Mshahara wa TShs 900,000 hautoshi kabisa

AZA KAMA MIMI VILE...
Ni kweli bora siasa kwani inalipa..LAKINI TUSISAHAU MAISHA YA WATANZANIA WENZETU
 
Wenye kujua naomba mnifahamishe,mshahara wa Dr wa kuanzia ni 900,000(gross or net?). Je wa specialist Dr ni bei gani?
Maanake hapa watu wanaongea as if hii 900,000 ndio highest Dr anapata.
 
I DONT KNOW HOW MUCH ARE THEY BEING PAID, BUT:

10,000,000-900,000=9,100,000/=

1 mp=10dr,s

10=regions=1 dr each (mwanza,kilimanjaro,lindi, mtwara,kigoma,singida,tabora,shinyanga,mbeya,rukwa) how many lives could be saved in these regions?

Can 1 mp stands for all these regions?....huh!!!
 
Hongera sana mkuu huo ndio wito tunaohitaji kuridhika na mshahara unaopewa, kuna Dr mmoja nilipeleka mgonjwa wangu akaniomba rushwa nikasema sina hela akaniambia sasa mbona umeniletea maiti? Na kweli nilikaa masaa 2 bila mgonjwa kuhudumiwa mpaka anafariki. Hawa madr wa mishahara bora wafukuzwe tu maana hawana msaada kwa wananchi wa kawaida, wakatafute kazi nje ya nchi kwetu hawatufai kabisa maana kama huna kitu kidogo ndio unazikwa hata kwa ugonjwa mdogo.
Kinachotafutwa hapa ni madaktari kufanya kazi kwa moyo na sio utajiri, unajua huyo dokta angekuwa ameridhika angemtbu mgonjwa wako kwa moyo na labda angepona lakini kutokana na hali aliyo nayo akaopt kukuomba rushwa. Mimi siungi mkono mgomo lakini pia sikubaliani na serikali kutowaongezea angalau wapate moyo wa kufanya kazi. Cha muhimu mgomo ungeisha hata kwa kukubaliana na sio kulazimishana kwamba asiyetaka kazi na aache. HAPA WATAKAOUMIA NI WATU WA CHINI TU NA SIO RAIS KIKWETE, tunapaswa kujifunza kuilazimisha serikali itupatie huduma bora katika maeneo mbalimbali
 
Even if it is net, haitoshi. Maisha ya watu wangapi yanaokolewa kwa hiyo laki 9? Maisha ya watu ni gross au net?

Ok let say you live ::::net life
i live ::::gross life..................can this make sense?
 
Mshahara wa kuanzia dr mwenye first degree ni 957,700/= na sio 900,000/=. Na mwaka huu upatanda kuanzia kati ya 15% - 20%
 
Katufu umekomaa, kwa hili unaweza kumshauri mtu. Si kwamba tukikosoa ndio tuko upande wa madaktari...hapana. Ila na serikali isihiriki mauaji kwa kuwanyima raia zake haki yao ya msingi. Ikisuluhisha na madaktari ni vifo vingi vinavyookolewa hapa. Sihitaji kutoa takwimu kimkoa au kikanda kuwa ni watu wangapi hufariki kutokana na migomo ya aina hii....kwani itaongeza machungu na kuchochea uhasama dhidi ya pande husika.
 
Leo katika hotuba ya Rais,alikua akitamka kwa sifa kua serikali inawalipa madaktari hela nyingi Tshs 900,000.Ila Laki tisa,ukikata PPF,PAYE inabaki kama TShs 550,000.Ukiangalia Dr anasoma miaka 5,anafanya kazi za riak kubwa sanaMbunge au waziri anapewa maslahi mazito sana,wengi hata ulinzi baada ya kustafu wanapewa.We unampa Dr mshahara net laki tano na nusu unategemea awe na umakini kwkazini.


Kimsingi ulichoandika huna uhakika nacho, mimi mshahara wangu ni 810,000 ,baada ya makato yote nabaki na 630,000.hivyo mwenye kupata laki tisa hawezi kubaki na 550,000. Lakini katika hili la mishahara siwaungi mkono madokta kwani alichosema rais alikuwa sawasawa kabisa.Mchumi, afisa Utumishi, Mwalimu, mhasibu wote wanaoanza kazi wanalipwa laki nne na point.dokta anayeanza laki 9 na point, halafu anadai aongezewe kutokana na kazi yake kuwa ngumu. Kiukweli nakubali kazi yao ni ngumu lkn si wao pekee wenye kazi ngumu,mbona hatuwasemi maaskari wanaolala nje wakilinda benki bila malipo,mbona hatuwasemi walimu wanaoishi kwa kula vumbi la chaki bila kunywa maziwa?

