wanajamii, naomba kuuliza wapi anaweza kupatikana msichana wa kazi za ndani (housegirl/housemaid). mfanyakazi aliyepo anakaribia kumaliza mkataba wake na ameamua kutoendelea na mkataba kwa sababu anataka kuanza maisha mengine. amekaa miaka takribani minne na sababu ya kutoendelea na mkataba ni genuine kabisa
maelezo mafupi kuhusu mwajiri:
maelezo mafupi kuhusu mwajiri:
- mwajiri anaishi Dar maeneo ya Boko,
- Nyumba ni ya mke na mume- wote wanafanya kazi
- kuna watoto wawili- mmoja miaka 6 na mwingine miaka 4 - watoto wanaenda shule asubuhi saa moja na nusu na kurudi nyumbani saa 9 na nusu alasiri; Mke anatarajiwa kujifungua mtoto mwingine baadae mwaka huu au mapema mwakani (Mungu amjalie)
- nyumba ni floor moja (siyo ya ghorofa);
- kuna houseboy anayefanya kazi za kusafisha mazingira ya nje na garden ndogo iliyopo. hakai kwa mwajiri - anakuja na kuondoka
- kusafisha nyumba ikiwemo kudeki na kusafisha madirisha
- kufua nguo hasa za watoto (houseboy anasaidia kazi hii marambili kwa wiki)
- kupiga pasi hasa za watoto (houseboy anasaidia kazi hii mara moja kwa wiki)
- kupika chakula
- Kulea watoto ikiwa ni kuhakikisha wanakula, wanaoga na kulala vizuri
- Mungu akijali mke akajifungua baadae mwaka huu au mapema mwakani, atahusika kulea mtoto mdogo ikiwa ni pamoja na kumlisha na kuhakikisha anakuwa katika hali ya usafi na huduma nyingine anazotakiwa kupewa mtoto
- kuhakikisha usalama wa nyumba (ikiwa na maana ahakikishe hatoki nyumbani bila sababu ya msingi wakati baba na mama wapo kazini (nyumba ina security wire)
- kuwakumbusha watoto kufanya homework pale wazazi wanapokuwa hawajarudi kutoka kazini
- awe mchapa kazi
- msichana mwenye umri unaomruhusu kufanya kazi kisheria
- awe mwaminifu na asiwe mwizi
- Awe muwazi na kumueleza mwajiri masuala yote muhimu mazuri na mabaya (ili hatua muafaka ichukuliwe)
- ajiheshimu na asiwe malaya
- Awe na mdhamini mmoja mwenye makazi na anuani inayoeleweka
- awe na upendo kwa watoto (watoto nao wamefundishwa kumpenda dada anayewalea)
- Mshahara wa mwezi ni Tsh 50,000 kianzio
- Atapata bonus ya miezi miwili (100,000) kwa kila mwaka anaokaa na itatolewa mwisho wa mwaka - asipotimiza mwaka hatapewa
- Atapata matiibabu bure
- Atapata chakula bure
- Atapata malazi (accomodation) ya bure (ataishi nyumbani kwa mwajiri)- atapewa chumba kilicho na kitanda
- Atakuwa anapewa bure vitu vyote vitakavyomwezesha kuwa katika hali ya usafi mfano sabuni, mafuta ya kupakaa, mswaki, nguo, n.k.
- Likizo ambapo atapewa nauli ya basi ya kwenda na kurudi nyumbani kwao. wakati wa kwenda likizo atapewa zawadi za kupeleka nyumbani kwa wazazi wake
- Akikaa muda usiopungua miaka 4 atapewa bonus ya kusomeshwa ufundi wowote atakaotaka ili umumsaidie huko mbeleni baada ya kumaliza mkataba