Msekwa: Chama (CCM) hakitoi maagizo kwa serikali

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Jul 1, 2008
10,564
7,973
Salam wadau,
Nilikuwa naangalia kipindi cha medani za siasa na uchumi, cha startv ambapo mgeni mwalikwa alikuwa makamu mwenyekiti wa ccm bara ndg. Pius Msekwa.

Akijibu swali alilokuwa ameulizwa na mtangazaji wa kipindi ndg. Mwolekwa juu ya dhana ya chama kushika hatamu, Msekwa amesema sasa hivi chini ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi chama hakiwezi kuiagiza serikali nini cha kufanya bali hilo ni jukumu la bunge na cabinet. Kwamba chama (ccm) kilikuwa kinatoa maagizo kwa serikali wakati wa mfumo wa chama kimoja.

Hivi karibuni baada ya ccm kutangaza kujivua gamba, katibu mwenezi wa chama hicho amekuwa akisikika mara kadhaa akisema kwamba chama (ccm) kimeiagiza serikali yake kufanya moja, mbili, tatu n.k
wadau mimi naona hizi ni statements mbili toka kwa viongozi wa juu wa chama kimoja lakini zinakinzana.

Naomba mawazo yenu.
 
Salam wadau,
Nilikuwa naangalia kipindi cha medani za siasa na uchumi, cha startv ambapo mgeni mwalikwa alikuwa makamu mwenyekiti wa ccm bara ndg. Pius Msekwa.

Akijibu swali alilokuwa ameulizwa na mtangazaji wa kipindi ndg. Mwolekwa juu ya dhana ya chama kushika hatamu, Msekwa amesema sasa hivi chini ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi chama hakiwezi kuiagiza serikali nini cha kufanya bali hilo ni jukumu la bunge na cabinet. Kwamba chama (ccm) kilikuwa kinatoa maagizo kwa serikali wakati wa mfumo wa chama kimoja.

Hivi karibuni baada ya ccm kutangaza kujivua gamba, katibu mwenezi wa chama hicho amekuwa akisikika mara kadhaa akisema kwamba chama (ccm) kimeiagiza serikali yake kufanya moja, mbili, tatu n.k
wadau mimi naona hizi ni statements mbili toka kwa viongozi wa juu wa chama kimoja lakini zinakinzana.

Naomba mawazo yenu.

Mzee Msekwa umri unapita inawezekana hata mambo ya kawaida ya msingi anayasahau. Chama ndio kinaiagiza serikali kupitia ilani inayoitangaza wakati wa kamoeni, na kupitia wabunge ambao walikuwa wanaimba kuhusu ilani hiyo.
 
Nadhani hapa kunamkanganyiko maana Nepi naye kwenye mdaharo alikuwa anajigamba kuwa chama ndo kinaelekeza serikali cha kufanya na wakienda nje huwarejesha kwenye mstari.

Kama haya yanayofanywa na serikali ya jk ndiyo maagizo na maelekezo ya chama basi chama cha magamba ndo kinachoipeleka nchi shimoni na kitalaumiwa milele. Siamini kama mwazo ua watu kama Nepi ndo yanayotuongoza sas hivi!
 
Jana kwenye mdahalo Nape alisema kuwa rais ni kama muuza duka na chama ni wenye duka.
Mwenye duka anamwekekeza muuza duka nin cha kufanya. Hapa alikuwa anaeleza dhana ya chama kuiagiza serikali.
Msekwa amezeeka!... Ame loose kumbukumbu.
 
Nadhani hapa kunamkanganyiko maana Nepi naye kwenye mdaharo alikuwa anajigamba kuwa chama ndo kinaelekeza serikali cha kufanya na wakienda nje huwarejesha kwenye mstari.<br />
<br />
Kama haya yanayofanywa na serikali ya jk ndiyo maagizo na maelekezo ya chama basi chama cha magamba ndo kinachoipeleka nchi shimoni na kitalaumiwa milele. Siamini kama mwazo ua watu kama Nepi ndo yanayotuongoza sas hivi!
<br />
<br />
hapa Msekwa anajitoa. Hatak kuhusishwa ktk madudu ya serikal.
Au atuambie kuwa Mwenyekiti hataki ushaur wa chama.
 
Hawa magamba wanatuchanganya sana mkutano wa Nec juzijuzi hapa et wanaagiza serikali ipunguze bei ya mafuta yataa heeeeee? nisawa na mkono wakushoto kuagiza mkono wa kulia sasa hao watu wanatumia kichwa kufikiri kweli?
 
Mzee Msekwa umri unapita inawezekana hata mambo ya kawaida ya msingi anayasahau. Chama ndio kinaiagiza serikali kupitia ilani inayoitangaza wakati wa kamoeni, na kupitia wabunge ambao walikuwa wanaimba kuhusu ilani hiyo.