Katika hili la mishahara JK yuko sahihi,waache kazi na watakuja wengine.siwaungi mkono kabisaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Mshahara wa kuanzia dr mwenye first degree ni 957,700/= na sio 900,000/=. Na mwaka huu upatanda kuanzia kati ya 15% - 20%
eLFU 57,700/= ANAKATWA KULIPIA MKOPO ALIOKOPESHWA NA SERIKALI
 
HAPO NI Mil 1.050.000/= sasa mimi nikisema 900,000/=haitoshi hawanielewi kabisa...jameni hiyo haitoshi kabisa.....
Mbona unataka kuminyana na muajiri wako? Tatizo lipo wapi wewe tafuta sehemu wanaolipa mshahara mzuri kafanye kazi uko usiladhimishe ulipwe unavyotaka mkuu serikali aina huo uwezo...au nenda TMJ, Agha Khan, Regency, Hindu, kachukuwe mamilioni.
 
Dah hapo nipite tu mimi, maana ugomvi wa Panzi Furaha ya kunguru, Maana kada za Uhasibu hazitajwi sijui sisi ndo hatufanyi kazi katika mazingira hatarishi! Maana kitendo cha kukaa na Mamilioni ya Watu kila siku ni zaidi ya Mazingira hatarishi, Maana ukiziiba tu Unanye.a Kopo, Sijui na sisi tudai Allowance ipo? Maana iyo Tsh. 446,000/= tunayolipwa na ukikata kodi kinabaki kituko! Na hapo unataka mwanao asome International School.
duh!.......mishahara yenyewe ndo hio,kunakutoka kweli hapo?
 
Leo katika hotuba ya Rais,alikua akitamka kwa sifa kua serikali inawalipa madaktari hela nyingi Tshs 900,000.Ila Laki tisa,ukikata PPF,PAYE inabaki kama TShs 550,000.Ukiangalia Dr anasoma miaka 5,anafanya kazi za riak kubwa sanaMbunge au waziri anapewa maslahi mazito sana,wengi hata ulinzi baada ya kustafu wanapewa.We unampa Dr mshahara net laki tano na nusu unategemea awe na umakini kwkazini.

Matatizo hapa sio kwamba 900000 hazitoshi kwa kazi ya madaktari. Tatizo ni pale messenger wa BOT, TRA, etc analipwa zaidi ya hizo. Wao serikali inazipata wapi? tatizo ni pale a lazy Procurement officer (Store keeper) wanapompa TShs 300000 (officially) halafu anamiliki mali za mamilioni bila kuonekana kuwa ni tatizo. Tatizo ni pale Regional traffic Officer anapojenga kitegauchumi worth billions bila mtu kumuwajibisha wakati rushwa kwa hawa trafic inadaiwa na kutolewa waziwazi!

Kimsingi, madai ya madaktari yanawakilisha dukuduku kubwa la matatizo ya mfumo usiowajibika na wa kulindana katika kufuja rasilmali za taifa na matumizi mabaya ya pesa za mlipakodi. Hii inafanyika waziwazi na hakuna dalili yoyote mbeleni inayoonyesha kuna nia ya dhati ya kuondoa madhila haya. Kinachoudhi, ni maneno yanayotumika kuelezea kinachofanyika kupambana na haya maovu.


  1. Kusingizia utatuaji wa matatizo kufuata utawala bora ambao wote tunajua haupo kwani waliopewa dhamana ya huo utawala ndio wakosaji
  2. Kusingizia kufuata utawala wa sheria wakati kila mtu anajua mahakama zetu sio huru na ni sehemu ya huo uozo
  3. Kutumia vibaya vyombo vya dola kukandamiza haki za raia.

Kwa hiyo kila Mtanzania anadai chake kwa kuwa inaonekana huo uwezo wa kulipa una matabaka. Wako wanaojiona wana haki zaidi ya kufaidi keki ya taifa zidi ya wengine. Hii itakapoondoka na/au kuonekana kuwa inashughulikiwa kwa dhati, wengine watavuta subira kwani muda utakuwa mfupi na kila mtu atapata kinachowezekana kwa haki ya taaluma yake.

Hotuba ya Mh. Rais ingeambatana na kuueleza uma serikali inafanya nini kuongeza uwezo wao kuwalipa wataalamu wake, hasa hasa, kwenye kubana matumizi makubwa ya serikali, kuwabana wabadhirifu na kuwachukulia hatua kali (pamoja na kurudisha walichoiba). Haya yanaweza kuongeza uwezo wa serikali kulipa wataalamu wake bila hata kuongeza uzalishaji! Juhudi za kuongeza tija katika uzalishaji ndizo zitaonyesha uhalisia wa kukua kwa hali ya Taifa kiuchumi.

Kwa maoni yangu, walichoanzisha Madaktari ni mwanzo wa kuanguka serikali kama haitakuwa makini. Walimu wana madai hayo hayo; manesi nao hivyo hivyo, Polisi (wasiokuwa makachero au trafiki) wanasota sana na ndio sababu wasipowasilisha mgawo kwa wakubwa wanatishiwa kupelekwa kikosi cha FFU, mbwa au farasi. Nchi italipuka wote wakigoma. Naona Serikali imecheza kamari kwa kutegemea kudra za mwenyezi Mungu na Walimu wasigome kwa mtindo wa madaktari. Vyovyote vile iwavyo, siku chache za mbaleni zitakuwa na changamoto nyingi kwa watawala. Nawaomba wasitumie nguvu ya dola bali busara.
 
