Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Wadau, juzi nikiwa safarini huko kwenye mapori mazito ya Kibondo-Kahama kutoka mwisho wa reli kurudi makazi yangu, nilipokea ujumbe wasimu kutoka kwa rafiki yanku kuwa Mzee Kawawa katutoka. Kwa kweli nilihuzunika sana, si kwa kuwa Mzee wetu katutoka, hapana (maana najua umri wake ulikuwa umesogea sana na afya yake haikuwa nzuri).
Huzuni yangu kubwa ilisababishwa na jinsi nilivyokuwa nikiisubiri kwa hamu kauli yake kuhusu mambo yanayoendelea nchini mwetu tangu Uongozi wa awamu ya 4 uingie madarakani. Nilisubiri kwa shauku kauli na msimamo wake kuhusu yafuatayo:-
1. Tuhuma za Ufisadi zinazowakabili viongozi wetu- EPA, RICHMOND, nk
2. Mparanganyiko/Msigano ulioanzishwa na Mtandao uliomuingiza JK madarakani
3. Ombwe la Uongozi linalodaiwa kuwepo nchini
4. Msimamo wake kuhusu Mdahalo wa MNF na maazimio yake kuhusu hatima ya Uongozi wa nchi yetu na nchi yetu
5. Mengineyo mengi
Kwa kuwa wazee wetu walokuwa viongozi enzi za MWalimu hadi Awamu ya wamezungumza na kutoa maoni yetu, Mzee Kawawa nilitarajia naye angetoa msimamo wake lakini kwa bahati mbaya sikubahatika kumsikia, maana mara nyingi imekuwa ni vigumu kwangu kupata habari za mambo yanayojiri kwa haraka kutokana na kuwa pembezoni-pembezoni mwa nchi ambapo hata mitando ya simu inapatikana kwa taabu.
Wadau namomba mnijuze, Mzee wetu Kawawa alituachia kauli gani kuhusu mambo yanayoendelea nchini mwetu?
Huzuni yangu kubwa ilisababishwa na jinsi nilivyokuwa nikiisubiri kwa hamu kauli yake kuhusu mambo yanayoendelea nchini mwetu tangu Uongozi wa awamu ya 4 uingie madarakani. Nilisubiri kwa shauku kauli na msimamo wake kuhusu yafuatayo:-
1. Tuhuma za Ufisadi zinazowakabili viongozi wetu- EPA, RICHMOND, nk
2. Mparanganyiko/Msigano ulioanzishwa na Mtandao uliomuingiza JK madarakani
3. Ombwe la Uongozi linalodaiwa kuwepo nchini
4. Msimamo wake kuhusu Mdahalo wa MNF na maazimio yake kuhusu hatima ya Uongozi wa nchi yetu na nchi yetu
5. Mengineyo mengi
Kwa kuwa wazee wetu walokuwa viongozi enzi za MWalimu hadi Awamu ya wamezungumza na kutoa maoni yetu, Mzee Kawawa nilitarajia naye angetoa msimamo wake lakini kwa bahati mbaya sikubahatika kumsikia, maana mara nyingi imekuwa ni vigumu kwangu kupata habari za mambo yanayojiri kwa haraka kutokana na kuwa pembezoni-pembezoni mwa nchi ambapo hata mitando ya simu inapatikana kwa taabu.
Wadau namomba mnijuze, Mzee wetu Kawawa alituachia kauli gani kuhusu mambo yanayoendelea nchini mwetu?