MadameX
JF-Expert Member
- Dec 27, 2009
- 7,792
- 3,848
Mahitaji
1/2 kg Mchele uliooshwa na kulowekwa.
1/4 kg Choroko zilizooshwa
1 cup Coconut powder
11/2 tsp Chumvi
Maelekezo
Chemsha choroko mpaka ziive, halafu bandika sufuria yako ya maji ya mchele, acha ichemke. Mimina mchele wako acha kwa muda wa dakika 5-7 kiini kiive. Unamwaga maji, ya huo mchele unabakisha kiasi tu, tia choroko, chumvi na nazi yako ambayo umeikorogo na maji kidogo, geuza geuza ili vichanganyikane vizuri. Funika vizuri ili mvuke usitoke kabisa, punguza moto uwe mdogo sana. Acha iive kwa muda wa dakika 20-25, unaweza kugeuza tena ili ishikane vizuri.
Tayari kwa kuliwa. Mimi kama mimi napenda ikiwa mseto wa nazi basi inaenda na supu. Ikiwa mseto wa bila nazi, ule uliopikwa na mafuta napendelea na mchuzi wa nazi, nyama au samaki.
1/2 kg Mchele uliooshwa na kulowekwa.
1/4 kg Choroko zilizooshwa
1 cup Coconut powder
11/2 tsp Chumvi
Maelekezo
Chemsha choroko mpaka ziive, halafu bandika sufuria yako ya maji ya mchele, acha ichemke. Mimina mchele wako acha kwa muda wa dakika 5-7 kiini kiive. Unamwaga maji, ya huo mchele unabakisha kiasi tu, tia choroko, chumvi na nazi yako ambayo umeikorogo na maji kidogo, geuza geuza ili vichanganyikane vizuri. Funika vizuri ili mvuke usitoke kabisa, punguza moto uwe mdogo sana. Acha iive kwa muda wa dakika 20-25, unaweza kugeuza tena ili ishikane vizuri.
Tayari kwa kuliwa. Mimi kama mimi napenda ikiwa mseto wa nazi basi inaenda na supu. Ikiwa mseto wa bila nazi, ule uliopikwa na mafuta napendelea na mchuzi wa nazi, nyama au samaki.