MWEEN Kwa hiyo Ma Dr wakitimiziwa shida yao nchi itakalika?
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo Ma Dr wakitimiziwa shida yao nchi itakalika?

Sina maana kuwa wao wapewe wanachodai. Nina maanisha kuwa huu ungekuwa wakati muafaka wa kuwaeleza na kuwashawishi WaTZ kwa ujumla kuwa matatizo ya mfumo yanashughulikiwa kwa dhati. Kuonyesha kwa vitendo maovu yanavyoshughulikiwa, waovu wanavyowajibishwa, upatikanaji wa haki unavyohangaikiwa.

Ubovu wa huduma za afya hauanzi kwa siki moja wala kutatuliwa kwa siku moja; Elimu bora haitajengwa kwa siku moja wala haikuanguka kwa siku moja. Kinachotakiwa kwa sasa ni kuonyesha kwa vitendo, nia ya dhati ya kushughulikia haya, na hii ni kwa ajili ya kutumaini kwamba Wa-TZ watawaelewa na kuvuta subira. Kadri wanavyochelewa kuyashughulikia kwa dhat ndivyo watu wanavyopoteza matumaini. Itakapofika hapo ndipo JANGA litakapokuja.
 
Sina maana kuwa wao wapewe wanachodai. Nina maanisha kuwa huu ungekuwa wakati muafaka wa kuwaeleza na kuwashawishi WaTZ kwa ujumla kuwa matatizo ya mfumo yanashughulikiwa kwa dhati. Kuonyesha kwa vitendo maovu yanavyoshughulikiwa, waovu wanavyowajibishwa, upatikanaji wa haki unavyohangaikiwa.

Ubovu wa huduma za afya hauanzi kwa siki moja wala kutatuliwa kwa siku moja; Elimu bora haitajengwa kwa siku moja wala haikuanguka kwa siku moja. Kinachotakiwa kwa sasa ni kuonyesha kwa vitendo, nia ya dhati ya kushughulikia haya, na hii ni kwa ajili ya kutumaini kwamba Wa-TZ watawaelewa na kuvuta subira. Kadri wanavyochelewa kuyashughulikia kwa dhat ndivyo watu wanavyopoteza matumaini. Itakapofika hapo ndipo JANGA litakapokuja.

Kwa hiyo ndugu yangu maneno ya kwenye hutuba yangewekwa hayo maneno ungeridhika?
 
Kwa hiyo ndugu yangu maneno ya kwenye hutuba yangewekwa hayo maneno ungeridhika?

Sio suala la mimi kuridhika ndugu yangu. Ni suala la kutumaini kuwa wa-TZ wataelewa na kuvuta subira na kujenga matumaini ya serikali yao kushughulikia kero za muda mrefu.
 
eLFU 57,700/= ANAKATWA KULIPIA MKOPO ALIOKOPESHWA NA SERIKALI
Hivi mnaelewa kwamba kuna madaktari wanavuta mpaka 5m na zaidi inategemea una miaka mingapi kazini.Vile vile nyumba au posho za nyumba wanapewa.Na rushwa hawaachi na wagonjwa hawawajali very sad....................,Daktari bingwa kama ndiyo kwanza ameajiriwa analipwa 1.5m! Kuna AMO wanalipwa zaidi ya hizo kutokana na miaka mingi kazini tangu wameajiriwa.
 
Kwa analysis yangu ndogo mshahara wa madaktari kama utaongezwa kufikia mil 3.5 kunaweza kutokea political and social instability kwa kuwa kada nyingine nazo zikidai kiasi hicho cha pesa itakuwa balaa kwani mapato ya ndani kwa mfumo uliopo hayawezi kugharamikia hayo yote. Wote tunakubaliana kwamba wabunge wapunguzwe mishahara na marupurupu lakini kitu kimoja kilichowazi duniani ni kuwa wabunge, ministers, diplomats na hata political leaders wengine ndani ya serikali wana political status. Kwa mfano wote tunakubaliana kwamba ni vigumu mbunge kupanga kwa mfano nyumba ambayo huyo doctor wa intern anapanga kwa kuwa status zao ni tofauti.
 
Sio suala la mimi kuridhika ndugu yangu. Ni suala la kutumaini kuwa wa-TZ wataelewa na kuvuta subira na kujenga matumaini ya serikali yao kushughulikia kero za muda mrefu.
Mbona Ma Dr hao hao kabla ya kugoma waliambiwa kua maswala yao yanashughulikiwa na wakagoma? mi hapa siafiki kusema kua maneno yatawafanya watu wavute subira.
 
Back
Top Bottom