Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Salam wadau,
Nilikuwa naangalia kipindi cha medani za siasa na uchumi, cha startv ambapo mgeni mwalikwa alikuwa makamu mwenyekiti wa ccm bara ndg. Pius Msekwa.
Akijibu swali alilokuwa ameulizwa na mtangazaji wa kipindi ndg. Mwolekwa juu ya dhana ya chama kushika hatamu, Msekwa amesema sasa hivi chini ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi chama hakiwezi kuiagiza serikali nini cha kufanya bali hilo ni jukumu la bunge na cabinet. Kwamba chama (ccm) kilikuwa kinatoa maagizo kwa serikali wakati wa mfumo wa chama kimoja.
Hivi karibuni baada ya ccm kutangaza kujivua gamba, katibu mwenezi wa chama hicho amekuwa akisikika mara kadhaa akisema kwamba chama (ccm) kimeiagiza serikali yake kufanya moja, mbili, tatu n.k
wadau mimi naona hizi ni statements mbili toka kwa viongozi wa juu wa chama kimoja lakini zinakinzana.
Naomba mawazo yenu.
Nilikuwa naangalia kipindi cha medani za siasa na uchumi, cha startv ambapo mgeni mwalikwa alikuwa makamu mwenyekiti wa ccm bara ndg. Pius Msekwa.
Akijibu swali alilokuwa ameulizwa na mtangazaji wa kipindi ndg. Mwolekwa juu ya dhana ya chama kushika hatamu, Msekwa amesema sasa hivi chini ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi chama hakiwezi kuiagiza serikali nini cha kufanya bali hilo ni jukumu la bunge na cabinet. Kwamba chama (ccm) kilikuwa kinatoa maagizo kwa serikali wakati wa mfumo wa chama kimoja.
Hivi karibuni baada ya ccm kutangaza kujivua gamba, katibu mwenezi wa chama hicho amekuwa akisikika mara kadhaa akisema kwamba chama (ccm) kimeiagiza serikali yake kufanya moja, mbili, tatu n.k
wadau mimi naona hizi ni statements mbili toka kwa viongozi wa juu wa chama kimoja lakini zinakinzana.
Naomba mawazo yenu.