopenda chama,chadema wamepata wapi takwimu kwamba wao ndo wanapendwa kuliko ccm wenye RAIS NA WABUNGE WENGI?,njoni mikoan chadema mpoteze muda kama IGUNGA,LAKINI MJUE KATIBA ITAANDIKWA NA WATANZANIA WATAIKUBALI.
 
Tatizo hamsemi kweli,mnadanganya watu sijui kwa faida ya nani? kenya walikataa katiba siyo mswada wa maandalizi ya katiba.chadema wanakataa mswada wa ,maandalizi ya katiba na kwa hakili zenu ndogo mnadhani nyinyi ndo wananchi wanawapenda kuliko ccm na cuf? kama tunapima uwakilishi ndo wingin wa watu wanaopenda chama,chadema wamepata wapi takwimu kwamba wao ndo wanapendwa kuliko ccm wenye RAIS NA WABUNGE WENGI?,njoni mikoan chadema mpoteze muda kama IGUNGA,LAKINI MJUE KATIBA ITAANDIKWA NA WATANZANIA WATAIKUBALI.
Wewe ndio muongo Kenya walikataa mchakato wa Kibaki katiba ilikuwa bado.
 
Mkuu uporoto kuna kitu nataka ujue,tukikosea step tukakubali kura ipigwe tumekwisha lazima watashinda,hakuna mtu mwenye uwezo wa kushindanna na ccm tunapoongea mambo ya kura,ni wazoefu wa kuchakachua,hilo siafiki hata kidogo
 
Mkuu uporoto kuna kitu nataka ujue,tukikosea step tukakubali kura ipigwe tumekwisha lazima watashinda,hakuna mtu mwenye uwezo wa kushindanna na ccm tunapoongea mambo ya kura,ni wazoefu wa kuchakachua,hilo siafiki hata kidogo
Mkuu hata mimi hilo kidogo linanipa wasiwasi wasimamizi si watakuwa hawa NEC ya Kivuyo ?
 
Hiyo ni ndoto ya mchana kwa tume hii ya uchaguzi itakayosimamia zoezi hilo.
Miaka kadhaa iliyopita Kibaki alitaka kufanya hichi anachokifanya sasa Jakaya ya kuandika katiba anayoitaka yeye sasa baadae kutakiwa kuwa na kura ya maoni kuikubali au kukataa njia hii.Wapenda mageuzi wa kweli wakajipanga na kupita nchi nzima kuipinga na kuwashawishi watu waikatae kwa kupiga 'NO' walijulikana kama orange,na upande wa Kibaki wa 'YES' ulijulikana kama ndizi.
Upande wa 'NO' au Orange ulishinda na hivyo kumlazimisha Kibaki kutumia njia ya kuwashirikisha Wakenya wote katika kuandika na kupitisha Katiba hii nzuri waliyoipata sasa.
Kwahiyo ni kujipanga tu wakati wa kura ya maoni kuhamasisha wananchi kuikataa Katiba hii,inawezekana kila mmoja akishiriki kikamilifu.
 
Mimi binafsi kwa maoni yangu naona njia hii ni sahihi zaidi kuliko maandamano ambayo hayana athari ya moja kwa moja kubadili maamuzi haya. Tujipange kuikataa kwenye kura ya maoni na hata ukiongea na watu wengi hawajaafiki uburuzwaji uliotokea.Vote 'NO' to The State House Constitution.

Tatizo muda Mkuu,mpaka wakati wa kura tkifika muda utakua umeenda sana,the only solution ni MAANDAMANO tu.Kwani ktk hayo maandamano tutaibua vitu vingine vingi na ikiwezekana through hayohayo maandamano tuung'oe utawala wa kidhalimu wa CCM
 
Tukirogwa tukakubali mchakato uendelee, mjue tumekwaa kisiki yawezekana hamkusikiliza hitimisho la Bi.Celena mchumba wangu.Amesema hivi: kura ya maoni itapigwa na wananchi waliojiandikisha ktk daftari la wapiga kura.Sote tunajua jinsi daftari lile lilivyo mtaji wa CCM, pili wa-magamba ni mabingwa wa kuchakachua hapo ndiyo itakuwa mwisho wa mchezo.

Nini kifanyike: watanzania tukubali hasara ya baadhi yetu kufa kwa ajili ya wengi, tuingie barabarani tupigwe risasi baadhi yetu tufe na baadhi wajeruhiwa ili watakaobaki waje wale matunda.Kwa mfano mimi nina watoto wawili nikifa watakuja kula bata watoto wangu au mnasemaje??.
Kinachotakiwa tulianzishe bila kuchelewa.
Leo tunaongelea Rwanda inafanya vizuri tunajua vizuri walikotoka??? tuulizeni sisi wana-lake zone tuliwahi kula samaki waliokula miili ya wanyarwanda, lakini leo hii Rwanda wanakula bata, tunawashuhudia akina ALPHA wa TUSKER PROJECT wakitesa lakini baba zoa walikumbana na cha moto.Wajerumani leo wanauchumi imara lakini ukisimuliwa historia yao huwezi amini. TULIANZISHE ILI TUMUENZI LEMA
 
Tena tusithubutu kuruhusu mchakato uendelee.Bora tubaki na katiba ya zamani watakuja kubadili watoto wetu.Kama tutashiriki kutengeneza katiba kupitia mswaada huu, wajukuu zetu watatushangaa tulisomaje!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mimi binafsi kwa maoni yangu naona njia hii ni sahihi zaidi kuliko maandamano ambayo hayana athari ya moja kwa moja kubadili maamuzi haya. Tujipange kuikataa kwenye kura ya maoni na hata ukiongea na watu wengi hawajaafiki uburuzwaji uliotokea.Vote 'NO' to The State House Constitution.

