Msimamo wa Jeshi la Polisi kufuatia mauaji ya Raia Arusha

Ndipo hapo tutakapojua kwamba wizara ya mambo ya ndani ni ya serikali tofauti na ile ya mambo ya nje! Shaghalabagala.... tuuu (spitting)!!!
 
Mi naona iwe unatoa taarifa polisi juu ya maandamano kama intelligencia yao inawaambia tusiandamane basi ni kuwaambia kuwa tutajilinda wenyewe
 
Yeye anasema sorce, ni viongozi wa CHADEMA, kusema mkawatoe waliokamatwa polisi, Je vipi kama CDM , wangeruhusiwa kuandamana, ?, yeye anadhani haya yote yangetokea, kiufupi KILICHOSABABISHA WATU WATATU KUFA ARUSHA, NI JESHI LA POLISI KUZUIA MAANDAMANO YA CDM.
 
at standard, temperature and pressure (STP),,,, jeshi la polisi halitaweza kusema wao ndio waliovunja sheria kwa kutumia mabavu kwenye mkusanyiko wa amani.... wameshaaibika jana 12/01/2011 na wanabaki wakilumbana na serikali yao... aibu imeshawakuta sasa wanajaribu kujisafisha ...kwani wafadhili wameshawakoromea
 
Wasema hawakukosea, Chadema ndo walikaidi amri halali ya serikali iliyoko madarakani

source BBC jioni hii
Hivi jamani MLITEGEMEA WAMESEMEJE???
Polisi wa Tanzania hawakuanza kazi ya kutumia risasi za moto jana ama juzi... ni kaugonjwa kalikopaswa kukemewa siku nyingi. Wakemeaji waliona ni sawa.. JOKA LIMEPEA sasa sijui nani mwingine wa kulizuia sasa!:eyeroll1:
 
at standard, temperature and pressure (STP),,,, jeshi la polisi halitaweza kusema wao ndio waliovunja sheria kwa kutumia mabavu kwenye mkusanyiko wa amani.... wameshaaibika jana 12/01/2011 na wanabaki wakilumbana na serikali yao... aibu imeshawakuta sasa wanajaribu kujisafisha ...kwani wafadhili wameshawakoromea
Ndugu yangu...
ACHANA NA WANASIASA!

Kama mnatarajia hao "wafadhili" Twafwaaaaa!! Ni kama rafiki aliyekwenda suluhisha ugomvi wa mtu na mkewe kisha akamkoromea sana yule mume. Mke akiona vile anajua bwana amepakiwa vilivyo - kisha yule mume na rafikie wanatoka wameshikana mikono! Soo limeisha!! Wanasifiana huko njiani na kurejea uovu wao uleule. Ni Wafadhili gani wema kwa Tanzania waliokoroma? Wale wanaopewa Mgodi wa Matrilioni kwa vyandarua vya milioni? au wale wanalioshapewa dhahabu kwa karne nzima ili watuachie mashimo na matetemeko ya ardhi miaka ijayo?

Hii ni Tanzania yetu, na tunawajibika kwayo... tusitegemee mboga ya jirani kwa ugali wetu
 
hivi ni nani waliokwenda na silaha? chadema au polisi na kwa nini waseme chadema ndio waliokosea ilihali hawakuwa na silaha yoyote? Ipo siku mambo haya yatakoma.
 
Shida ingine ni kwmb mapolisi we2 hawawez kubadilika. Mtu anaulizwa maswali anakwepa, kichwani kwake ameweka kwmb raia ni mtu wa chini sn toka kwenye nafac yake kijeshi...ujeshi-ujeshi tu hata kwny ishu sensitive za mauaji ya raia. Infact wako kwny enzi ya jeshi la luga-luga. Wanaongea juu ya dhana ya Ushirikishaji raia, kumbe ni dhana-mfu, na ya kinadharia tu.
 
Wana JF Kupitia taarifa ya habari ya BBC na CH 10 jioni hii, tumeshuhudia msemaji wa polisi akitoa tamko kuhusu mauaji ya Arusha. Tamko hilo linadai kuwa viongozi wa CHADEMA ndo walosababisha baada ya kuwachochea waandamanaji kwenda kuvamia kituo cha polisi ili kuwakomboa watu wa CHADEMA na viongozi wao waliokamatwa na kutiwa ndani.

Swali la kujiuliza, ni jana tu Waziri Membe alitoa taarifa baada ya kumaliza mkutano wake na mabalozi, aliweka wazi kuwa Polisi walikurupuka. Sasa kati ya Membe na huyo comissioner wa polisi ni nani mwenye mamlaka makubwa yakuwahabarisha Watanzania? Sitta, Mwakyembe wanasema tusilipe Dowans, Pinda, Werema na baadhi yao , wanadai tulipe Dowans. Yupi ni yupi na nani ni nani? Hivi karibuni Wasira anasema Maaskofu waikosoe serikali mahali inapokosea, Makamba, Chitanda wao wanasema maaskofu wasiingilie siasa. Hivi hii serikali ya Kikwete inaweza kutuambia inajiendesha serikali ya aina gani? na inafuata utaratibu upi? Au tuseme sasa Mkwere ameamua yeyote anaweza endesha nchi kwa jinsi yeye anavyoona inafaa. Kuna serikali ngapi? Naomba wanaJF mnisaidie kwa hili.
 
Wakati mwingine nashawishika kuamini kwamba " huenda hata Mungu hazielewihizi akili za polisi".
Full of contradictions
 
Back
Top Bottom