Update:
Hali ya soko imerudi kama kawaida yake, yale mayai yaliyokuwa yanauzwa kwa mafungu (4000 - 4500) kwa tray yemeisha. Tray kwa sasa ni 6500 hadi 7,000 kwa bei ya Jumla.
Serikali msiruhusu tena wahuni wahuni kuingiza mizigo ya vyakula kwa njia za panya!! lindeni wazalishaji wazawa wa ndani - maana mmeshatuambia kuwekeza kwenye GESI HATUWEZI - sasa huku kwenye mifugo nako mnataka kutukimbiza, swali je tuende wapi?
Hili si la kubeza, ni suala muhimu kabisa - LAZIMA KUWAJALI WAKULIMA NA WAFUGAJI WA NDANI.
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Wakuu nawapa pole sana wafugaji wa kuku wa mayai, mji mzima mayai yamefurika, hayana soko na wafugaji wanahaha huko na huko kutafuta soko la kuyauza. Katika upelelezi wangu kuna habari ambazo hazijathibitika kwamba mayai yanatoka mombasa kwa volume ya ajabu kabisa, mayai haya ndiyo yanakuja kuua soko la ndani na kutangaza msiba kwa wajasiriamali wadogo wadogo ambao wengi ni wamama wajane na vijana walitoka vyuo ambao wanajaribu kujiajiri wenyewe.
Ninachojiuliza:
Je Wizara ya kilimo na ufugaji inalijua hili? na inachukua hatua gani kuwalinda wazalishaji wadogo wadogo wa ndani?
Je hawa wafanyabiashra wanaoingiza mayai nchi wanalipa kodo sitahiki?
na je gharama zao za uzalishaji ni gharama zipi huko mombasa maana tray moja wanauza mpaka shs 4500 hadi 5000 bei ambayo kwa mfugaji wa nchini haimlipi. Mfugaji wa ndani anatakiwa auze tray si chini ya sh 6500 ili aweze kusonga mbele.
Mwisho kama hizi habari ni za kweli basi wajasiriamali wadogo wadogo huu ni msiba kwenu, kama hamtaungana na kulepeka malalamiko yenu wizarani basi mmekwisha. nawashauri mfungue chama chenu kiwatetee.
Hebu tujadili hili kwa kina maana tusipokuwa makini hwa wakenya watatuua njaa kwani wao wana mitaji mikubwa sana hasa kwenye suala zima la ufugaji na wanaweza ku-supply Maziwa, Mayai, Nyama za kusindika, Ngozi kwa volume ya ajabu.
Tuamke watanzania hasa wafugaji hali ni mbaya.
Hali ya soko imerudi kama kawaida yake, yale mayai yaliyokuwa yanauzwa kwa mafungu (4000 - 4500) kwa tray yemeisha. Tray kwa sasa ni 6500 hadi 7,000 kwa bei ya Jumla.
Serikali msiruhusu tena wahuni wahuni kuingiza mizigo ya vyakula kwa njia za panya!! lindeni wazalishaji wazawa wa ndani - maana mmeshatuambia kuwekeza kwenye GESI HATUWEZI - sasa huku kwenye mifugo nako mnataka kutukimbiza, swali je tuende wapi?
Hili si la kubeza, ni suala muhimu kabisa - LAZIMA KUWAJALI WAKULIMA NA WAFUGAJI WA NDANI.
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Wakuu nawapa pole sana wafugaji wa kuku wa mayai, mji mzima mayai yamefurika, hayana soko na wafugaji wanahaha huko na huko kutafuta soko la kuyauza. Katika upelelezi wangu kuna habari ambazo hazijathibitika kwamba mayai yanatoka mombasa kwa volume ya ajabu kabisa, mayai haya ndiyo yanakuja kuua soko la ndani na kutangaza msiba kwa wajasiriamali wadogo wadogo ambao wengi ni wamama wajane na vijana walitoka vyuo ambao wanajaribu kujiajiri wenyewe.
Ninachojiuliza:
Je Wizara ya kilimo na ufugaji inalijua hili? na inachukua hatua gani kuwalinda wazalishaji wadogo wadogo wa ndani?
Je hawa wafanyabiashra wanaoingiza mayai nchi wanalipa kodo sitahiki?
na je gharama zao za uzalishaji ni gharama zipi huko mombasa maana tray moja wanauza mpaka shs 4500 hadi 5000 bei ambayo kwa mfugaji wa nchini haimlipi. Mfugaji wa ndani anatakiwa auze tray si chini ya sh 6500 ili aweze kusonga mbele.
Mwisho kama hizi habari ni za kweli basi wajasiriamali wadogo wadogo huu ni msiba kwenu, kama hamtaungana na kulepeka malalamiko yenu wizarani basi mmekwisha. nawashauri mfungue chama chenu kiwatetee.
Hebu tujadili hili kwa kina maana tusipokuwa makini hwa wakenya watatuua njaa kwani wao wana mitaji mikubwa sana hasa kwenye suala zima la ufugaji na wanaweza ku-supply Maziwa, Mayai, Nyama za kusindika, Ngozi kwa volume ya ajabu.
Tuamke watanzania hasa wafugaji hali ni mbaya.