hii picha imenikumbusha mbali sana,zamani nilipokuwa mdogo sana mitaa ya mbeya,kuna jamaa alikuwa kampakia demu wake kwenye pikipiki aisee nakubali alikua mzuri hasa shepu ya kibantu,sasa jamaa alikuwa anateremka mteremko mkali na kulikua na kona kali sana na jamaa alikua spidi kali pia,sijui ikawaje yule mdada akatereza kutoka kwenye pikipiki na kudondoka,bahati mbaya gauni alilovaa likanasa kwenye taa ya indiketa ya pikipiki aisee,jamaa hana habari.alimburuza yule dada umbali mrefu kweli kwenye lami,mpaka anasimama loh yule dada kichwa kilikuwa hakitamaniki,ubongo wote nje,yaani sikulala siku hiyo kwa kuota.sijui kama yule dada alipona.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.