Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,438
- 113,445
Wanabodi,
Nimepata nafasi kuhudhuria msiba hapa nyumbani kwa Jeremia Sumari.
Kama ilivyo kwa Regia, hapa kwa Sumari ni vivyo hivyo, viongozi wa vyama vya upinzani wameungana na viongozi wa CCM na waombolezaji wengine kuwafariji wafiwa.
Jioni hii, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akiongozana na Naibu Katibu Zitto Kabwe wameungana na Mwenyekiti wa UDP Mzew John Cheyo wapo kwa pamoja na mawaziri kadhaa wa serikali ya JK wakiongozwa na Mawaziri Wakuu Wastaafu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa!. na Fredrick Tuluway Sumaye!
Jana rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Wilbrod Slaa wakifika nyumbani hapa kuwafariji wafiwa!.
Mawaziri Wasira, Nchimbi, wabunge wakiongozwa na Katibu wa Bunge Dr Kashilila etc pia wapo!
Ni jambo jema na la kupendeza uonapo ndugu wakikaa pamoja kwa upendo wakati wa shida na raha. Huu ni uthibitisho kuwa licha ya tofauti za kiitikadi, Watanzania tu wamoja kwa upendo na mshikamano miongoni mwetu!.
"Mahali ni Pazuri..Ndugu Wanapokaa...
My Take:
Wanabodi hivi kama ushirikiano, upendo, amani na mshikamano unaofanyika misibani kama ungepelekwa mpaka Bungeni Dodoma, Jee Tanzania tungekuwa wapi?.
Rip Jerry Solomon Sumari!.Thanks kwa Upendo, Amani, Ushirikiano na Mshikamano!
Pasco.
Update:
Ratiba imetolewa.
1. Misa kesho saa 2:00 Msasani Lutheran
2. Saa 5 Mwili kupelekwa Karimjee
kuagwa kitaifa.
3. Mwili kurudi kulala nyumbani.
4. Jumapili asubuhi kusafirishwa kwa ndege kwenda Arusha.
5. Maziko Jumatatu.
Nimepata nafasi kuhudhuria msiba hapa nyumbani kwa Jeremia Sumari.
Kama ilivyo kwa Regia, hapa kwa Sumari ni vivyo hivyo, viongozi wa vyama vya upinzani wameungana na viongozi wa CCM na waombolezaji wengine kuwafariji wafiwa.
Jioni hii, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akiongozana na Naibu Katibu Zitto Kabwe wameungana na Mwenyekiti wa UDP Mzew John Cheyo wapo kwa pamoja na mawaziri kadhaa wa serikali ya JK wakiongozwa na Mawaziri Wakuu Wastaafu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa!. na Fredrick Tuluway Sumaye!
Jana rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Wilbrod Slaa wakifika nyumbani hapa kuwafariji wafiwa!.
Mawaziri Wasira, Nchimbi, wabunge wakiongozwa na Katibu wa Bunge Dr Kashilila etc pia wapo!
Ni jambo jema na la kupendeza uonapo ndugu wakikaa pamoja kwa upendo wakati wa shida na raha. Huu ni uthibitisho kuwa licha ya tofauti za kiitikadi, Watanzania tu wamoja kwa upendo na mshikamano miongoni mwetu!.
"Mahali ni Pazuri..Ndugu Wanapokaa...
My Take:
Wanabodi hivi kama ushirikiano, upendo, amani na mshikamano unaofanyika misibani kama ungepelekwa mpaka Bungeni Dodoma, Jee Tanzania tungekuwa wapi?.
Rip Jerry Solomon Sumari!.Thanks kwa Upendo, Amani, Ushirikiano na Mshikamano!
Pasco.
Update:
Ratiba imetolewa.
1. Misa kesho saa 2:00 Msasani Lutheran
2. Saa 5 Mwili kupelekwa Karimjee
kuagwa kitaifa.
3. Mwili kurudi kulala nyumbani.
4. Jumapili asubuhi kusafirishwa kwa ndege kwenda Arusha.
5. Maziko Jumatatu.