Kutokana na kuchukiwa kila upande na Watanzania na kuihofia CHADEMA serikali na CCM wameamua kuipakia JF kuwa ni mali ya CHADEMA bila kutoa ushahidi(refer Nipashe ya April 12). Yaani wao kila awapingaye sasa hivi ni CHADEMA wakati si kweli. Binafsi ningependa kulaani kauli hii yenye nia ya kuibana JF. WATU WOTE WAKO HURU KUJIUNGA HUMU bila kujali itikadi zao. Labda kwa vile watendaji wa CHADEMA kama Dr Slaa,Zitto,John Mnyika na Regia Mtema wao wameamua kutumia ID zao za kweli ndio maana wao wanahukumu hivyo. Tunajua kuwa vigogo wengi wa serikali na CCM ni members humu.
We say JF SHALL NEVER DIE
Mlio wengi humu ni chadema..... Sisi tuko wachache hiyo ni fact na siyo dhambi kwenu ila ni dosari kwetu
Huu ni UJINGA wa hali ya juu. Yaani mie kuwa JF tayari nimekuwa MALI ya Chadema?
Mtu mwenyewe hata Kadi ya chama chochote sina na leo unaambiwa "umemilikiwa na Chadema."
JF ni watu na wala siyo Maxence Melo au sijui nani. Wale ni wadhamini wetu tu.
Ukitaka kuamini hilo, jiulize kitu kimoja: Kuna forum nyingi sana za Watanzania na Blog kibao ila kwa nini JF ndiyo inatesa namna hiyo? Ni kwa makala za wadhamini wa JF au MEMBERS wa JF?
Michuzi Blog ingeliweza kuwa kwenye nafasi ya JF leo hii ila kutokana na Michuzi kubania thread za watu na comments za watu, Michuzi blog imebakia kuwa kama kitawi cha CCM na Bwawa la Maini. Blog nyingine ya wauza nywele nayo iko juu na sababu ni kuwa wanafanya vizuri sana katika Issue ambazo wameamua wazifanye. Hata Ze-Utamu na yeye alifanikiwa saaana kwa sababu HAKUBANIA habari za watu.
JF imekuwa wazi kwa watu na kuachia habari ziandikwe na kuachwa hata kama ni SIRI NZITO ya Serikali. Zimeondoloewa tu zile ambazo au zinatukana au zina majungu. Kuachia habari huku zisomwe na watu wote wanaoingia JF ndiyo kumeifanya JF iwe hapo ilipo na kuwapa SIFA za UJASIRI wadhamini wa JF.
Ila leo mtu akija na kusema JF ni mali ya Chadema ni sawa na kusifia Jiko fulani linapika vizuri na LIMEDHAMINIWA na fulani na unasahau kuwa WAPISHI wake wakihama, jiko litabako historia. Wanataka kusema mtu kama FMes ni Chadema? Kibunango ni Chadema? Malaria Sugu, Mwiba, Junus, Kishonga, Ndalu, Tumaini, Ngongo, X-Pasters na wengine wengi wanaoshinda hapa wakimtukana Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla na wao wamekuwa ni Chadema?
Hebu mwangalia Waberoya na makala zake, unataka kusema huyo ni Chadema?
Kweli MFA MAJI, HAACHI KUTAPATAPA.......... Atashika hata kitoto cha Ndege/bata ili asizame.
naona hawa "consultants" ni wasomaji haswa wa michango ya humu jf, lakini kinachonikera ni kufikiri hii ni forum ya chadema!!!!!
Mimi sijifichi ni mwana ccm lakini nakerwa sana na ufisadi na mafisadi.
Ccm imelilea hili tatizo kwa makusudi, sasa viongozi wetu walitegemea nini haswa?-kupongezwa kwa kula na kunywa na mafisadi? Na je wao kweli hawkuliona hili tatizo hadi waambiwe na the so-called "consultants".
Hapa ndipo panaponisikitisha maana nakitakia mema chama changu, na je vikao vingi vinavyo endesha chama vimeshindwa kuona makosa yanayotendeka?
I fear for ccm.
Uzuri wa jf ni kutoa maoni huru ili kujenga na kusahihisha makosa, kwa ripoti ya "consultants" inaelekea ujumbe umefika panapostahili na hatua zimechukuliwa-this is a positive move.
Kwa mantiki ya kufikiri kuwa jf ni ya chadema ccm itafanya kosa la kuanzisha forum yake ambayo itakosa mvuto kama itakuwa kazi yake ni kusifia viongozi na kuwapamba-kama afanyavyo issa michuzi na blogspot yake. Fuatilia kwa makini issa michuzi blogspot na utaona idadi ya watu wanaotembelea pale imekuwa ikipungua kadri sifa za viongozi (hata wale mafisadi) zinavyozidi kupambwa.
CCM wafanye mpango wanunue hii site kama wanaona ina manufaa kwao, kuanzisha mpya itachukua muda kuzoeleka
Niliwai kuona kada wa CCM aitwaye Sabodo akichangia CDM fedha, CCM wameshindwa nini kulijadili hili lilifanyika adharani!?
Kwani kuna tangazo lao humu?Mimi nimejiunga JF kutokana na uwazi na uhuru wa kutoa maoni yangu pamoja na kupata habari zilizo huru, najua kuna wengine waliojiunga kutokana na matamanio ya aina hii. Lakini kitu kizuri cha kuwashukuru CCM ni kuwa wanaiongezea JF umaarufu.
Wakiwanyima matangazo tutalipia kuiendesha!
Mimi nimejiunga JF kutokana na uwazi na uhuru wa kutoa maoni yangu pamoja na kupata habari zilizo huru, najua kuna wengine waliojiunga kutokana na matamanio ya aina hii. Lakini kitu kizuri cha kuwashukuru CCM ni kuwa wanaiongezea JF umaarufu.
Wakiwanyima matangazo tutalipia kuiendesha!