Nimemsikiliza Msekwa akihojiwa na BBC(JUMAMOSI) kwa kweli inatia uchungu sana,Wana jamii ustaarabu wa kiafrika uko vipi????,Labda tunahitaji elimu kiasi gani ili kuwajibika na makosa ya wazi tunayoyatenda.Msekwa anasisitiza Mambo yote ya kifisadi yanayowaandama vigogo kuwa ni tuhuma tu,Hivyo hawawezi kuwasimamisha kazi zao mpaka ibainike kuwa ni kweli waliyatenda je hii ni halali??.Na nyie vigogo mtu unatuhumiwa mpaka aliyetoa hongo anakubali kuwa nilimpa fulani halafu bado mnakataa kwa kudai kuwa ni tuhuma tu.Kama ni tuhuma tu basi kaa pembeni tuhuma ikionekana ni ya uongo basi utarudi na nguvu mpya.Wabunge wanatuhumiwa kwa ufisadi na wao wanasema maamuzi yao yalibarikiwa na ikulu bado ikulu inakaa kimya na wabunge hao wanaenda bungeni na kusimama na kuchangia hoja AJABU GANI HII TZ.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.