kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,214
- Asema Kimepata Nguvu Mpya Baada ya Uchaguzi wa 2010
- Akiri CCM kujisahau na Kubweteka baada ya 2005
- Athibitisha Nape Kuomba fedha moja kwa moja kwa Mwenyekiti.
Amesema Chadema wamepata Nguvu hiyo baada ya kushinda viti vingi vya majimbo na kata. CCm walijisahau baada ya ushindi wa 80% mwaka 2005.
Pia Msekwa amethibitisha mara mbili Nape kuomba fedha moja kwa moja kutoka kwa mwenyekiti (JK) na mwenyekiti amekuwa akimpatia. kwa njia moja ama nyingine hili halikueleweka pale makao makuu, lakini pia mwenyekiti huwa ana pesa zake anazotumia kwa ajili ya kukiendesha chama.
Hata hivyo Nape amekanusha kuwahi kuomba pesa kutoka kwa mwenyekiti.
Habari kamili; Soma RAI July 26 - Aug 2.
Maoni yangu;
- Anachokisema msekwa ni kweli na kama TANU ilivyoweza kumtoa mkoloni mweupe, Chadema itamtoa mkoloni mweusi - CCM
- Shutuma za kwamba Nape anatumiwa na mwenyekiti kuidhoofisha kambi fulani zinaweza kuwa za kweli, hii inatokana na ukweli wa yeye kupewa pesa moja kwa moja na mwenyekiti, kitu ambacho si utaratibu wa chama na kimelalamikiwa makao makuu.
- Nape asipende kukanusha kila kitu, sidhani kama mzee msekwa ana sababu yoyote ya kumsingizia nape kupokea Pesa moja kwa moja kutoka kwa JK.