Bassanda
Member
- May 14, 2009
- 53
- 3
Msimu wa utalii katika kisiwa cha Zanzibar umepamba moto mwezi huu wa Julai lakini kuna mambo na vijimambo kwa wageni wenyeji. Hivi majuzi kuna jamaa mmoja katokea Zanzibar alikuwa kaenda huko kikazi akitokea bara. Anasema imemtokea si chini ya mara mbili kuondolewa kwenye chumba cha hoteli mbili tofauti alikokuwa kafikia baada ya watalii wa kizungu kuwasili kwenye hoteli hizo. Kinachotokea ni kwamba kama wewe ni mswahili, haijalishi uwe umetokea bara, Zanzibar au kwingineko, uombe tu wasitokezee wazungu wakahitaji kupata vyumba hapo ulipo. Kama vyumba havitoshi ukiwa mswahili utaambiwa "yakhe tulisahau kukujulisha kuna wageni wanawasili leo walishafanya bukingi siku nyingi, hivyo tunakusihi utafute hoteli nyengine". Ukibahatisha kubakia, utashanga huduma kama ya breakfast inabadilika. Mtaanza kuhudumiwa hadi matunda ambayo mlikuwa hamyapati mlipokuwa wapangaji waswahili watupu. Kwa hivyo ukitokea bara ukaenda na hasira zako Unguja haitakusaidia kwani hoteli nyingi Zanzibar ndiyo mchezo wao huo, inabidi tu uwe mpole hakuna ujanja. Tunashukuru kwa bara upuuzi huo haupo na mtu akikufanyia hivyo mtafikishana pabaya, kwanza hawezi kudhubutu!