Msichana wa miaka 13 afanyishwa ukahaba

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
Msichana wa miaka 13 afanyishwa ukahaba
6180206.jpg

Picha ya mmoja wa anaosadikiwa ni changudoa akiwa mawindoni
Sunday, January 08, 2012 11:52 PM
Habari kutoka Majengo Tanesco, mjini Sumbawanga zimeripoti kuwa msichana ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba alietumikishwa ngono ya lazima kwa miezi saba akitafutiwa wanaume na mwenye danguro kwa malipo ya kupewa wa mlo.
Binti huyo, jina napicha kapuni, ametoboa siri ya kutisha kuhusu biashara ya ngono inayoendelea bongo. Binti huyo amedai kuwa alirubuniwa kuondoka nyumbani kwao kisha kujikuta akitumikishwa kwenye biashara ya ngon jijini Mbeya.
Binti huyo alisema kwamba hakuwa peke yake, bali zaidi ya wasichana wadogo 30 ambao waliofungiwa nyumbani kwa tajiri wakilindwa na walinzi wenye silaha usiku na mchana, lakini usiku husambazwa kwenye majumba ya starehe kwa ajili ya kuuza miili yao, chini ya ulinzi wa mabaunsa.
 
Kumbe biashara ya ngono ime-advance namna hii? Hadi ma-CD wetu wanakuwa na pimps! Kweli tumethubutu, tumewezwa.
 
Watu wanajitafutia laana sasa, huyo tajiri ni *****e.

Tatizo serikali kwani iko wapi? Serikali inazifumbia macho hizi danguro ikidhani kwamba zinafanya biashara halali. We unafikiri wataweka mibibi kwenye hizi danguro?,lazima waweke vibinti vidogovidogo kuwavutia wanaume. Serikali ifungue macho na nyie wamiliki wa hizi danguro acheni ujinga muogopeni mungu.
 
Kama serikali ingeonyesha nia ya dhati katika kuzuia hili tatizo basi naamini na sisi wananchi tunge toa mchango mkubwa kabisa ili kuzuia ukahaba.
 
Madanguro ya wasichana wadogo wengine hata miaka tisa wamewekwa na wanawake kwa wanaume ili kuuzwa sasa hivi ni makabila yote hata rangi zisizopenyeka kama wasomali wahindi waarabu wanaidadi kubwa tu ya watoto pia wananyanyaswa na kufanyiwa ukatili wa kutisha kwa kulazimishwa kufanya ngono na wanaume hata zaidi ya 12 kwa siku
 
Msichana wa miaka 13 afanyishwa ukahabalakini usiku husambazwa kwenye majumba ya starehe kwa ajili ya kuuza miili yao, chini ya ulinzi wa mabaunsa.


Sunday, January 08, 2012 11:52 PM

Hivi majumba ya Starehe Mbeya ni yapi?
 
Niliwa kuweka thread hapa majuzi! Watoto wengi wanarubuniwa kwa ahadi kedekede ikiwemo kupata kazi,shule n.k na huishia kuuzwa. Hali inatisha!
 
Kiukweli inasikitisha lakini ukweli kuliko huo ni kwamba biasha ya KuUZA MWILI tena inayohusisha watoto wadogo limekua suhala LISILO ShtUSHA tena..(kawaida sana)..

Kwanin limekuwa la kawaida,tena kawaida sana..?
Ni JAMII inayoshindwa KUWAJIBIKA.. tena kila mwanajamii kwa nafasi yake...!!

SERIKAL : inawajibika vipi kulinda watoto wetu, na kama haitoshi serikali inatoa ufafanuzi gani juu ya neno Utu..??
Sheria nazo zinasemaje na vip utekelezaji wa sheria hzo..

WAZAZI : kama mzazi unamtoto mwenye umri chini ya miaka 18..
Lakini haujui anaishi vip..,anakula nini..,na nin hali yake kiafya..
Nin wajibu wa mzazi katika hili..

WafanyaBIASHARA : mim sisemi kitu juu ya hawa watu..
Wajibu wao mkubwa ni kutafuta faida bana na wanaitengeneza kwelikweli..
Ila biashara hii kweli ni halali..?!

WATEJA : hawa ndiyo watu ambao nalia nao usiku na mchana kila nikisikia biashara hii ya ngono inayohusisha watoto..
Hakika kushamiri na kukua kwa hii biashara ni NyiNYi...
Kwani ukisema mim sinunui mtoto na mwengine akasema hvyo,hvyo..
Biashara hii imekufa..

WADAU : hapa nawazungumzia wenye KuMbI za STAREHE na MaGESt na machaka kama hayo..
Kwanini uangalie pesa na kuuzika UTu jamani..