Hili ndilo jambo lililonishangaza na nikaanza kujiuliza kama mzee msekwa anastahili kuwepo kwenye safu ya uongozi wa ccm kwa sasa. Nadhani huyu mzee anastahili kuwa pembeni labda awe mshauri tu. Haiingii akilini kwamba chama kimenadi ilani halafu kiiachie serikali itekeleze bila maelekezo ya chama. Ama kwa kuwa viongozi wengi wa chama ndo hao hao wa serikali kwahiyo anaona kwamba chama hakiwezi kuiagiza serikali?

Nadhani hapa kunamkanganyiko maana Nepi naye kwenye mdaharo alikuwa anajigamba kuwa chama ndo kinaelekeza serikali cha kufanya na wakienda nje huwarejesha kwenye mstari.

Alichosema Nape juu ya chama kuielekeza serikali ni kitu sahihi. Chama ndicho kiliomba ridhaa kwa wnanchi, ndicho kinadeni na wananchi kutokana na manifesto yao kwahiyo lazima kiiagize na kuisimamia serikali yake.

Kama haya yanayofanywa na serikali ya jk ndiyo maagizo na maelekezo ya chama basi chama cha magamba ndo kinachoipeleka nchi shimoni na kitalaumiwa milele. Siamini kama mwazo ua watu kama Nepi ndo yanayotuongoza sas hivi!

Mkuu usisahau kwamba mwenyekiti wa ccm ndiye raisi kwahiyo kiongozi wa chama ndiye huyo huyo kiongozi wa serikali. Kwahiyo chama kimekuwa lege lege na hivyo ni lazima serikali nayo itakuwa lege lege.

Jana kwenye mdahalo Nape alisema kuwa rais ni kama muuza duka na chama ni wenye duka.
Mwenye duka anamwekekeza muuza duka nin cha kufanya. Hapa alikuwa anaeleza dhana ya chama kuiagiza serikali.
Msekwa amezeeka!... Ame loose kumbukumbu.

Lakini muuza duka (JK-Raisi) ndiye huyo huyo mwenye duka(JK-M/Kiti wa chama). Sasa inakuwaje muuza nduka anapokuwa ndiye mwenye duka?

<br />
<br />
hapa Msekwa anajitoa. Hatak kuhusishwa ktk madudu ya serikal.
Au atuambie kuwa Mwenyekiti hataki ushaur wa chama.

Yeah, huyu mzee bila shaka anajaribu kukinasua ccm kutokana na ulege lege wa serikali yao. Ye mwenyewe ambaye ni makamu mwenyekiti wa ccm bado pia ni mwenyekiti wa bodi mbalimbali za mashirika ya umma; Ngorongoro anayotuhumiwa kufanya ufisadi ikiwa mmojawapo.

Kama hakitoi kwa sirikali kitakuwa kinatoa kwa mafisadi

Mafisadi wenyewe wametapakaa kuanzia kwenye chama hadi serikalini!

Hawa magamba wanatuchanganya sana mkutano wa Nec juzijuzi hapa et wanaagiza serikali ipunguze bei ya mafuta yataa heeeeee? nisawa na mkono wakushoto kuagiza mkono wa kulia sasa hao watu wanatumia kichwa kufikiri kweli?

Na kwa kuwa wanaiagiza tu serikali bila chama kufanya uchambuzi wa kina na serikali inatekeleza maagizo ya chama bila kuyatafakari kwa umakini, tukaishia kupanga foleni za kununua mafuta hivi karibuni ili wao watuhadae kwamba serikali yao ni sikivu, matokeo yake ikaishia kuaibika vibaya.
 
Kweli huyu mzee amechoka na maana ya "chama kushika hatamu" wanalotambia ni nini kama hawawezi kutoa maagizo?
 
Kama chama hakiwez kumpa maagizo Kikwete nan atakayempa maagizo rais. Tumejua kuwa kwanin Rais anavurunda, tatizo ni chama kushindwa kumshaur. Chama hakijui majukum yake.
 
Ninasita kuchangia zaidi hasa kwa sisi ambao hatukuona kipindi hicho.

Kama kuna mtu aliifahamu vizuri maana ya Chama kushika hatamu kuliko hata Nyerere basi ni huyu Msekwa ambaye aliandika kitabu kabisa kuhusu principle ya Chama Kushika hatamu.

Leo, anaposema Chama hakitoi maagizo huku anaunganisha na dhana kwamba Chama hakishiki hatamu, maana yake ni kinyume na dhana yake iliyojaza journals siku zile.