Tunaikataa serikali dhalimu ya jk na makinda, tunataka baraza la mpito litakalo tuongoza kupata katiba ya wananchi, hii ya jk, makinda na ccm hatuitaki.
 
Mimi binafsi kwa maoni yangu naona njia hii ni sahihi zaidi kuliko maandamano ambayo hayana athari ya moja kwa moja kubadili maamuzi haya. Tujipange kuikataa kwenye kura ya maoni na hata ukiongea na watu wengi hawajaafiki uburuzwaji uliotokea.Vote 'NO' to The State House Constitution.
Ni wazo zuri, lakini hiyo YES na NO itafanya kazi vizuri mahali ambapo mna tume huru inayosimamia huo upigaji kura. Lakini huo mswada unaipa madaraka tume tuliyo nayo ya uchaguzi (ya kikwete) jukumu la kuisimamia hiyo kura. Unategemea nini hapo?
 
Tatizo hamsemi kweli,mnadanganya watu sijui kwa faida ya nani? kenya walikataa katiba siyo mswada wa maandalizi ya katiba.chadema wanakataa mswada wa ,maandalizi ya katiba na kwa hakili zenu ndogo mnadhani nyinyi ndo wananchi wanawapenda kuliko ccm na cuf? kama tunapima uwakilishi ndo wingin wa watu wanaopenda chama,chadema wamepata wapi takwimu kwamba wao ndo wanapendwa kuliko ccm wenye RAIS NA WABUNGE WENGI?,njoni mikoan chadema mpoteze muda kama IGUNGA,LAKINI MJUE KATIBA ITAANDIKWA NA WATANZANIA WATAIKUBALI.

Linapokuwa suala la katiba, mkuu hakuna u ccm / CDM /NCCR. Unaweza kuta ndani ya ccm half wako against na hiyo rasimu, ukiwatoa mavampire yanayonyonya damu zetu
 
Tatizo hamsemi kweli,mnadanganya watu sijui kwa faida ya nani? kenya walikataa katiba siyo mswada wa maandalizi ya katiba.chadema wanakataa mswada wa ,maandalizi ya katiba na kwa hakili zenu ndogo mnadhani nyinyi ndo wananchi wanawapenda kuliko ccm na cuf? kama tunapima uwakilishi ndo wingin wa watu wanaopenda chama,chadema wamepata wapi takwimu kwamba wao ndo wanapendwa kuliko ccm wenye RAIS NA WABUNGE WENGI?,njoni mikoan chadema mpoteze muda kama IGUNGA,LAKINI MJUE KATIBA ITAANDIKWA NA WATANZANIA WATAIKUBALI.

Nimetembea nchi yote hii, yaani ccm haipendwi na walio wengi, ila sema kinachowakomboa ccm ni wizi wa kura na uelewa mdogo wa baadhi ya watanzania wenzetu, ila kwa sasa vijijini wanaelimika kwa kasi kuliko hapa mjini.
 
Mimi binafsi kwa maoni yangu naona njia hii ni sahihi zaidi kuliko maandamano ambayo hayana athari ya moja kwa moja kubadili maamuzi haya. Tujipange kuikataa kwenye kura ya maoni na hata ukiongea na watu wengi hawajaafiki uburuzwaji uliotokea.Vote 'NO' to The State House Constitution.

Sasa baada ya hapo iweje? Katiba inahitaji kabla ya 2015 voting no will send us into a dead end! suggest a better way forward rather than this Vote No thing.

 
kufanya hivyo ni kuruhusu kupoteza fedha zetu za kodi kwa kazi isiyo na maana. hapa hapa mpaka kieleweke!!!!!
 
Acheni mambo ya ajabu nyie,eti tukatae wakati wa kupiga kura ina maana tukubali kuburuzwa wakati wa mchakato kwa kuundiwa tume yenye washkaji wa CCM,bunge la katiba lenye washkaji na hadidu za rejea za mtu mmoja?kama tulivyosema tukikubali sasa hivi tutaburuzwa na hata kuikataa baadaye tutashindwa.Acheni uoga nyie msidhani maandamano ndo vita kwani vita vinaweza kutokea bila hata maandamano
 
Mchakato huu hauna tofauti na mbuni aliyeficha kichwa chake shimoni hali mwili wote uko nje. Bunge limetumika kupitisha uozo mwingi sana wa serikali ya CCM, matokeo yake tunayajua. Hatujakoma tunazidi kufanya madudu yaleyale, na matokeo yatakuwa yaleyale. Mchakato mbovu, utazaa kamati mbovu, itakayokusanya maoni na kurudisha ripoti mbovu, itapelekwa kwenye bunge la katiba bovu, lenye idadi kubwa ya wawakilishi walioanzisha mchakato mbovu, watapitisha rasimu ya katiba mbovu, kwenda kupigiwa kura ya maoni itakayosimamiwa na tume mbovu. KATIBA ITAKUWA MBOVU
 
Back
Top Bottom