WanaJAMII : una HAKI ya KUHOJi na KuTILia shaka kila kitu unachoona hakiko sawasawa katika jamii usika..
Kuogopa kuitwa mnoko au kimbelembele haita saidia jamii bali kuiharibu..

Na kila mmoja wetu ajiulize..
Hana mausiano na mtu yeyeto mwenye umri wa chini ya miaka 18...?!
Haujachelewa bana..
Amua leo..
2walinde watoto bana licha ya mwonekano wao wa KUVutIA na wepesi wa kushawishi...!
2geuke leo..
SOUTH AFRIca tu hapa,hautaingia 9t club ikiwa utatiliwa mashaka juu ya umri wako othwise umeonyesha ID..
Kwetu ikoje..
NAUMIA..!!
 
Msichana wa miaka 13 afanyishwa ukahaba
6180206.jpg

Picha ya mmoja wa anaosadikiwa ni changudoa akiwa mawindoni
Sunday, January 08, 2012 11:52 PM
Habari kutoka Majengo Tanesco, mjini Sumbawanga zimeripoti kuwa msichana ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba alietumikishwa ngono ya lazima kwa miezi saba akitafutiwa wanaume na mwenye danguro kwa malipo ya kupewa wa mlo.
Binti huyo, jina napicha kapuni, ametoboa siri ya kutisha kuhusu biashara ya ngono inayoendelea bongo. Binti huyo amedai kuwa alirubuniwa kuondoka nyumbani kwao kisha kujikuta akitumikishwa kwenye biashara ya ngon jijini Mbeya.
Binti huyo alisema kwamba hakuwa peke yake, bali zaidi ya wasichana wadogo 30 ambao waliofungiwa nyumbani kwa tajiri wakilindwa na walinzi wenye silaha usiku na mchana, lakini usiku husambazwa kwenye majumba ya starehe kwa ajili ya kuuza miili yao, chini ya ulinzi wa mabaunsa.



Hii mbaya sana; Haitakuwa ajabu muuzaji akawauza hata wanawe
 
Hii biashara nilidhani ipo kwenye miji mikubwa tu kama Dar, Mwanza, Mbeya na Arusha kumbe mpaka Sumbawanga? Sasa utaona kadri maisha yanavyozidi kubana ndivyo biashara ya ngono inavyoendelea kushamiri kwa sababu mtaji unao mweeenyewe:eyebrows:
 
hii source naifahamu usihangaike kuisoma. Ni bora magazeti ya shigongo kuliko nipehabari
 
YAANI NI HATARI TUPU; BINTI MWENYEWE KASEMA WALIKUWA ZAIDI YA 30 WENYE UMRI USIOZIDI MIAKA 20. NA MWEZI WA 11 MWAKA JANA, 10 KATI YAO WALIFUZU MAFUNZO NA KUPELEKWA URUSI KWENDA KUFANYA UKAHABA. JUMBA LENYEWE LINALINDWA USIKU NA MCHANA. PIA WANAFANYISHWA MAZOEZI KILA SIKU SAA ILI WAWE FITI KWA SHUGHULI.
SWALI LANGU; HIVI POLISI WETU HAWAKO KWELI KWENYE NETWORK YA WATU HATARI KAMA HAWA WANAOWARUBUNI WATOTO AMBAO HATA UELEWA WAO UNA SHIDA ILI KUWAFANYISHA SHUGHULI HII HARAMU?
Je, kama Wazungu waliweza kumfanyia yule binti unyama hapa kwetu Kiteto juzi, je hawa wanaopelekwa nchi za watu bila taarifa; je ni unyama gani wanafaanyiwa hawa watoto? Yaani inaumiza sana ndugu zangu; ebu jaribu kufikiria kwamba huyo aliyerubuniwa ni mdogo wako au mwanao? hakika inaumiza sana.
 
Huyo tajiri achukuliwe hatua za kisheria .. a hukumiwe hata kunyongwa .. do
Fundisho kwa wengine.......
 
Duuu kwa hali hii ile mvua ni bora ingeendelea kunyesha mwezi mzima mfululizo.
 
Madanguro ya wasichana wadogo wengine hata miaka tisa wamewekwa na wanawake kwa wanaume ili kuuzwa sasa hivi ni makabila yote hata rangi zisizopenyeka kama wasomali wahindi waarabu wanaidadi kubwa tu ya watoto pia wananyanyaswa na kufanyiwa ukatili wa kutisha kwa kulazimishwa kufanya ngono na wanaume hata zaidi ya 12 kwa siku

yanapatikana wapi hayo madanguro mkuu? nataka nikajionee mwenyewe..
 
Wazee wenye watoto wa umri huo, wako wapi kutafuta watoto wao wafikisha habari kwenye vyote vya usalama kama watoto went missing.
 
Back
Top Bottom