Kwamba ideology ya Msekwa imebadilika. Kama ni kweli, basi nina mashaka na mleta mada ama hakumwelewa Msekwa, kwani kubadili ideology si rahisi kufafanuliwa kama mleta mada alivyoileta ambapo hata paragraph moja haikutimia!
 
wenyewe mnaona wanavyopandana kichwani..wewe umeona wapi Raisi anaarifiwa taarifa nyeti siku moja baada ya maamuzi kufanyika?!

wacha tumalizie mipango wataondoka mmoja baada ya mwingine....
 
wamepigwa kwenye mshono......yule mzee anadai eti ameborehsa ngoro ngoro wakati hakuna lolote.....mwizi mkubwa sana yule.....
 
jana kwenye mdahalo nape alisema kuwa rais ni kama muuza duka na chama ni wenye duka.
mwenye duka anamwekekeza muuza duka nin cha kufanya. Hapa alikuwa anaeleza dhana ya chama kuiagiza serikali.
Msekwa amezeeka!... Ame loose kumbukumbu.

haya maneno ya nape yamenitia faraja hata ninajua nini cha kutarajia kutoka serikalini,
kila siku nilikuwa nasugua kichwa inakuwaje wanauza nchi na mali asili zake kama marimao/machungwa
kumbe wako dukani

wakuu kuweni makini na kauli za nape ana maanisha
 
Salam wadau,
Nilikuwa naangalia kipindi cha medani za siasa na uchumi, cha startv ambapo mgeni mwalikwa alikuwa makamu mwenyekiti wa ccm bara ndg. Pius Msekwa.

Akijibu swali alilokuwa ameulizwa na mtangazaji wa kipindi ndg. Mwolekwa juu ya dhana ya chama kushika hatamu, Msekwa amesema sasa hivi chini ya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi chama hakiwezi kuiagiza serikali nini cha kufanya bali hilo ni jukumu la bunge na cabinet. Kwamba chama (ccm) kilikuwa kinatoa maagizo kwa serikali wakati wa mfumo wa chama kimoja.

Hivi karibuni baada ya ccm kutangaza kujivua gamba, katibu mwenezi wa chama hicho amekuwa akisikika mara kadhaa akisema kwamba chama (ccm) kimeiagiza serikali yake kufanya moja, mbili, tatu n.k
wadau mimi naona hizi ni statements mbili toka kwa viongozi wa juu wa chama kimoja lakini zinakinzana.

Naomba mawazo yenu.

Mkuu,hii ni kawaida ya serikali hii ya awamu ya nne....chini ya kijana JK....kuna mifano mingi ya kukinzana nakupa michache...
  1. Kikwete v/s Luhanjo(ishu ya Jairo)
  2. Kikwete v/s Magufuli(ishu ya bomoabomoa)
  3. Ewura v/s Ngeleja(ishu ya mafuta)
  4. Kikwete v/s Prof.Tibaijuka(uzio wa ubungo)
Hii ni mifano michache ya kutusaidia kutoshangaa kutofautiana kwa hawa magamba............
 
Huyu Msekwa kachoka wenzie wote wamepumzika kabaki yeye na Wasira. Chama ndio kinacho ongoza serikali kupitia manifesto yake na kinaiagiza serikali nini cha kufanya kwa mujibu wa manifest
 
wenyewe mnaona wanavyopandana kichwani..wewe umeona wapi Raisi anaarifiwa taarifa nyeti siku moja baada ya maamuzi kufanyika?!

wacha tumalizie mipango wataondoka mmoja baada ya mwingine....

Kama na wewe ni mwepesi kuamini hayo kwenye red basi nyinyi ndiyo mnaofanya humu paonekane kijiwe cha porojo badala ya ThinkTank.

Hii ndiyo taabu ya mitandao ambayo mnawasiliana bila kujua mwenzako ni calibre ya aina gani. Hivi wewe na akili yako unaweza kuamini porojo kwamba Luhanjo alipoenda kwenye media basi wewe umekuwa more informed figure than the president!

Kama huju kwamba president yoyote is the most informed person in the world nenda pale Butiama kwenye makumbusho ya Mwl. Nyerere. Utaona kuna redio yenye zaidi ya mitabend 24. Nyerere alikuwa anatembea nayo na alikuwa anakamata karibu kila station duniani.

Ukisoma maelezo unaambiwa kwamba alipewa zawadi toka Ujerumani mwaka 1962.

Leo unatuletea habari za wapuuzi kwamba Rais anashindwa kujua Publc imejulishwa nini tena na mtu alieko ofisi moja! Nimeyasoma hayo magazetini nikayapuuza lakini cha kushangaza inaonekana kuna wengi kama wewe mmepatikana wa kuamini porojo hiyo!

Kama ni kumpa likizo apishe uchunguzi wa bunge hilo ulitakiwa ulitegemee maana hujamsikia Kikwete akitutangazia kuwa Luhanjo kakosea.

Rudi kwenye mada ya Msekwa, toa hoja zitakazotufanya tui-miss JF tunapokatiwa umeme au coverage.
 
Tuyakumbuke maneno ya Prof. Lipumba "Kuna ombwe la uongozi ktk serikali ya CCM". huu ndio ukweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom