only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...........WanaJF wenzangu kwanza awali ya yote napenda kuwapa pole kwa matatizo haya ya umeme yanayoendelea kwa kasi...mgao huu wa umeme unaweza ukawa unaenda kufanana na ule mgao wa umeme wa 2006..Ni hali ya kuhuzunisha sana ktk hali hii hakuna kiongozi mkubwa wa kitaifa halieye kubali kutoa tamko la wazi kuhusu hii hali tata..Na cha kushangaza wanawarushia mzigo TANESCO waseme..Juzi siku ya ijumaa Clouds Fm kupitia kipindi chao cha JAHAZI walifanikiwa kumpata injinia mmoja wa TANESCO kuzungumzia hilo baada ya kupata taarifa kuwa BADRA MASOUD msemaji wa TANESCO yuko nje ya nchi kikazi..kwakweli waliofanikiwa kumsikia halisema wazi kama ifuatavyo...
Inakera na inaumiza...mimi jana nimekosa umeme tangu saa 1 usiku mpaka saa 7 usiku....itakuwaje?
- Tuache siasa tatizo la umeme ni kubwa sana na akasema hitaji la Taifa ni megawatt zaidi ya 800 na kwasasa mashine zetu zinazalisha megawatt 500 tu..kwahiyo tunaupungufu wa megawatt 300 na zaidi..
- Na akasema kwa uwazi kabisa...mgao wa umeme utadumu kwa nusu mwaka wote kwa wastani wa masaa 10 mpaka 24..hii inamaana kuwa kuna siku tunaweza kosa umeme kwa siku nzima.....
Inakera na inaumiza...mimi jana nimekosa umeme tangu saa 1 usiku mpaka saa 7 usiku....itakuwaje?